Nifanyeje niache tabia ya kujitenga na watu?

Nifanyeje niache tabia ya kujitenga na watu?

kibla matata

JF-Expert Member
Joined
Mar 3, 2020
Posts
412
Reaction score
380
Habari za mida hii wapendwa

Mimi ni wa kwanza kuzaliwa katika familia ya watoto wawili. Katika makuzi yangu tokea Primary School nilikuwa naishi kwa style fulani ya kujitenga tenga na wenzangu. Ikafika kipindi wenzangu niliokuwa nikisoma nao shule wakawa wananiita mimi mchawi.

Kwa mfano labda kama kuna kitu shuleni ambacho kinahusisha wingi wa watu mimi lazima nitatoroka shuleni au kama zile group discussions basi mimi lazima nitajitenga. Nilikuwa sipendi kuwa na rafiki kuna jamaa yangu mmoja alikuwa anapenda kuwa karibu na mimi lakini ilifika mahali hata akija nyumbani kuniuliza nilikuwa namkwepa.

Sasa wadau tatizo limekuwa sugu hadi sasa hivi nimekuwa sina rafiki hata nikisema nijichanganye kwa watu nakuwa sijisikii kujiamini. Kuna muda nasema labda nianze kushabikia mpira lakini sina muda navyo hivyo vitu kwa kifupi hadi saivi sina rafiki hata mmoja.

Kuna wengine nawaona wanaoenda kuwa karibu na mimi lakini nimekuwa mtu wa kujitenga nao. Kwa kifupi nikienda kazini ya huko nayaacha huko huko nikirudi nyumbani napenda kujifungia ghetto kuangalia movies kuchati nikitoka mgahawani narudi tena mbio nyumbani. Bahati nzuri nyumba niliyopanga niko peke yangu yule mama kashanizoea naweza kukaa na watu nakuwa mpenzi msikilizaji tu siongei neno hata moja, wakinisemesha najibu short ama nakuwa mkali.

Naombeni ushauri jamani, kuna muda nawaza hadi nafika mbali. Kwanini nimekuwa mtu wa kujitenga?
 
Sio lazima uwe karibu na watu!

After all unataka kujifunza nini kwa watu ambao asilimia 90 ya mazungumzo yao ni ngono, udaku na porojo!

Lock yourself in a room and watch a good movie or read a book!

Mimi nadhani uko sawa tu na ndio tabia yako hiyo!

Ukikaa na hawa waswahili watakuambukiza uwezo duni wa kufikiri tu. Hakuna lolote utakalojifunza zaidi ya staili za ngono na kupiga domo forodhani.
 
Habari za mida hii wapendwa

Mimi ni wa kwanza kuzaliwa katika familia ya watoto wawili. Katika makuzi yangu tokea Primary School nilikuwa naishi kwa style fulani ya kujitenga tenga na wenzangu. Ikafika kipindi wenzangu niliokuwa nikisoma nao shule wakawa wananiita mimi mchawi.

Kwa mfano labda kama kuna kitu shuleni ambacho kinahusisha wingi wa watu mimi lazima nitatoroka shuleni au kama zile group discussions basi mimi lazima nitajitenga. Nilikuwa sipendi kuwa na rafiki kuna jamaa yangu mmoja alikuwa anapenda kuwa karibu na mimi lakini ilifika mahali hata akija nyumbani kuniuliza nilikuwa namkwepa.

Sasa wadau tatizo limekuwa sugu hadi sasa hivi nimekuwa sina rafiki hata nikisema nijichanganye kwa watu nakuwa sijisikii kujiamini. Kuna muda nasema labda nianze kushabikia mpira lakini sina muda navyo hivyo vitu kwa kifupi hadi saivi sina rafiki hata mmoja.

Kuna wengine nawaona wanaoenda kuwa karibu na mimi lakini nimekuwa mtu wa kujitenga nao. Kwa kifupi nikienda kazini ya huko nayaacha huko huko nikirudi nyumbani napenda kujifungia ghetto kuangalia movies kuchati nikitoka mgahawani narudi tena mbio nyumbani. Bahati nzuri nyumba niliyopanga niko peke yangu yule mama kashanizoea naweza kukaa na watu nakuwa mpenzi msikilizaji tu siongei neno hata moja, wakinisemesha najibu short ama nakuwa mkali.

Naombeni ushauri jamani, kuna muda nawaza hadi nafika mbali. Kwanini nimekuwa mtu wa kujitenga?
Utakuwa introvert mzeee. La msingi jaribu kutengeneza mzungumko mchache tu watosha.

Sio lazima huwe kama kila mtu alivyo, tafuta faida za wew kuwa hivo then zitumie effectively
 
Kusema ukweli hata huyo jamaa yangu nilikuwa hata nilikaa naye natamani aondoke au naweza nikaanzisha kasafari ili niweze kukaa naye mbali
 
Sio lazima uwe karibu na watu!

After all unataka kujifunza nini kwa watu ambao asilimia 90 ya mazungumzo yao ni ngono, udaku na porojo!

Lock yourself in a room and watch a good movie or read a book!

Mimi nadhani uko sawa tu na ndio tabia yako hiyo!

Ukikaa na hawa waswahili watakuambukiza uwezo duni wa kufikiri tu. Hakuna lolote utakalojifunza zaidi ya staili za ngono na kupiga domo forodhani.
Aisee ni kweli unayomuambia ila umekua too general kua kujichanganya na watu ni hasara. Kitu ambacho si kweli kutokana na maelezo ya jamaa ana tatizo na inapaswa alitatue haya maisha ya sasa huwezi ishi kama kisiwa interaction ni muhimu, hivyo kumuambia abaki hivyo hivyo ni kumpotosha. Ajitahidi kutafuta few positive friends na awe interactive.
 
Sio lazima uwe karibu na watu!

After all unataka kujifunza nini kwa watu ambao asilimia 90 ya mazungumzo yao ni ngono, udaku na porojo!

Lock yourself in a room and watch a good movie or read a book!

Mimi nadhani uko sawa tu na ndio tabia yako hiyo!

Ukikaa na hawa waswahili watakuambukiza uwezo duni wa kufikiri tu. Hakuna lolote utakalojifunza zaidi ya staili za ngono na kupiga domo forodhani.


Naunga mkono hoja..sasa hivi ukipata kijana anaongelea mafanikio na anajibidisha bora umgande kizazi cha ajabu sana hiki...bora kuwa alone!
 
Mimi Nipo kama wewe huwa sipendi sana kujichanganya ovyo na watu ambao najua hatuwezi kupiga nao stori hata dk3 tu

Ishi maisha yako tu mkuu Huwezi kumfurahisha kila mtu hapa Duniani!
kuna kipindi nipo school nilikuwa nafaulu masomo yotee A+.. Lakini kwenye report teacher wa darasa pale kwenye uhusiano na jamii alikikuwa ananipa ziro, sifuri!But nilikuwa the BEST.
 
Back
Top Bottom