Ni wasanii wapi wa muziki unaowajua wanalazimisha fani?

Kwa sababu ney, tunda na msechu ni wasanii wazuri na wana awards wametuzwa mara nying na burudani Tanzania ina pande mbili mziki na soka kama huwajui wasanii wakali basi unawajua wanasoka wakali.
 
Huwa nashindwa kumwelezea nandy,!sijui shida ni nini,siwezi sema hana sauti nzuri,,!!ila kusema anajua kuimba ama hajui ni mtihani
Nkama ana aina Fulani ya uimbaji wa kufundishwa darasani.
Ni mawazo yangu
Mm sijawahi hata kuskia nyimbo zake, simjui
 
Paul Makonda[emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125]
 
Mi naona watu kama mmechanganya hapa.

Hoja ilikua ni wasanii gani wasiojua kuimba. Wanalazimisha fani.

Ila kwa uelewa wangu naona watu wengi wameandika wasanii wasio wapenda(wasio wakubali)

Kiukweli wapo wasanii wanaolazimisha fani nataona wengi wanatoa wimbo mmoja alafu wanapotea. . . wengine hata nyimbo zao hazi sikiki . kwenye kundi hilo ndio kuna wasanii wengi ambao wanalazimisha fani.
Japo wapo ambao wapo huko ila hawana bahati au hawajapata jinsi ya kutoka na kusikika. . . ili wapate kuingia kwenye ulimwengu huo.

Kuwa msanii (mwimbaji) mzuri unahitaji kuwa na package, ya kwanza na muhimu kulikozote ni kuwa na sikio la kusikia mziki, sauti ya kuimba na kujua kuimba, pili kujua kuandika mziki, nyimbo, na/au kujua kuusoma mziki, kuwa na mvuto wa kisanii etc. . .

Zipo sifa nyingi ila mimi naamini kubwa sana ni ile ya kwanza hizi nyingine unaweza ukazibypass na bado watu wakakusikia na kukuelewa.

Shida yetu au na ya wasanii wetu wanadhani kuwa msanii mwanamziki unatakiwa uandike lyrics mwenyewe. Utengeneze( compose) melody/ mziki wewe mwenywe, na uu imbe wewe mwenyewe.
Yaani wanataka the whole package awenalo mtu mmoja na afanye mtu mmoja.
Na sisi pia tunadhani kwamba kuwa mwanamziki ni kuwa na uwezo huo.

Ila sio sahihi. Naamini kaz inapo fanywa kwa ushirikiano na watu zaidi ya mmoja inakua bora zaidi na ya kuvutia.

Hivyo hata mimi kuna wanamziki nisio wapenda au hata sipendi baadhi ya nyimbo zao ila nawakubali ni wanamziki wazuri. . .
 
Wapo wengine pia kweli huwa siwaelewi. Labda kweli hawa watakua wamevamia fani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…