Ni wasanii wapi wa muziki unaowajua wanalazimisha fani?

Ni wasanii wapi wa muziki unaowajua wanalazimisha fani?

Japo umesema hajui muziki lakini mi hizi ngoma nazikubali sana,
1.Tundaman ft. Chid Benz-Neilah
2.Tundaman & JI- Nipe Ripoti
Yaani we jamaa Wenger kakuchanganya kweli kweli...

Hiyo Ngoma ya Nipe Ripoti JI katokea wapi?!

Humo kuna C Pack na Mtu mzima Madee.
 
Tunda Man
anajua sana jamaa Ana Hit song nyingi sana kutoka Neila,Nipe Ripoti,Starehe gharama mpaka Msambinungwa.
ila ngoma zake za siku hizi zipo chini sana pengine kichwa kimechoka kuandika.Mtoe huyu jamaa

Peter Msechu
Anajua kuimba ila hajui kuandika nyimbo....kitu kizuri amejua kosa lake siku hizi watu wanamuandikia nyimbo na anaimba vzuri tu mfano nyimbo kama "Nyota" aliyofanya na Amini ni nyimbo nzuri.Umemuonea huyu bonge

Ney Wa Mitego
Anajua anachokifanya ndio maana yupo pale.Anajua kabisa hana kipaji kikubwa cha kuandika wala kuchana ila alijiweka karibu na Diamond wakafanya ngoma...jamaa ni mfanya biashara na ile kuwa mchanga inampa ujanja Wa kutafuta pesa.Huyu hafai kuwa kwenye list


Hapo labda ningemuweka
-Abdu Kiba
-Queen Darleen
-Q Boy Msafi
 
Back
Top Bottom