Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Duh sasa itakuwa vipi na mimi niko Single.Hapana
Happy New Year DarlingDah, sijui kwanini nimeumia kuachana kwenu,
Natamani mngeelewana na kuendeleza safari, i hate breakup kwani lazima kuna upande tu umeumia,
Nahisi bado mnanafasi yakuyaweka sawa na safari kuendelea
Love is beautiful thing
Happy new year Nifah
Mfyuuuuh [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Yeye ana waza ki Nietzsche, wee una waza ki lokole[emoji3][emoji23]
Oh, thank you.Nifah your brain work is next level. Salute!
Ninayo Imani ya kutosha kuamini kuwa msingi wa mgogoro ama tofauti za penzi lenu ni penzi lenu wenyewe. Kimombo niseme: methodological implementation and presentation of your love life. Hili ni hitimisho nimeikia baada ya kusoma maandiko yako kwenye sakata hili.
Imani yangu kwenu ni kuwa ikitokea mkaketi chini na kuamua kutanzua tofauti hizo, ikiwapendeza msione shida kupandisha daraja mahusiano yenu. Maana mnachopitia wakati huu ni misukosuko wa kawaida kabisa kwenye maisha ya mapenzi na mahusiano.
Hivyo wala usiwaze sana, wala usiumie moyo sana. Maana that's how the love pendulum swing on its axis
Best wishes
We maji matupu kweli😀😀, sema uta change tu 😂😂Mfyuuuuh [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Amen, nashukuru sana.@Nifah Swaiba, Rafiki. Kuna watu kwetu ni ngumu kukubaliana na hili mliloliamua. Twatamani tuwaitishe pamoja ili tu solve hili jambo. Kwakuwa mmeamua kwa kuridhia wenyewe pasi sisi kuwashauri basi ikawe Njema kwenu.
Ila Isigeuke vita baina yenu.
All right 🤒🤒Na sasa hivi mwalimu wako kichwa kimetulia, nitakuwa nakufundisha vyema.
U too 🤒Ndicho ninachokifanya my student
Happy New Year
Mtoto je?View attachment 2858656
Mapenzi kama yalivyo mambo mengine yana mwanzo na mwisho pia. Ni wachache waliobarikiwa na wenye bahati katika mapenzi huishia pamoja kwa kudumu milele hadi kifo kuwatenganisha, Huku wengi wakiishia njiani na hakuna ubaya katika hilo. Ndio maisha na mapenzi…. Ni safari isiyotabirika.
Miaka kadhaa iliyopita nilipata kuingia katika mapenzi yaliyofahamika na wengi hapa jamvini.
Hivyo basi, kwa kuwa mapenzi yale hayapo tena, imeniwia vyema kurudi tena hapa kuweka hilo wazi.
Tulikuwa na malengo ya kufika mbali, lakini kutokana na kutofautiana katika mambo mengi tulishindwa hata kufikia hatua za kuyarasimisha mahusiano yetu kuwa halali.
Tulitengana rasmi mwezi August mwaka huu 2023, na kutokana na hilo pengine huenda yakawa ndio mahusiano yangu ya mwisho kuyaweka wazi.
Mapenzi ya wazi hapa yamenipa wakati mgumu kujibu mamia ya wanachama waliokuwa wakihoji endapo bado tupo pamoja, na ndio sababu kuu naweka uzi huu kuwafahamisha wote kwa pamoja, hatupo tena katika mahusiano.
Tumeachana kwa amani, na kwa dhati kabisa namtakia kheri katika maisha mapya bila ya uwepo wangu kwa aliyekuwa mwenzangu.
Nifah