Magical power
JF-Expert Member
- Sep 27, 2022
- 2,158
- 5,626
Nifanye Nini, Niliacha Kazi Nikijua Napendwa Kumbe Mimi Ni Mume Wa Mchongo Tu!
Baada ya kumuoa mke wangu, alinishawishi niachane na kazi ili nisaidie kusimamia biashara zake. Nilikuwa nimeajiriwa kwenye kampuni moja ya simu na kipato changu kwa mwezi, mshahara na marupurupu, kilikuwa kama milioni moja na nusu.
Ukiangalia, mke wangu alikuwa na biashara na maduka mawili ya vipodozi Kariakoo, kwa mwezi mauzo si chini ya milioni 50, yaani kila kitu kilikuwa vizuri. Kila kitu alinishirikisha na kweli niliona kama ni ujinga kuendelea na kazi wakati naweza kusimamia biashara zetu.
Mwaka wa kwanza katika biashara ulikuwa mzuri, alinishirikisha kwa kila kitu, na wakati mwingine tulikuwa tunasafiri pamoja. Ukiingia Instagram na kuniona na mke wangu, ungedhani kweli hii ndoa ni nzuri. Kizuri zaidi, alikuwa anafanya kama mimi ndiye nina pesa, hakutaka kunidhalilisha, hivyo ilinifanya niamini vizuri. Mambo yalibadilika baada ya kubeba ujauzito. Ujauzito ukawa unamsumbua sana, akalazwa hospitalini, hivyo mimi ndiye niakawa nasimamia biashara zetu kwa asilimia mia moja.
Kuna mtu aliniunganisha naye kwa ajili ya kuchukua mizigo yake, mara nyingi aliniambia nimnunulie vitu na kuna mambo mengine ambayo hayakuwa ya kueleweka. Ni mwanaume na alinionyesha kama dharau fulani. Nilimwambia mke wangu, “Mbona unaweza kufanya kila kitu mwenyewe, simhitaji huyu mtu.” Akanijibu, “Hapana, ukitaka tugombane, gombana na huyo mtu.”
Kweli nilishtuka na kujiuliza huyu ni nani, lakini niliamua kukaa kimya. Baadaye yule mwanaume alianza kuja dukani, kuuliza kuhusu mapato na kuongea na wafanyakazi kwa kujiamini kana kwamba mimi sipo. Nilimuuliza mke wangu, na akaniambia, “Msikilize tu, ananipa madili.” Nikasema, “Hapana, hata kama anakupa madili, hawezi kunidhalilisha, mimi ni mume wako.” Siku moja, wakati mke wangu alikuwa anakwenda kujifungua, nilimwambia jamaa kuwa sitaki uje dukani kwangu kusimamia kaa huko kama mlifanya biashara na mke wangu sitaki tena.”
Alicheka na kuniambia, “Yaani unajiona wewe una kauli? Subiri nitakuonyesha.” Sikukaa sawa, mke alipotoka tu kujifungua, nilikwenda kumuona mtoto, akanambia, “Usiende tena dukani, naona unataka kuniharibia na watu wangu.” Sijakaa sawa, na yule mwanaume akaanza kupiga simu kuuliza kuhusu mtoto. Nilimuuliza mke wangu inakuwaje, akanijibu, “Wewe rudi nyumbani.”
Kweli nilichanganyikiwa ila sikuenda dukani kwa mwezi mzima, mwanamke alinikatalia katakata. Kadri siku zilivyoendelea, nilimuangalia mtoto na kuona jinsi alivyofanana na yule mwanaume kabisa. Nilipomuuliza mke wangu, akaniambia, “Ni akili zako tu.” Ndipo nilipoanza kufuatilia na nikaambiwa kwamba huyo ni mtu wake wa muda mrefu na ndiye aliyemfungulia yale maduka.
Kila mtu anajua mke wangu anatembea na huyo mwanaume na ndiyo kampa mtaji wa kila kitu, hata zile fremu ni za jamaa mke wangu ana mali tu siku wakigombana anamfukuza! Nilichunguza zaidi na kugundua kuwa hata mimi kumuoa ilikuwa ni mipango yao, kwani mke wa jamaa alishaanza kushuku na kuleta shida, hivyo akaamua mke wangu aolewe na mimi ili ionekane ana ndoa.
Niligundua kuwa hata kule kupostiwa kila siku si kwa sababu alikuwa ananipenda, bali mke wa yule jamaa ajue kuwa ana mume wake. Nilipomuuliza mke wangu, akaniambia, “Fanya unavyotaka!” Sasa niko hapa nimechanganyikiwa, hata sijui nifanye nini. Ndoa yenyewe haina amani, sina hata kazi nilishaacha. Narudije kuanza sifuri
MWISHO
Baada ya kumuoa mke wangu, alinishawishi niachane na kazi ili nisaidie kusimamia biashara zake. Nilikuwa nimeajiriwa kwenye kampuni moja ya simu na kipato changu kwa mwezi, mshahara na marupurupu, kilikuwa kama milioni moja na nusu.
Ukiangalia, mke wangu alikuwa na biashara na maduka mawili ya vipodozi Kariakoo, kwa mwezi mauzo si chini ya milioni 50, yaani kila kitu kilikuwa vizuri. Kila kitu alinishirikisha na kweli niliona kama ni ujinga kuendelea na kazi wakati naweza kusimamia biashara zetu.
Mwaka wa kwanza katika biashara ulikuwa mzuri, alinishirikisha kwa kila kitu, na wakati mwingine tulikuwa tunasafiri pamoja. Ukiingia Instagram na kuniona na mke wangu, ungedhani kweli hii ndoa ni nzuri. Kizuri zaidi, alikuwa anafanya kama mimi ndiye nina pesa, hakutaka kunidhalilisha, hivyo ilinifanya niamini vizuri. Mambo yalibadilika baada ya kubeba ujauzito. Ujauzito ukawa unamsumbua sana, akalazwa hospitalini, hivyo mimi ndiye niakawa nasimamia biashara zetu kwa asilimia mia moja.
Kuna mtu aliniunganisha naye kwa ajili ya kuchukua mizigo yake, mara nyingi aliniambia nimnunulie vitu na kuna mambo mengine ambayo hayakuwa ya kueleweka. Ni mwanaume na alinionyesha kama dharau fulani. Nilimwambia mke wangu, “Mbona unaweza kufanya kila kitu mwenyewe, simhitaji huyu mtu.” Akanijibu, “Hapana, ukitaka tugombane, gombana na huyo mtu.”
Kweli nilishtuka na kujiuliza huyu ni nani, lakini niliamua kukaa kimya. Baadaye yule mwanaume alianza kuja dukani, kuuliza kuhusu mapato na kuongea na wafanyakazi kwa kujiamini kana kwamba mimi sipo. Nilimuuliza mke wangu, na akaniambia, “Msikilize tu, ananipa madili.” Nikasema, “Hapana, hata kama anakupa madili, hawezi kunidhalilisha, mimi ni mume wako.” Siku moja, wakati mke wangu alikuwa anakwenda kujifungua, nilimwambia jamaa kuwa sitaki uje dukani kwangu kusimamia kaa huko kama mlifanya biashara na mke wangu sitaki tena.”
Alicheka na kuniambia, “Yaani unajiona wewe una kauli? Subiri nitakuonyesha.” Sikukaa sawa, mke alipotoka tu kujifungua, nilikwenda kumuona mtoto, akanambia, “Usiende tena dukani, naona unataka kuniharibia na watu wangu.” Sijakaa sawa, na yule mwanaume akaanza kupiga simu kuuliza kuhusu mtoto. Nilimuuliza mke wangu inakuwaje, akanijibu, “Wewe rudi nyumbani.”
Kweli nilichanganyikiwa ila sikuenda dukani kwa mwezi mzima, mwanamke alinikatalia katakata. Kadri siku zilivyoendelea, nilimuangalia mtoto na kuona jinsi alivyofanana na yule mwanaume kabisa. Nilipomuuliza mke wangu, akaniambia, “Ni akili zako tu.” Ndipo nilipoanza kufuatilia na nikaambiwa kwamba huyo ni mtu wake wa muda mrefu na ndiye aliyemfungulia yale maduka.
Kila mtu anajua mke wangu anatembea na huyo mwanaume na ndiyo kampa mtaji wa kila kitu, hata zile fremu ni za jamaa mke wangu ana mali tu siku wakigombana anamfukuza! Nilichunguza zaidi na kugundua kuwa hata mimi kumuoa ilikuwa ni mipango yao, kwani mke wa jamaa alishaanza kushuku na kuleta shida, hivyo akaamua mke wangu aolewe na mimi ili ionekane ana ndoa.
Niligundua kuwa hata kule kupostiwa kila siku si kwa sababu alikuwa ananipenda, bali mke wa yule jamaa ajue kuwa ana mume wake. Nilipomuuliza mke wangu, akaniambia, “Fanya unavyotaka!” Sasa niko hapa nimechanganyikiwa, hata sijui nifanye nini. Ndoa yenyewe haina amani, sina hata kazi nilishaacha. Narudije kuanza sifuri
MWISHO