Nichagulieni gari kwa bajeti ya Milioni 10

Nichagulieni gari kwa bajeti ya Milioni 10

Shikamoni waheshimiwa,
Mimi sijawahi kumiliki gari tangu nizaliwe.

Kazi yangu ni kuuza duka la Mangi. Kipato changu ni wastani wa Laki 5 kwa mwezi (hakiko imara kabisa; kinaweza kupungua au kuongezeka kidogo kutegemea na hali ya biashara).

Nimedunduliza hela kwa miaka miwili nimepata milioni kumi. Lengo langu nipate gari la kutembelea mjini na mimi.

Sasa ninachoomba waheshimiwa, Nichagulieni gari kwa kuzingatia kipato changu hapo juu.

Kuna watu wataniuliza maswali ya kitaalamu hapa, Mara Injini silinda sita, mara cc za mafuta, Mimi sina ujuzi huo.

Mimi ninachotaka mnichagulie gari dogo lolote, Mimi nitaendesha tu ili mradi litoke Japan na mpaka kulipia gharama zote na kuanza kuliendesha kwa uhuru isizidi kiasi tajwa hapo juu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu mimi kuna sehemu umeniacha kidogo.
10M kwa miaka 2 inamaanisha ni zaidi ya laki 4 kwa mwezi na wewe kipato chako ni laki 5 kwa mwezi. Maana yake unafanya saving zaidi ya 80%. Au hiyo laki 4 ipo nje ya laki 5 kwa mwezi??? Kama unauwezo wa kusave 80% ingependeza kutupa technics unazotumia maana inaweza kuwafaidisha wengi sana.

Tukirudi kwenye mada kuu, maana yake unauwezo wa kutumia 400k bila kuharibu mambo yako mengine.
Hivyo basi nakushauri ununue ist kama wengi walivyoshauri.
Kama utaamua kuagiza unaweza tembea mitandao ya bf, sbt, tcv n.k
1. Angalia cif +
2. Makadirio ya tax tra +
3. Port & bima ~ 300000
Ukishalipata kuna gharama za ziada za kijinga kuwa makini nazo (kuchora vioo, reverting, tint, alarm nk).
Mwisho kuwa makini barabarani, ukiachana na ukweli kuwa usalama wako ni muhimu sana pia unaweza ukajikuta unaingia katika mikono ya wazee wa fedha au mafundi ya garage bila sababu za msingi
 
Mkuu mimi kuna sehemu umeniacha kidogo.
10M kwa miaka 2 inamaanisha ni zaidi ya laki 4 kwa mwezi na wewe kipato chako ni laki 5 kwa mwezi. Maana yake unafanya saving zaidi ya 80%. Au hiyo laki 4 ipo nje ya laki 5 kwa mwezi??? Kama unauwezo wa kusave 80% ingependeza kutupa technics unazotumia maana inaweza kuwafaidisha wengi sana.

Tukirudi kwenye mada kuu, maana yake unauwezo wa kutumia 400k bila kuharibu mambo yako mengine.
Hivyo basi nakushauri ununue ist kama wengi walivyoshauri.
Kama utaamua kuagiza unaweza tembea mitandao ya bf, sbt, tcv n.k
1. Angalia cif +
2. Makadirio ya tax tra +
3. Port & bima ~ 300000
Ukishalipata kuna gharama za ziada za kijinga kuwa makini nazo (kuchora vioo, reverting, tint, alarm nk).
Mwisho kuwa makini barabarani, ukiachana na ukweli kuwa usalama wako ni muhimu sana pia unaweza ukajikuta unaingia katika mikono ya wazee wa fedha au mafundi ya garage bila sababu za msingi
Nikipata hela ya mauzo, natunza 15,000/= kila siku mkuu.

Zaidi ya hiyo sina chanzo kingine cha kipato.

Hiyo IST nitaizingatia, ila kuna waheshimiwa humu wameshauri kuwa kwa hiyo bajeti yangu ni vema niongeze kama Milioni 1.5 ya emergency,
Hivyo yabidi nidundulize tena mpaka mwezi Machi ili kuongeza hicho kiasi tukijaaliwa uzima.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani maisha ni mpaka ghorofa mzee????

Hata kwa hivi vya kawaida tu tunapeana ushauri..
Hata hao wenye maghorofa walianza na nyumba za makuti.......Usijione una ka gari kako , jumapili umavaa kapensi unazungusha kafunguo basi ukaijiona maisha ndo ushayapatiaaa......mwehu wewe

Sent using Jamii Forums mobile app
Kaomba ushauri wa gari we unamshauri biashara.Nadhani we ulikuwa offpoint

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu kijana kaomba ushauri aina gani ya gari Anunue lakini kuna watu wanamwambia hafanye biashara Come on watanzania
 
Mkuu ni mwaka sasa na siku mbili tangu uanzishe huu uzi....vipi ulifanikiwa kupata gari..
Daah Mangi aliona avute zake Pikipiki tu mzee baba.
Screenshot_2020-12-25-16-24-41-1.jpg
 
Biashara kubwa ninayoifikiria kwa hali yangu ni ya duka kubwa la dawa za binadamu, na ikiwezekana niwe nayo hata mawili, mjini 1 na kijijini 1.

Mtaji ni kuanzia Milioni 15,
Changamoto kubwa kwangu ni elimu ya hiyo biashara, na nilijaribu kumuulizia mtu anayefanya hiyo biashara yeye ana maduka ya dawa manne na ni daktari,
Kwa kuwa sina mazoea naye akaniambia kwa kifupi tu kuwa kwa kuwa mimi sina elimu hasa ya masuala ya dawa, itanipa shida sana kwenye usimamizi, kwani nitategemea kuwaajiri watu wanaojua.




Sent using Jamii Forums mobile app
Duka la dawa utahitaji mfamasi asajiliwe kwa ajili ya duka lako. Utamtafuta mtakubaliane umlipe kiasi fulani kutumia cheti chake.
 
Duka la dawa utahitaji mfamasi asajiliwe kwa ajili ya duka lako. Utamtafuta mtakubaliane umlipe kiasi fulani kutumia cheti chake.
Hivi hii sio kosa kisheria?
Na ikitokea shida kwa hilo duka mwenye cheti atakuwa salama?
 
Back
Top Bottom