Nida

Nida

kasinge

JF-Expert Member
Joined
May 22, 2011
Posts
1,259
Reaction score
319
Ebana wadau wana jf, hii siyo tetesi, bali nina ushahidi, NIDA wanaitana kwa kujuana. Nina jirani yangu mmoja ameitwa interview tayari. Nilimuuliza ali-aply lini akasema wala hakuwahi apply, alipigiwa simu, akaenda hata interview hakufanyiwa, akaambiwa ataitwa kwa training any time.
Akasema kuna mmmmangi mmoja kamuunganisha, si unajua kigogo wa nida ni Mmmmangi.
Hii ni kasoro kubwa kwa nida ambayo ilikuwa criticised, afu inaanza na haka ka mchezo kachafu.
Take care.
 
mhh hii hatari, na zile post za kimya kimya ambazo watu walikuwa wakipigiana cm, mi nilipeleka lakin nikaambiwa wengine walipokuwa wakipeleka application walifanyiwa interview palepale.du yote maisha ila tutashinda.
 
Ebana wadau wana jf, hii siyo tetesi, bali nina ushahidi, NIDA wanaitana kwa kujuana. Nina jirani yangu mmoja ameitwa interview tayari. Nilimuuliza ali-aply lini akasema wala hakuwahi apply, alipigiwa simu, akaenda hata interview hakufanyiwa, akaambiwa ataitwa kwa training any time.
Akasema kuna mmmmangi mmoja kamuunganisha, si unajua kigogo wa nida ni Mmmmangi.
Hii ni kasoro kubwa kwa nida ambayo ilikuwa criticised, afu inaanza na haka ka mchezo kachafu.
Take care.

Boss wangu sishangai unapowataja hawa jamaa akina mangi ni hatar sana na ndo mchezo huo huo wanaoufanya TRA wanaweka vigezo vya ajabu km upper 2nd ni ya nini kwa mfanyakazi anaekamata bidhaa za magendo km zaman hizo kazi zilikuwa zinafanywa na watu wa kidato cha nne tu leo hii graduate wa kawaida unamwona hawezi hiyo kaz,na serikali ikiendelea kuwalea hivyo nchi hii haitaendelea kwani wanalindana mtu na mdogo wake hakuna wa kufichua uozo.wanjiwekea malengo ya chini ya kukusanya kodi ili mwisho wa siku waonekane wamevuka makisio kutulaghai kumbe pesa nyingi za nchi zinaishia mifukoni mwao!
 
Kaka sio Nida Peke yake. Nothing is based on qualifications any more. Sijui udaktari, pilot, Tanesco, Mikataba ya madini, Mahakimu na ................. endelea mwenyewe. Nchi inaelekea pabaya. NA SIO KINAMANGI PEKE YAO. This is a serious problem.
 
Kaka sio Nida Peke yake. Nothing is based on qualifications any more. Sijui udaktari, pilot, Tanesco, Mikataba ya madini, Mahakimu na ................. endelea mwenyewe. Nchi inaelekea pabaya. NA SIO KINAMANGI PEKE YAO. This is a serious problem.


Sio "nchi inaelekea pabaya" bali ni NCHI IMESHAFIKA PABAYA
 
Shida ni kuwa kazi ziko chache. kwa mfano nafasi iko moja, ukitangaza wanaomba watu 2,000. kati ya hao, 100+ wote wana meet vigezo. Utamchagua nani na kumuacha nani? so kigezo cha ziada au mbinu ya ziada lazima itumike. Wa kulaumiwa ni mwenye kaya na wenzake ambao wametuahidi kuongeza ajira 1m wakati hata mazingira ya kujiajiri tu wanashindwa kuyatengeneza. basi walau wakusanye kodi kwenye migodi ili wale wasio na kazi wawe wanalipwa unemployment benefits.
 
Mmh sasa wasio na marefa ctutaumia lakini ndo Bongo hiyo kila kitu kinachakachuliwa
 
jaman hvyo ndivyo hali ilivyo sasa kwny soko la ajira.. Kwa jinsi 2navyotaabika hv ndoo maana 2naishia kuwa mafisadi 2 cc watoto wa wakulima.
 
Boss wangu sishangai unapowataja hawa jamaa akina mangi ni hatar sana na ndo mchezo huo huo wanaoufanya TRA wanaweka vigezo vya ajabu km upper 2nd ni ya nini kwa mfanyakazi anaekamata bidhaa za magendo km zaman hizo kazi zilikuwa zinafanywa na watu wa kidato cha nne tu leo hii graduate wa kawaida unamwona hawezi hiyo kaz,na serikali ikiendelea kuwalea hivyo nchi hii haitaendelea kwani wanalindana mtu na mdogo wake hakuna wa kufichua uozo.wanjiwekea malengo ya chini ya kukusanya kodi ili mwisho wa siku waonekane wamevuka makisio kutulaghai kumbe pesa nyingi za nchi zinaishia mifukoni mwao!

nafasi ni chache walioomba ni wengi zaidi ya 10,000+ unategemeaje lazima tuweke vitu vya ziada kuwapunguza inabidi kidogo ujutie ule mchezo uliofanya ukapata lower class au pass vinginevyo tutalalamika bila sababu. kwa Tz tunaamini aliyefaulu mtihani ndio mwenye uwezo zaidi(ingawa siyo lazima ikawa hivyo) ni bora uwe na 1st au uper second chance ya kukosa inakuwa ndogo.
 
nafasi ni chache walioomba ni wengi zaidi ya 10,000+ unategemeaje lazima tuweke vitu vya ziada kuwapunguza inabidi kidogo ujutie ule mchezo uliofanya ukapata lower class au pass vinginevyo tutalalamika bila sababu. kwa Tz tunaamini aliyefaulu mtihani ndio mwenye uwezo zaidi(ingawa siyo lazima ikawa hivyo) ni bora uwe na 1st au uper second chance ya kukosa inakuwa ndogo.
Angalia, sio wote wanaopata lower second walifanya mchezo. Imagine mtu anaekaa mtaani ambako lazima ajipikie, akachote maji na shuguli nyingine za home. Usije ukajilinganisha nae hata ka una upper second kitaa kugumu bwana. Big up waajiri wote wasiotaja ma upper second. Kuhusu nida, hiyo system ipo tangu enzi za mwalimu, kinachotakiwa ni ku-fight kuiua. Sometimes wanatuepusha na matatizo kama ya UDOM.
 
nafasi ni chache walioomba ni wengi zaidi ya 10,000+ unategemeaje lazima tuweke vitu vya ziada kuwapunguza inabidi kidogo ujutie ule mchezo uliofanya ukapata lower class au pass vinginevyo tutalalamika bila sababu. kwa Tz tunaamini aliyefaulu mtihani ndio mwenye uwezo zaidi(ingawa siyo lazima ikawa hivyo) ni bora uwe na 1st au uper second chance ya kukosa inakuwa ndogo.
Jino kwa jino, hiyo avata yako huwa inaniacha hoi sana (inanibamba mazee). Nahisi inafanana na ukweli. Ila ungekuwa mrefu kidogo nadhani hata mawazo yangepanuka zaidi
 
udini, ukabila, ukanda, urangi, uzuri, jinsia......................... Inatosha jamani, chanzo ni nini??? Kwa nini hii????????? Kweli mwenye nacho anaongezewa...
 
Jamani msije mkazani ni utani vitu vinavyoandikwa hapa kwenye jamvi la wana JF.....Mimi mwenyewe binafsi nilipigwa na butwaa wiki moja iliyopita kuna jamaa yangu tulikuwa tunachapa nae mzigo akanipigia simu kuwa mkewe amepata NIDA kwenda kufanya registration za vitambulisho! nikamuuliza walitangaza lini hizo nafasi? akanijibu hazijatangazwa bali ni kimyakimya kama unamjua mtu NIDA muone...duh nilishiwa nguvu mana nikajiuliza Taasisi kama hiyo ya Serikali inafanya mambo kienyeji namna hii kweli tutafika????? sikuridhika ikabidi nimcall tena nikaongea na mkewe live akanijibu amepata kweli na wataanza training hivi karibuni. Nilijaribu kumuomba aniunganishe kwa huyo mhusika aliyempa mchogo aliniahidi lakini mpaka sasa giza tu. Kwa hiyo sisi wavimba macho tutaendelea kuapply mpaka mikono itaota sugu mana siku hizi wanapokea applications na kuchambua watu wao. TUOMBE MUNGU SANA SISI VIJANA WA KIMASIKINI AMBAO WAZEE WETU HAWAKUPATA BAHATI YA KUWEPO KWENYE ANY SYSTEM...
 
tutatoka tu hata wakiitana wenyewe kwa wenyewe. unajua wakati mwengine hata kama wanazo nafasi na ndugu zao hawapo, basi hawatangazi izo nafasi pia. karibu kwenye ujasiriamali ndugu yangu achana nao
 
Back
Top Bottom