Niffer atoa majibu baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kutaka akamatwe kwa uchangishaji wa fedha kwa ajali ya maafa Kariakoo

Niffer atoa majibu baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kutaka akamatwe kwa uchangishaji wa fedha kwa ajali ya maafa Kariakoo

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mfanyabiashara maarufu Jennifer Jovin, anayefahamika kama Niffer, ametoa majibu yake baada ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, kumtaja katika hotuba yake ya hadhara akitaka afuatiliwe na kueleza nani aliyempa mamlaka ya kuchangisha fedha kufuatia ajali ya kuporomoka kwa gorofa la Kariakoo.

Soma: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Watu 7 wengine waokolewa

Kupitia majibu yake yaliyojaa shukrani na kueleza nia njema, Niffer amesema:

"Kwanza kabisa, Alhamdulillah, namshukuru sana Allah kwa kunipa nafasi ya kuiona siku ya leo. Kwa kweli, ni jambo kubwa sana kwangu kuona Waziri Mkuu wa nchi yangu ametaja jina langu mbele ya hadhara ya watu mashuhuri. Hii ni ndoto kubwa iliyotimia kwa ulimwengu wa roho."

Niffer ameeleza kuwa nia yake kuu ilikuwa kusaidia wahanga wa ajali hiyo, akisisitiza kuwa hakujua sheria zinazohusiana na uchangishaji wa fedha kwa ajili ya mafaa kama hayo. Ameeleza:

"Nilikuwa tayari tangu mwanzo kutoa ushirikiano kwa Serikali na jamii kwa ujumla. Niliomba muongozo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa kabla ya kuanza zoezi hili. Ninaamini nia yangu haikuwa mbaya, na kupitia changamoto hii, nimeona umuhimu wa kuwa na taasisi inayotambulika rasmi, Niffer Foundation."

Waziri Mkuu Majaliwa, wakati akizungumza eneo la Kariakoo, alisisitiza kuwa hakuna mtu anayepaswa kuchangisha fedha bila kibali maalum kutoka serikalini na akatoa agizo kwamba Niffer atafutwe ili aeleze ni nani aliyempa mamlaka hiyo.

Soma, Pia: Jeshi la polisi tayari limempata Niffer kwa kuchangisha michango ya wahanga wa Kariakoo

Baada ya agizo hilo, taarifa zilitolewa kuwa Niffer ameshapatikana na yuko tayari kushirikiana na mamlaka husika.
1731929432654.png


1731929682294.png
 
Mfanyabiashara maarufu Jennifer Jovin, anayefahamika kama Niffer, ametoa majibu yake baada ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, kumtaja katika hotuba yake ya hadhara akitaka afuatiliwe na kueleza nani aliyempa mamlaka ya kuchangisha fedha kufuatia ajali ya kuporomoka kwa gorofa la Kariakoo.

Kupitia majibu yake yaliyojaa shukrani na kueleza nia njema, Niffer amesema:

"Kwanza kabisa, Alhamdulillah, namshukuru sana Allah kwa kunipa nafasi ya kuiona siku ya leo. Kwa kweli, ni jambo kubwa sana kwangu kuona Waziri Mkuu wa nchi yangu ametaja jina langu mbele ya hadhara ya watu mashuhuri. Hii ni ndoto kubwa iliyotimia kwa ulimwengu wa roho."

Niffer ameeleza kuwa nia yake kuu ilikuwa kusaidia wahanga wa ajali hiyo, akisisitiza kuwa hakujua sheria zinazohusiana na uchangishaji wa fedha kwa ajili ya mafaa kama hayo. Alieleza:

"Nilikuwa tayari tangu mwanzo kutoa ushirikiano kwa Serikali na jamii kwa ujumla. Niliomba muongozo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa kabla ya kuanza zoezi hili. Ninaamini nia yangu haikuwa mbaya, na kupitia changamoto hii, nimeona umuhimu wa kuwa na taasisi inayotambulika rasmi, Niffer Foundation."

Waziri Mkuu Majaliwa, wakati akizungumza eneo la Kariakoo, alisisitiza kuwa hakuna mtu anayepaswa kuchangisha fedha bila kibali maalum kutoka serikalini na akatoa agizo kwamba Niffer atafutwe ili aeleze ni nani aliyempa mamlaka hiyo.

Baada ya agizo hilo, taarifa zilitolewa kuwa Niffer ameshapatikana na yuko tayari kushirikiana na mamlaka husika.
Huyu dada alikwishalalamikiwa sana na wafanya biashara wa Kariakoo kwa kuwharibia biashara zao.

Ni wakati sasa TRA waruke naye kuangalia kama analipa kodi ya mapato
 
Niffer ni mjanja sana kwenye mambo ya pesa ndio maana anatajirika haraka haraka

Hela za michango ya wahanga. Zinatumwa kwenye Lipa namba zenye jina lake.

Halafu idadi ya waliotuma pesa haijulikani. Majina yao na kiasi walichotuma hakiwekwi wazi. Yaani Hakuna Auditor

Kwa jinsi wa Tanzania walivyo wajinga. Huyu dada angepata mtaji mkubwa sana wa biashara zake kupitia hiyo michango.

Kwenye page yake ana wafuasi milioni moja na nusu. Imagine wafuasi Laki 5 tu. Wakituma shilingi elfu moja moja kila mmoja.. Niffer anakusanya milioni 500 fasta fasta.

Hapo anapeleka kwa wahanga milioni 200 kisha 300 anazibana.

Hakuna atakaye gundua
 
Kuchangisha mchango lazima uwe na kibali, nadhani kinatoka Polisi. Namuonaga hata Malisa anachangisha, lakini hainyeshi kibali kinachomruhusu. Kibali huepusha matapeli kujiingiza. Nashauri mamlaka zinazohusika zitoe elimu ya kuhusu kibali.

These people are not audited, wanatangaza kiwango wanachoona kinafaa, wasichotangaza haijulikani. Let the procedure ya michango iwe properly described
 
Back
Top Bottom