Ni watekaji wa Chaula ama ni matapeli ndio walitaka 3 milioni wamuachie?

Ni watekaji wa Chaula ama ni matapeli ndio walitaka 3 milioni wamuachie?

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Kuna mchezo kama si wa kijinga basi ni wa kitoto unachezeka hapa..!
Watekaji mahiri hukuteka kwa lengo maalum kama si kisasi basi ni mambo ya kisiasa ama kikomboleo (ransom)

Sakata la Shadrack kwa mazingira yote ni la kisiasa.. Ni kijana fukara hana visasi na watu wanaoweza kumteka..labda kama kisasi kitokane na yeye kulipiwa faini na watanganyika wenzake kwenye kesi iliyokuwa inamkabili

Alilipiwa faini na akatolewa gerezani na mambo yakaishia hapo.. Lakini mara ghafla akatekwa na kupotea kusikojulika licha ya kelele zote kila kona ya nchi. Baba yake mzazi alishaomba apewe hata kama ni maiti ya mwanae amzike kama imeshindikana kumrudisha, lakini bado imeshindikana.

Sasa hivi karibuni kuna watu wamempigia baba yake wakimtaka awapatie milion 3 ili wamrudishe mwanae(pengine akiwa hai) Sasa hapa kuna maswali ya kujiuliza

Hawaogopi police? Hawaogopi kujulikana? Mbona hawakumpa masharti yoyote kama ya kutoripoti polisi?

Cha kushangaza zaidi baba mtu kaenda polisi, katoa taarifa na mawasiliano yote.. Lakini hakuna kilichofanyika hadi sasa
Je ni watekaji wenyewe ama ni matapeli walitaka kumpiga Mzee wa watu hela?

Soma Pia: Baba Chaula: Nimepigiwa simu na namba ngeni, kaniambia nitoe Tsh. Milioni 3 ili Chaula apatikane

20240902_111150.jpg
 
Huo ni mchezo. Wamemuua wanataka kupata mpenyo kuwa issue yake haina uhusiano na mambo ya siasa.
Hata mtoto wa drs la pili huwezi kumzunguka kwa game kama hii.
Ukae naye mtu wiki 3 , gharama za kumtunza ni zaidi ya millioni 3 waliyoiomba.
Vyombo vya habari vilivyopromote vimelipwa.
Possibility ya kuwa hai huyo kijana ni 15%
 
Baba mtu katoa taarifa polisi, tayari magazeti na polisi bila kujua athari yake wameshapost.
Polisi baada ya kupata taarifa wangefanya uchunguzi na kutoa taarifa.
Hapo ndio tunahoji Kama hukumu ya mahakama ilikuwa sahihi.
Uchunguzi wa nini huku hii ni drama ili kuwahadaa wajinga kuwa hakutekwa kisiasa. I hope wamemuua wametengeneza script ya kijinga
 
Vijana kma unaweza kuruka dimbwi la tope liruke tu usitake ukanyage tope halafu ukafue kisa unajua kufua vizuri
Mambo mengine vijana tunajitakia wenyewe
 
Kuna mchezo kama si wa kijinga basi ni wa kitoto unachezeka hapa..!
Watekaji mahiri hukuteka kwa lengo maalum kama si kisasi basi ni mambo ya kisiasa ama kikomboleo (ransom)

Sakata la Shadrack kwa mazingira yote ni la kisiasa.. Ni kijana fukara hana visasi na watu wanaoweza kumteka..labda kama kisasi kitokane na yeye kulipiwa faini na watanganyika wenzake kwenye kesi iliyokuwa inamkabili

Alilipiwa faini na akatolewa gerezani na mambo yakaishia hapo.. Lakini mara ghafla akatekwa na kupotea kusikojulika licha ya kelele zote kila kona ya nchi. Baba yake mzazi alishaomba apewe hata kama ni maiti ya mwanae amzike kama imeshindikana kumrudisha, lakini bado imeshindikana.

Sasa hivi karibuni kuna watu wamempigia baba yake wakimtaka awapatie milion 3 ili wamrudishe mwanae(pengine akiwa hai) Sasa hapa kuna maswali ya kujiuliza

Hawaogopi police? Hawaogopi kujulikana? Mbona hawakumpa masharti yoyote kama ya kutoripoti polisi?

Cha kushangaza zaidi baba mtu kaenda polisi, katoa taarifa na mawasiliano yote.. Lakini hakuna kilichofanyika hadi sasa
Je ni watekaji wenyewe ama ni matapeli walitaka kumpiga Mzee wa watu hela?

Soma Pia: Baba Chaula: Nimepigiwa simu na namba ngeni, kaniambia nitoe Tsh. Milioni 3 ili Chaula apatikane

View attachment 3084882
Vibaka..
 
Vijana kma unaweza kuruka dimbwi la tope liruke tu usitake ukanyage tope halafu ukafue kisa unajua kufua vizuri
Mambo mengine vijana tunajitakia wenyewe
Wengi wakiwa na mtazamo kama huu uonevu hautakaa uishe hapa nchini
 
Kwa ulinzi alionao Chaula, mabaya kumpata, labda Mungu mwenyewe aruhusu.
 
Yote yanawzekana, kuwa ni hao walinzi wa watu na mali zao au kuwa ni wahuni tu, ila hili kundi la kwanza lipe asilimia nyingi.

Huyo mzazi wa chaula, kama ni mtu wa asili ya kyela ninaowajua, hao watekaji wataisha wao na vizazi vyao.

Labda let's see.
 
Back
Top Bottom