NIDA VS UHAMIAJI: Ukikamilisha taratibu zote, unapata passport baada ya wiki 2. NIDA wao unapata kitambulisho baada ya Mwaka au zaidi

NIDA VS UHAMIAJI: Ukikamilisha taratibu zote, unapata passport baada ya wiki 2. NIDA wao unapata kitambulisho baada ya Mwaka au zaidi

Mwanamaji

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
2,905
Reaction score
4,518
Habari zenu wakuu.

Kwa kadri miaka inavyosogea, ndivyo mahitaji ya huduma za haraka na zenye ufanisi yanaongezeka.
"Being Quick, Efficient and Consistent is being Good"
Kasi ya maisha ya mwaka 1980 haiwezi kuwa sawa na ile ya 2020.

Katika taratibu za kawaida za kazi, kuanzia siku ambayo utakua umekamilishia taratibu zote (umepiga picha na kuchukuliwa fingerprints) pale uhamiaji, unapewa passport yako baada ya wiki mbili.

Kwa upande mwingine, kuanzia siku ambayo umekamilisha taratibu zote (umepiga picha na kuchukuliwa fingerprints) pale NIDA, itakuchukua Mwaka mmoja, hadi miwili au awamu nzima (miaka mitano) kupata kitambulisho chako.

Mnaojua hebu tujuzeni na sisi, kwani kuna ugumu gani kutengeneza kitambulisho cha taifa ukilinganisha na ugumu uliopo kwenye kutengeneza passport ?

Pili, ukishakamilisha "taratibu zote" pale NIDA, unapewa wiki tatu ili upate namba ya NIDA (NIN) ? How comes a computerised system generates "numbers" at such a slow pace ?
Yaani siku zote 21 namba tu ?

Tatu, uki "renew" kadi yako (baada ya ile ya awali kupotea au kuharibika, n.k), inaweza kukuchukua miezi sita hadi mwaka kuipata tena, mara baada ya kukamilisha taratibu zote.
Na hii ni hata kama haubadilishi chochote katika taarifa zako.
Yaani ku "reprint" tu, utasubiri miezi sita hadi mwaka.

Tusiwe wasiri, kuna ugumu upi ?

Juzi hapa "tumesaini" mkataba wa ujenzi wa reli ya SGR kutoka Makutupora kuelekea Tabora, kwa mtu ambaye alijiandikisha NIDA siku hiyo, anaweza kujikuta anapanda treni ya umeme kutoka Makutupora kuelekea Tabora akiwa hana kadi yake ya NIDA kwenye wallet (bado haijatoka).
 
Hawa jamaa wa NIDA ni kiboko, nilikwenda kwaajili ya kurekebisha jina mwaka juzi mwezi wa 9, huo mlolongo niliopewa hadi kukamilisha ilikuwa ni cha moto.

Nilifika mahakama ya ardhi kwaajili ya DEEP POLL hii unasubiri wiki 2 hadi itangazwe gazeti la serikali baada ya hapo nikarudi tena huko NIDA ku submit supportive evidences za jina ikiwemo hiyo DP, cheti cha kuzaliwa, vivuli vya card ya bank, passport, card ya mpiga kura, barua ya M/kiti wa mtaa, pamoja na kufanya malipo yote yaliyotakiwa kupitia control number nilizopewa n.k. Leo tayari ni mwaka na miezi kibao hakuna card wala taarifa yoyote nimekwenda tena huko juzi naambiwa mchakato wako bado.

Kwa kweli inashangaza sana card ya mpiga kura ni siku hiyohiyo chap kwa haraka hii ya vitambulisho inachukuaje miaka kibao! I really wonder
 
Wakati mwingine serikali ikubali hata kushirikiana na sekta binafsi ili kuongeza ufanisi. Wao wangefanya usajili na uhakiki, wacha kampuni binafsi zifanye printing, halafu tuone kama kungekuwa na huu utopolo wa kitambulisho kuchukua miaka 5.

Makampuni ya simu yangekuwa ni NIDA, account za Mpesa zingekuwa zinachukua miaka 2 kuanza kazi
 
Kadi ya mpiga kura inatoka siku hiyo hiyo baada ya kujaza fomu na picha + fingerprints [emoji3] = MASLAHI YA KUTUMIWA KISIASA....
Sasa kadi ya NIDA haina maslahi kwa mwana siasa hivyo kwao haina maana...
Mimi since 2018, leo mwaka wa 5 huu sina NIDA, nisinge print online copy na kuifanya hardcopy leo ningekuwa nasota
 
Hawa jamaa wa NIDA ni kiboko, nilikwenda kwaajili ya kurekebisha jina mwaka juzi mwezi wa 9, huo mlolongo niliopewa hadi kukamilisha ilikuwa ni cha moto. Nilifika mahakama ya ardhi kwaajili ya DEEP POLL hii unasubiri wiki 2 hadi itangazwe gazeti la serikali baada ya hapo nikarudi tena huko NIDA ku submit supportive evidences za jina ikiwemo hiyo DP, cheti cha kuzaliwa, vivuli vya card ya bank, passport, card ya mpiga kura, barua ya M/kiti wa mtaa, pamoja na kufanya malipo yote yaliyotakiwa kupitia control number nilizopewa n.k. Leo tayari ni mwaka na miezi kibao hakuna card wala taarifa yoyote nimekwenda tena huko juzi naambiwa mchakato wako bado. Kwa kweli inashangaza sana card ya mpiga kura ni siku hiyohiyo chap kwa haraka hii ya vitambulisho inachukuaje miaka kibao! I really wonder
Ukijiangalia kwa undani, hilo suala lako ni la kuisha ndani ya wiki moja.
Sasa wao wanachukua muda kana kwamba wanatengeneza silaha za nyuklia au wanajenga Uwanja wa ndege.

Hii ni taasisi cheleweshi.
 
Wakati mwingine serikali ikubali hata kushirikiana na sekta binafsi ili kuongeza ufanisi. Wao wangefanya usajili na uhakiki, wacha kampuni binafsi zifanye printing, halafu tuone kama kungekuwa na huu utopolo wa kitambulisho kuchukua miaka 5.

Makampuni ya simu yangekuwa ni NIDA, account za Mpesa zingekuwa zinachukua miaka 2 kuanza kazi
Wazo zuri sana umetoa. Kazi ya NIDA ingepaswa kuishia kwenye kusajili, kuhakiki na kutunza database.

Kuprint wapewe sekta binafsi. Mambo yangekua yanakwisha chap chap
 
Kadi ya mpiga kura inatoka siku hiyo hiyo baada ya kujaza fomu na picha + fingerprints [emoji3] = MASLAHI YA KUTUMIWA KISIASA....
Sasa kadi ya NIDA haina maslahi kwa mwana siasa hivyo kwao haina maana...
Mimi since 2018, leo mwaka wa 5 huu sina NIDA, nisinge print online copy na kuifanya hardcopy leo ningekuwa nasota
Hata leseni za udereva zinatoka kwa muda mfupi, NIDA sijui wanatuonaje yaani...
 
Wazo zuri sana umetoa. Kazi ya NIDA ingepaswa kuishia kwenye kusajili, kuhakiki na kutunza database.

Kuprint wapewe sekta binafsi. Mambo yangekua yanakwisha chap chap
Tatizo watu wa serikali, inefficiency haijawahi kuwaumiza. Kwani kuna mtu amewahi kukosa mshahara kwa sababu kitambulisho kimechelewa? Lakini mtu wa private, akipewa target zake, tunataka vitambulisho kadhaa kila siku, utaniambia speed watakayokuwa nayo. Maana wanajua, huko ndiko pesa zao zinatoka.
 
Kadi ya mpiga kura inatoka siku hiyo hiyo baada ya kujaza fomu na picha + fingerprints [emoji3] = MASLAHI YA KUTUMIWA KISIASA....
Sasa kadi ya NIDA haina maslahi kwa mwana siasa hivyo kwao haina maana...
Mimi since 2018, leo mwaka wa 5 huu sina NIDA, nisinge print online copy na kuifanya hardcopy leo ningekuwa nasota
mkuu unasema ukweli ila kitambulisho changu cha Taifa nilikipata ndani ya mwezi. Baada ya Kukamilisha taratibu zote mwezi wa 9 tarehe 31, 2018 nikapigwa picha . Tarehe iyo iyo October, 2018 nilienda kukichukua.
 
Kwa uhamiaji sio wiki mbili, ni wiki 1 tuu unamiliki passport yako ya kielektroniki. Mimi nilipeleka maombi mkoani nilipo na hazikutimia wiki mbili nikapigiwa simu kua pass ipo tayari nikachukue.
 
Back
Top Bottom