Mkuu nitumie njia gani au we ulifanyaje angalau nipate kulifresh
Kwanza unajua football inavyochezwa?? Kama ndio safi, kama hapana tafuta mtu akuelezee.
Ukishaelewa au kama unaelewa, tafuta shabiki wa timu yeyote anae elewa hiyo timu na akusimulie mchezaji au wachezaji fulani wa hiyo timu uwezo wao pamoja labda na kocha.
Pia akuelezee na mifumo pamoja na timu hasimu za hiyo timu anayoipenda.
Hayo hapo juu yafanyike kabla ya kwenda kuangalia timu hiyo ikicheza.
Sasa kaangalie mechi moja ukiwa na huyo muelekezaji wako mkaangalie hiyo timu anayoipenda na awe anakupa dondoo ya kinachoendelea.
Pia akuelezee kuhusu ligi na umuhimu wake na mafanikio yanayopatikana timu ikishinda kombe la ligi fulani.
Kama atakua muelekezaji mzuri basi utaanza kuifuatilia hiyo timu kila ikicheza huku ukilinganisha na timu zingine na uwezo wa mchezaji mmoja mmoja na timu kwa ujumla huku ukifuatilia zile dondoo alizokupa.
Nakuhakikishia utapata timu ya kuishabikia na sumu itakuingia tu inapofungwa na utaanza kulia kabisa ila usijinyonge.
Mfano mie nilijikuta naishabikia Manchester United hapo zamani na kuna baadhi ya wachezaji walinivutia. Walipoondoka au kuondolewa nilikasirika sana. Nikasoma article moja ilimhuhusu mchezaji mmoja aliitwa Makelele akinyanyasika wakati yuko real madrid, akahamia Chelsea nikawa namfuatilia ili nione huo uwezo wake.
Nikawa kila mechi ya Chelsea lazima niangalie....hapo nikajikuta nimehamia kuishabikia Chelsea mwishowe nikavutiwa na Mourinho. Basi nikabaki huko hata Makelele alipoondoka.
Naamini mchango wangu utakusaidia walau kiduchu.