Nifanyeje kuwa Mchambuzi mzuri wa Siasa?


Uomeona eh? AshaDii anasukumia wengine wakati yeye ni moja wa hao hao vinara.

Mie nishambook kwa ajili ya semina endelevu ya jinsi ya kuchambua nyuzi za MMU.
 

looks fine, japo bado nimebaki na maswali ngoja nijichunguze kidogo, nadhani nachanganya mambo mawili kwa wakati mmoja juu ya hitaji la huyu bwana kati ya kuwa "fair minded mchambuzi wa mambo ya kisiasa" au "fair minded mwanasiasa"

My thinking is, kama anataka kuwa mchambuzi maana yake amekwishaamua kutoside na upande wowote ule zaidi ya kutoa opinions kitu kinachonifanya nione haitaji kuwa na msimamo what so ever.
 

lol, Mtu mzima kumbe na wewe hiyo hali huwa inakukuta pia?

Dah nina mda mrefu sana sijaanzisha sred hapa jamvini sababu ya hicho kitu..... :smiling: nimecheka sana kujua tupo wote!

Pamoja na yote Bro, una kitu maalum sana ndani yako..... mara zote unafunguka kuhusu kitu chochote unachokiamini basi huwa unatoa chote bila uchoyo na binafsi huwa naona raha kukufuatilia tu... japo mida michache tunapishana lol...

Hakika u-mchambuzi mzuri n' a true Great Thinker!

Miongoni mwa mijadala naukumbuka uliuleta kwa stail yako ya taarifa ni ule ulisimulia historia ya Mtwara, na tukawa na wapendwa wetu wengine hapa tukasema mengi mazuri juu ya Mtwara......

Nikionaga watu kama nyie huwa najiachia sana na kukubali kuwa kweli JF ni nyumbani kwangu.
 
Reactions: EMT

Tuwe wakweli, wapiga kura wa tanzania wanauwezo wa kuchanganua mambo ya kisiasa? hata wanasiasa wenyewe (majority) wanaelewa makujumu ya kisiasa? wanaweza kuchanganua maamuzi ya kisiasa? wamepata op opportunity ya kulitumikia taifa katika mchakato wa katiba, unawaona wanachokifanya? wanashiriki?
 
Mzima wa afya Olesaidimu, namshukuru Mungu kwa hilo. I am humbled to have missed me. Habari ya siku lakini?[/QUOTE]

Bukheir dada tuendelee kuombeana yenye kheri
 
Uomeona eh? AshaDii anasukumia wengine wakati yeye ni moja wa hao hao vinara.

Mie nishambook kwa ajili ya semina endelevu ya jinsi ya kuchambua nyuzi za MMU.

Huyu dada ni mzuri sana wala hawezi kukwepa hilo. Kuna hawa watu sikuhizi siwaoni humu ndani sijui wako wapi? Dua, kiruma, Mgumu, Mwanagenzi, Field Marshall ES, Augustine Moshi, Tatu, Eric ongora, Phillemon Mikael, Jasusi, Washawasha, Ogah, Tabasamu, Manji makuti, Mkira, Sam, Jizaledo, Kulikoni, Mkuyuga, mTz, alles, Mkandara, quarz, @kichunguu, timbwilitimbwili. Hawa jamaa kila nikisoma maandishi yao natamani niwaone wakiendelea kutoa darasa za mambo ya siasa humu ndani. Popote walipo Mungu awe nao manake wametuachie elimu kubwa humu.
 
Last edited by a moderator:

Nafikiri hapa ndipo ilipo demarcation kati ya politician na political analyst..sidhani pia kama ni dhambi kwa political analyst kuwa na anachokiamini (side) kwasababu as human being ni ngumu kuzuia...ni sawa na refa mtanzania ambaye sio mpenzi wa ama Yanga au Simba....ni ngumu kutokea. La Msingi anakuwa fair hata kukosoa kile anachoamini. Hili ndilo linalokosekana hapa JF miaka ya karibuni....
 

Katika siasa zetu ambazo tunaambiwa madhumuni ya chama cha siasa ni kushika dora, inakuwa ngumu sana kuwa na fair minded politicians, ambao wanashika dora watahakikisha wanawapinga wanaotaka kushika dora na wale wanaotaka kushika dora watawapinga wale wanaoshika dora hata katika mambo ya msingi kabisa ili mradi tu ama waendelee kushika dora ama wawaangushe wenzao.

Namna moja ya kuhakikisha tunakuwa na wanasiasa wanaosimamia majukumu ya kisiasa ya Taifa hili kwa manufaa ya Taifa, na sio wao au vyama vyao ni kuwa na bunge huru, namna ingine ni kuelimisha wananchi ili waelewe makujukumu ya kisiasa ni yepi ili, japo wakati wa uchaguzi waweze kupambanua na kuchagua wale wanaoweza kuyatimiza.

Lakini hata mazingira ya kisiasa yakiwa mazuri namna gani, sidhani kama ni sawa kutegemea kuwa na mwanasiasa fair, hasa hapa kwetu.
 

Kwa hapa kwetu ni vigumu kupata mwanasiasa anayepractice siasa then ukamtegemea awe pia political analyst na akawa fair... wengine si walipojaribu wamekolimbwa na tunakumbuka? Hata nyerere kuna wakati walitishia kumpoka kadi baada ya kuwasema, Sitta naye amekuwa akijaribu (though kwa motives zake) na cha moto ameshakiona kwani ilibidi tupate hata spika mwanamke bila kupenda wala kujiandaa...pengine tuangalie waliopo nje unaweza kukuta wachache....very few of them.....wapo watu kama kina Jenerali Ulimwengu pengine nikikumbuka mwingine nitarejea....Bongo kila kitu ni kipya na ni vigumu kukiandikia maana tupo unique kwenye mambo mengi.
 
Habari Wakuu,

Kwa watu wanaopenda kutoa maarifa kwa manufaa ya wengine ningependa wanisaidie kwa hili; nahitaji kuwa mchambuzi wa masuala ya Siasa ila sijui njia itakayo niwezesha kuwa mchambuzi.

Msaada wenu tafadhali.

Anza kufanya mazoezi ya kuvumilia kung'olewa kucha bila ganzi.
 

KIONGOZI
Chanzo cha Tatizo ni vyuo vyetu, na sasa hali ndio mbaya sababu wakufunzi wetu wameamua kushiriki siasa actively, hapo usitegemee vyuo (ambavyo ndio chungu cha kupika watu wenye uwezo wa kuhoji na kujadiri bila uoga mambo ya msingi katika jamii yoyote ile) kutoa maintellectual (nakumbuka tulikuwa tunajiita hivyo chuoni)

Ushahidi ni namna wanavyuo wetu wanavyoshiriki katika siasa, wale walio vyuoni na wale fresh from college, mategemeo ni kwamba hawa bado yale mambo mazito yanayofundishwa huko yako kwenye finger tips hivyo watuletee sisi tuliokitaa kwa muda mrefu hoja nzito ambazo kimsingi tutakubaliana nazo tu, sababu nyingi zina mantiki kubwa sana, lakini wapi? na wao wamekuwa watu wahovyo zaidi.

Muangalie mtu kama DR Kitilya Mkumbo, mkufunzi pale UDSM na ni kada kindakindaki wa CHADEMA, unategemea anaweza kuwapitisha wanafunzi wake kwenye tanuru la hoja zinazohoji msimamo na muelekeo wa kisiasa wa chama chake? au BAREGU? na hawa afadhali hawajaharibika, Muangalie Benson Bana, Profesa na Mkuu wa kitengo kikubwa tu, mtazame jinsi alivyokuwa biased kiasi kwamba anaonekana kama kichekesho anapoongea, wote hawa wamejishusha na kufikia viwango vya siasa za Lowasa, Cheap,unethical,self centered, currupted politics.

Na bado, hata bila kuangalia siasa uchwara zilivyoingia vyuoni na kuharibu mahala pale, hata kabla, mambo yaliyokuwa yakifundishwa huko siyo mambo yanayoweza kuzaa watu wenye uwezo wa kudadavua maswala haya kwa undani wake.
Na sikumbuki kuona mjadala matata japo juu ya sera za ujamaa,ubepali,democracy, n,k na hata wakufunzi waliokuwa wajijaribu kuteka wanafunzi kwa hoja zao walikuwa one sided.

Kwa mfano ufundishwe na Profesa Baregu alafu utegemee kutoka apo na mtazamo chanya wa aina yoyote ile kwa marekani, thubutu.

Ndio maana tuko hivi.
 
Tuwe wakweli, wapiga kura wa tanzania wanauwezo wa kuchanganua mambo ya kisiasa?

Wakitaka wanaweza tena sana tuu. Ni kutokana na wao kutofanya hivyo kumesabanisha kuwe na wanasiasa wasioweza kuchanganua mambo ya siasa.

hata wanasiasa wenyewe (majority) wanaelewa makujumu ya kisiasa? wanaweza kuchanganua maamuzi ya kisiasa?

Wapo wengi wengi tuu wakitaka wanaweza tena sana. Wengine mpaka maprofesa wa chuo lakini lakini wanashindwa kuchanganua au hata kupima madhara ya kauli zao.

wamepata op opportunity ya kulitumikia taifa katika mchakato wa katiba, unawaona wanachokifanya? wanashiriki?

Kwa nini hawashiriki?
 

Mkuu EMT, haya mambo ni kama hobby, ni kama Imani fulani hivi, haya mambo ni burudani kuyashiriki, ukimuona mtu hayashiriki ujue hajui.

Unaniuliza kwa nini hawashiriki?
 
Mkuu, kwanza kabisa asubuhi amka fanya jogging,
Ukishamaliza kula supu na chapati,
Baada ya hapo mchana kula ugali mkubwa na samaki, halafu baadae jioni nenda katafute mademu, amini usiamini utatisha mkuu.
 
kitu kibaya ni kwamba watanzania wengi hufikiri kujua siasa ni kujua majina ya wabunge, mawaziri , viongozi wa chama na na ni yuko wapi na anaongoza nini. kumbe siasa ni kama mfumo wa maisha ambao watu wamejichagulia au wanaufuata wakiamini utawasaidia kuyafikia malengo yao. kwa hiyo mkuu ukitaka kujua siasa za nchi, watu au chama fulani angalia kwanza visions na missions za hao watu. usiingie katika mtego wa kujua majina. ukifanya hivyo utakuwa na uwezo wa kupredict next move ya mwanasiasa yeyote. lakini hili haliji kirahisi inabidi uwe na hobby ya kujisomea na kuelewa mambo.
 
Kuwa mchambuzi wa kitu ni zaidi ya kusoma. Jambo la msingi ni kuwa na kiu ya weledi na maarifa. Sikiliza wachambuzi mbalimbali, soma vitabu, majarida na magazeti. Sikiliza redio na tazama luninga. Jitahidi kuenda na wakati kwa kutafuta taarifa mpya na za zamani ambazo ni za kipekee. Ukiweza soma Falsafa kwa ajili ya kukusaidia kufikiri kwa mantiki, pia si vibaya ukijifunza lugha tofauti tofauti za kimataifa ili kujiweka katika fursa nzuri ya kupata maarifa na weledi bila kikwazo.
 

Sasa nimeelewa kuwa ni wapi tumepishana. Hiyo para yako ya mwisho ni haswa inavyotakiwa kuwa... Nadhani ni kheri tukaenda step by step tukajaribu kuwekana sawa. Unaweza kuta kuwa pengine mimi ndiyo nachanganya habari hapa na nakosea mtazamo.

Naamini kuwa hata ukiwa Mchambuzi ambaye huegemei upande wowote kuna principles ambazo one has to hold. Kusimamia unacho amini, si tu kwa misingi ya kipi unaamini kati ya makundi mawili - nadhani hata pia kile ambacho unaamini in relation ya makundi hayo mawili.
 

Mimi nidhani hapo nilipobold ndio anapaswa kusimamia badala ya kuwa na msimamo wake.
 
soma kijana
siasa safi,uchambuzi makini ni matokeo ya kukamata kitabu.Usichague cha kusoma.SIASA imebeba mambo mengi ya kiuchumi,kijamii na maisha ya kila siku.Kwa maana hiyo lazima uwe na uwanja mpana wa uwelewa ili ukichambua Professors,DK na watu wa kawaida ndani ya jamii wakuelewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…