TATACHACHA
JF-Expert Member
- Jun 16, 2022
- 793
- 1,671
Mamlaka ya vitambulisho vya taifa tanzania ( NIDA) sidhani kama walikuwa na lengo la kukamilisha mradi huu kwa wakati,
Nahisi kuna watu ndani ama nje ya idara hii kwa makusudi na kwa malengo yao binafsi wanayoyajua wao wanaosababisha kadhia hii iendelee kwa makusudi kabisa.
Urasimu huu unakuja hasa kutokana na kitambulisho hichi ama namba kuhitajika sehemu mbali mbali hasa katika kupata ajira mahali fulani, na hii sheria imeletwa na serikali yenyewe huku ikijua kabisa haijajipanga kikamilifu( kiteknolojia) kumalizia kadhia hii kwa wananchi.
Haiingii akilini zoezi lilioanza kiujumla kwa nchi nzima zaidi ya miaka mitano iliyopita, mpaka sasa bado watu hawajapata namba wala vitambulisho kweli!?
Nimekwisha kuijaribu hii system yao ya kufetch NIN number online pia nikiwa na details Kamili na vitambulisho vitatu tofauti ( halali kabisa!) Na hakuna details iliyokosewa. Lakini inaleta msg " unable to fetch nin number!" What a hell!
Ni system gani ya kipuuzi hii inayoshindwa kutambua hata kitambulisho ilichokitengeneza yenyewe!?
....inachekesha na kusikitisha sana!...
Kisingizio kimekuwa kile kile eti " vinachapishwa kwa awamu!" Nonsense!
Kwa sasa vijana wanaoomba ajira kwenye kampuni yoyote kigezo cha kwanza ni kuwa na NIN number, na hii imepelekea urasimu ofisi za NIDA wilaya hasa hapa nilipo, kupata NIN number kwa haraka bila kuwa na 30k-50k kuendelea ndipo unapewa NIN kwa haraka. Imegeuzwa mradi kama urasimu uliopo kwenye kupata leseni ya udereva na hati ya kusafiria.
Mamlaka hii akiwemo mkurugenzi wake inapaswa kujipima, kujitathmini kama kweli inatosha kuwahudumia wananchi.
Nahisi kuna watu ndani ama nje ya idara hii kwa makusudi na kwa malengo yao binafsi wanayoyajua wao wanaosababisha kadhia hii iendelee kwa makusudi kabisa.
Urasimu huu unakuja hasa kutokana na kitambulisho hichi ama namba kuhitajika sehemu mbali mbali hasa katika kupata ajira mahali fulani, na hii sheria imeletwa na serikali yenyewe huku ikijua kabisa haijajipanga kikamilifu( kiteknolojia) kumalizia kadhia hii kwa wananchi.
Haiingii akilini zoezi lilioanza kiujumla kwa nchi nzima zaidi ya miaka mitano iliyopita, mpaka sasa bado watu hawajapata namba wala vitambulisho kweli!?
Nimekwisha kuijaribu hii system yao ya kufetch NIN number online pia nikiwa na details Kamili na vitambulisho vitatu tofauti ( halali kabisa!) Na hakuna details iliyokosewa. Lakini inaleta msg " unable to fetch nin number!" What a hell!
Ni system gani ya kipuuzi hii inayoshindwa kutambua hata kitambulisho ilichokitengeneza yenyewe!?
....inachekesha na kusikitisha sana!...
Kisingizio kimekuwa kile kile eti " vinachapishwa kwa awamu!" Nonsense!
Kwa sasa vijana wanaoomba ajira kwenye kampuni yoyote kigezo cha kwanza ni kuwa na NIN number, na hii imepelekea urasimu ofisi za NIDA wilaya hasa hapa nilipo, kupata NIN number kwa haraka bila kuwa na 30k-50k kuendelea ndipo unapewa NIN kwa haraka. Imegeuzwa mradi kama urasimu uliopo kwenye kupata leseni ya udereva na hati ya kusafiria.
Mamlaka hii akiwemo mkurugenzi wake inapaswa kujipima, kujitathmini kama kweli inatosha kuwahudumia wananchi.