Nidhamu katika Matumizi ya Kodi za Wananchi kwa Serikali na Viongozi wa Umma

Nidhamu katika Matumizi ya Kodi za Wananchi kwa Serikali na Viongozi wa Umma

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Amani iwe nanyi wanabodi!

Hata tuwe na makusanyo kikodi ya trilioni 100 kwa mwezi kama hatutakuwa na nidhamu katika matumizi ya fedha za wananchi nchi yetu itaendelea kuwa maskini milele!

Ukweli ni kwamba, hata haya makusanyo madogo tunayokusanya kupitia TRA, endapo Viongozi wetu wangeheshimu kuwa hizi ni kodi za wananchi na kuzitumia kwa nidhamu Nchi yetu ingepiga hatua kubwa sana za kimaendeleo kwa haraka sana!

Leo hii tunaona wasanii wakisafirishwa kwa makundi kwenda nchi za Nje kwa kodi za wananchi.

Leo hii tunaona Serikali ikinunua magari ya kifahari kwa viongozi wake na wakati mwingine magari hayo yanatumika katika shughuli za Chama cha Mapinduzi. Haya yote ni kodi za wananchi

Leo hii tunaona kiongozi anaamua tu kugawa pesa anavyojisikia. Kwa kuwa haulizwi kazitoa wapi na ni za kwake au za Serikali basi anagawa tu atakavyo. Hizi nazo ni kodi za Wananchi

Leo hii tunaona mabango na picha za Viongozi kila mahala hadi kwenye mechi za mpira watu wanaingia na picha na tshirt zilizokuwa printed za Viongozi. Ukiangalia haya yote ni matumizi mabaya ya kodi za Wananchi.

Tuliona awamu ya Tano, Rais Magufuli alikuwa anatembea na mabulungutu ya hela huku akigawa kwa mtu yeyote anayejiskia mtaani. Zote zile ni kodi za wananchi.


Leo tunaona shughuli sizizo na msingi, mara kupokea Mwenge, mara kupokea ndege, mara uzinduzi wa hiki na kile. Yote haya ni matumizi yasiyo sahihi ya kodi za wananchi.


Nipende kuwaasa Viongozi. Ingawa Watanzania wanaweza kuwa wajinga kwa wakati huu ila nina uhakika hawatakuwa wajinga milele. Kuna siku watapata akili na kuhoji namna mnavyotumia vibaya kodi zao.

Ipo siku wanaweza kugoma hata kulipa kodi maana wanaona kodi wanayolipa inamsafirisha na kumpa hela Irene Uwoya aende Korea kusini kupiga picha na kuuza sura.

Kwa Wananchi.
Pambaneni sana kupata Katiba Mpya. Katiba inayoweka misingi ya uwajibikaji na kuwawajibisha Viongozi wanaotenda kinyume chake au kinyume na Sheria za Nchi.

Msingi wa Uwajibikaji ni Katiba. Msingi wa kuheshimu Sheria za Nchi na Katiba ni Katiba yenyewe.

Machawa tunaowalalamikia wanatunzwa na fedha zetu / kodi zetu ambazo zinatumiwa hovyo kwa sababu Katiba haijaweka misingi mizuri ya kuheshimu kodi za wananchi.
 
Tunayo mengi ya kujifunza kwa wakenya.
Kenya Viongozi wanaiba kupitia madili. Huwezi ona matumizi mabaya ya pesa za walipakodi alafu wakaa kimya! Lazima wataongea tu
 
RAC.jpeg
 
Sio kuwa Tu na katiba ndugu ila usimamiaji WA utekelezaji WA Sheria kupitia hiyo katiba! Enforcement! Anglia South Africa have one of the most progressive constitutions in Africa na pia at the same time Wana rushwa na crimes za kutisha! Tupate kiongpzi jasiri Tz kama kiongozi Yew wa Sngapore alete nidhamu miaka kumi kwanza hata bila ya uchaguzi kuweka nidhamu kwanza
 
Sio kuwa Tu na katiba ndugu ila usimamiji WA utekelezaji WA katiba! Enforcement! Anglia South Africa have one of the most progressive constitutions in Africa na rushwa na crimes za kutisha! Tipate kiongpzi jasiri Tz kama kiongozi Yew waSingapore alete nidhamu miaka kumi kwanza hata bila ya uchaguzi kuweka nidhamu ndo haul unayoomgelea yatekelezwe
Katiba yetu haijaweka mipaka na misingi katika kuhakikisha kodi za wananchi zinatumika kwa shughuli za maendeleo ya wananchi tu na sio vinginevyo.

Katiba yetu haiwaweka kosa endapo kiongozi akifanya kinyume chake anawajibishwaje?

Katiba yetu imetengeneza miungu watu ambao wanaweza fanya lolote na wasihojiwe popote pale.

Hili ni ombwe kubwa sana!
 
Hii ndo hoja yangu sasa. Kuna haja gani ya Mkurugenzi wa shirika kutembelea gari kama hili?

Akitembelea Toyota Hilux atakufa?
Akitembelea Harrier atakufa?

Ulaji tu wa mafuta kwa gari hili ni mzigo tosha kwa Serikali. Hapo hujaweza service yake!

Viongozi wa nchi hii wajifunze kwa kweli. Wasipojifunza tuendako ni kubaya sana
 
Hii ndo hoja yangu sasa. Kuna haja gani ya Mkurugenzi wa shirika kutembelea gari kama hili?

Akitembelea Toyota Hilux atakufa?
Akitembelea Harrier atakufa?

Ulaji tu wa mafuta kwa gari hili ni mzigo tosha kwa Serikali. Hapo hujaweza service yake!

Viongozi wa nchi hii wajifunze kwa kweli. Wasipojifunza tuendako ni kubaya sana

Kama mwalimu anayelipwa mshahara wa laki 5 anamiliki gari lake ,why DED,RAC,DAS,RAS,RC,DC,NW,W,KM na watu wanaofanana na hao wapewe LC300 series za bure? Ni matumizi mabovu ya pesa.

Naungana na wewe watumie magari ya kawaida tu ,ya nini umnunulie gari la 600m?
 
Kama mwalimu anayelipwa mshahara wa laki 5 anamiliki gari lake ,why DED,RAC,DAS,RAS,RC,DC,NW,W,KM na watu wanaofanana na hao wapewe LC300 series za bure? Ni matumizi mabovu ya pesa.

Naungana na wewe watumie magari ya kawaida tu ,ya nini umnunulie gari la 600m?
Hakujawahi kuwepo kwa any logic kwa Viongozi wa Serikali kutumia gari zenye thamani ya zaidi ya Mil 100.
 
Kiukweli viongozi wetu hawafanani kabisa na wapigakura wao..wanakula hadi wanavimbirwa ndio maana wakitenguliwa kwenye hizo nafasi WANAPAGAWA

Magari ya kifahari ilihali hali ya barabara kwa sasa ni nzuri,lami sehemu kubwa ya nchi
Kutwa wapo barabarani Dar - Dom - Dar

Nyumba mbili mbili ,Dar na Dodoma na zote zinahudumiwa

Misafara ya kutisha wawapo kwenye shughuli za kiserikali mikoani

TUANZE KWA KUDAI KWA NGUVU ,KATIBA MPYA ILIYO BORA KAMA MSINGI NA DIRA YA UWAJIBIKAJI
 
Katiba yetu haijaweka mipaka na misingi katika kuhakikisha kodi za wananchi zinatumika kwa shughuli za maendeleo ya wananchi tu na sio vinginevyo.

Katiba yetu haiwaweka kosa endapo kiongozi akifanya kinyume chake anawajibishwaje?

Katiba yetu imetengeneza miungu watu ambao wanaweza fanya lolote na wasihojiwe popote pale.

Hili ni ombwe kubwa sana!
Nasema hivi katiba haiwezi saidia chochote kama wananchi wenyewe wasipobadilika. Taifa lenye raia wasiojiamini ni rahisi wanasiasa kujiona na miungu watu. Taifa ambalo kila msomi na asiye msomi anaamini ili awe tajiri ni lazima aingie kwenye siasa ili apate teuzi, cheo au madaraka ni ngumu kuendelea.
 
Nasema hivi katiba haiwezi saidia chochote kama wananchi wenyewe wasipobadilika Taifa lenye raia wasiojiamini ni rahisi wanasiasa kujiona na miungu watu. Taifa ambalo kila msomi na auseye msomi anaamini ili awe tajiri ni lazima aingie kwenye siasa ili apate teuzi, check au madaraka ni ngumu kuendelea.
Tukifanikiwa kuweka nidhamu na kuisimamia kwenye Katiba mengi sana yatabadilika hadi mtaani huku.

Wasomi wa nchi hii ni laana. Unamsikia mtu anasema kabisa Kiongozi ndo ameamua tena kwenye jambo ambalo kisheria sio sawa kabisa alafu anajiita msomi.

Nakubaliana na wewe tuna safari ndefu ila ipo sehemu ya kuanzia ambayo ni lazima tufanye kwa sehemu yetu!
 
Ipo siku wanaweza kugoma hata kulipa kodi maana wanaona kodi wanayolipa inamsafirisha na kumpa hela Irene Uwoya aende Korea kusini kupiga picha na kuuza sura.
Aaah mkuu acha hizi bhana ......usitaje majina ya watu kwa kuwatweza hivyo bhana.
 
Kenya Viongozi wanaiba kupitia madili. Huwezi ona matumizi mabaya ya pesa za walipakodi alafu wakaa kimya! Lazima wataongea tu
Kumbe madili na matumuzi mabaya ni vitu tofauti! Sikulijua hilo.
 
Back
Top Bottom