Nifanye kazi gani nipate laki tano kwa siku 30?

Nielekeze zaidi nakuja pm
 
Hii unafanyaje nipe mwanga kidogo
 
Hapo Dodoma ulipo nunua nguo za kike uza, utawapata masista duu wa Udom muda sio mrefu chuo kitafunguliwa. Utapata hata zaidi ya hizo laki 5
 

Ndugu tupe ufafanuzi kidogo kuhusu suala hili, kana ni kuandika unakua unawaandikia kitugani na kama ni ku uppload picha na video ni za aina gani
 
Ushauri Wangu Huu
Hongera Sana Kwa Hatua Kubwa Sana Kwenye Maisha Ambayo Ni Ngumu
Nia Yako Ni Nzuri Sana Umalize Nyumba Uwe Unatoka Kwako
Hapa Utapewa Ushauri Mwingi Lakini Lazima Uuchuje Sana Kufikia Malengo





Itapendeza Ukiwa Mvumilivu Na Subira Kuliko Kufanya Haraka Na Kujutia
Unaweza Kuweka Mlango Wa Chumba Kimoja Na Dirisha Tu Ukahamia
Kuliko Yote Wakati Uwezo Hauruhusu
 
Hii unafanyaje nipe mwanga kidogo
Kuna nyuzi zinatrend jukwaa la Jamii Intelligence mfano utakuta uzi unasema 'Wadudu kumi hatari duniani' au 'Magonjwa kumi hatari duniani' au 'Watu 10 warefu duniani'

Zile nyuzi wanazitoa online kutoka kwenye website ya Listverse. Now Listverse hawawezi kuandika kila kitu wao hivyo wanaajiri freelancers wa kuandika maudhui yao.

Wanalipa Dola 100 wakikubali utakachowaandikia. Isipokua wanalipa kwa kutumia Paypal ambayo kwa Tz ukiwa na akaunti ya Paypal hautaweza kupokea pesa hivyo hakuna mtu aliye Tz ataweza kulipwa.

Websites ambazo hazitumii Paypal hulipa pesa kidogo. Mfano Mysterious world wanalipa dola 25 hivyo tafuta website itakayokuridhisha, fanya nao kazi. Fuatisha masharti yao ya uandishi ukikubaliwa article yako wanakulipa.

Picha ulipwaji wake utategemea na unapoupload na camera yako pia. Mfano picha za smartphone huwezi kuziweka Getty image au Stock photo ukatarajia pesa ndefu.

Pia malipo ni tofauti na website. Mfano sehemu nyingine watakulipa kadri watu wanavyodownload picha yako na sehemu nyingine watakulipa hapo hapo ila watu wakidownload picha ulizoweka haupati tena kitu.
 
Ndugu tupe ufafanuzi kidogo kuhusu suala hili, kana ni kuandika unakua unawaandikia kitugani na kama ni ku uppload picha na video ni za aina gani

 
Shukrani. Hii nzuri aisee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…