Ni wazi Zitto Kabwe na ACT Wazalendo wamepotea

Naanto Mushi

JF-Expert Member
Joined
Oct 16, 2015
Posts
6,236
Reaction score
15,677
Ama niseme hiki chama cha ACT Wazalendo au mwenyekiti wake Zitto Kabwe ni kama wameshakubali kushindwa siasa za Tanzania, au niseme tu labda wamepoteza mwelekeo.

Nikiri kwamba kati ya miaka ya 2016 mpaka 2019, Zitto alikuwa mwanasiasa active sana, na mimi mwenyewe ilikuwa ni mojawapo ya watu ilikuwa kila siku namfuatilia kwa karibu sana hususana twitter.

Ila nikaja kushangaa ghafla, anaanza kujiita mwanaharakati wa Tigray, hapo ndo nikaona huyu ameshapotea kwenye siasa za Tanzania na baada ya hapo na kuendelea yaani kuanzia mwaka 2020 mpaka leo hii, sijawah kumfuatilia tena Zitto Kabwe kwa karibu, nimehisi ya kwamba amepoteza relevance. Na hata na hivo kwa hii miaka 2 sijaona kama Zitto yupo series kufanya siasa za kiushindani tena.

Ukija kwa chama chake ACT Wazalendo, napo strategy ni hiyo hiyo. Hakuna relevance, hapa kati kwenye issues za bandari sijawasikia kabisa. Issue za Ngorongoro na wamasai pia sijawasikia.

Kwasababu mimi ninachoamini, ukijiita chama cha siasa, inatakiwa usimamie kwenye issues za kitaifa na uoneshe msimamo thabiti wa chama chako kwenye hiyo issue.

Asa kwa ACT na Zitto sijaona kwa hiki kipindi cha miaka 3 kama wamekuwa wanafanya mapambano kama wenzao wa CHADEMA.

ACT na Zitto waamshwe, naona kama wamepotea!

N. Mushi
 
Ama niseme hiki chama cha ACT Wazalendo au mwenyekiti wake Zitto Kabwe ni kama wameshakubali kushindwa siasa za Tanzania, au niseme tu labda wamepoteza mwelekeo.

Naatombe mushi, so unasema una miaka 2 humfuatilii Zitto ila unajua kuwa she kuhizi zitto kapotea .are serious

USSR
 


Unaongeaje na chakula mdomoni?
 
Ukata wanajipanga.

Othman anabana mno licha ya kuwa kwenye SUK
 
DHAMBI YA USALITI KWA UPINZANI WA DHATI INAMTAFUNA
 
Umesema umewacha kumfuatilia, suala la bandari wameshasema wanaunga mkono uwekezaji hawaungi mkono wenye kupinga , pili Act sio chama cha kudandindia matukio kama wale wengine wasio na jina!
 
Hawezi kumkosoa mtu wa Imani yake,ngoja Mgalatia aingie Ikulu utadhangaa.

Hili tatizo si la Zitto pekee yake hata yule CAG aliyestaafishwa na Magufuli ana ujinga huu huu.
 
Kibaraka Zitto yupo sana, anasubiri 2025 tu aanze kugombana na vyama vya upinzani ili kuipa ushindi tena CCM, subirini mtaona!
 
Zitto shida yake na kifo chake ni kutokana na udini mkubwa alionao, zitto ni mdini mno na hafai kabisa!
 
Kwanini unapoteza muda kumjadili mtu aliyepotea?

Zitto kaondolewa Chadema tangia 2013, miaka 10 sasa bado mnamjadili?

Mmeshindwa ku-move on naye mkamwacha na upotevu wake?
 
Zitto ana muda sasa toka ameacha kuwa na AKILI na ameshindwa kabisa kujitafakari kwa Akili hakuna.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…