Nigeria ilianza kuchimba mafuta 1956, bado inauza mafuta ghafi nje na kununua yaliyosafishwa. Tanzania tutatoboa na gesi?

Wakati mwingine hata hao usalama taifa wanatimba kwenye rushwa ndiyo maana nchi inataabika kupata maendeleo haraka kama inavyo tarajiwa.

Kama usalama wangeweza kudill na wahuni wote wanaoisababishia nchi yetu hasara tungekuwa mbali sana.

Katiba mpya nimuhimu sana itakayo weka mufumo mzuri wa taasisi zote kusimamiana kwa masilahi ya nchi.

Kuliko sasa watu wanateuliwa na mtu mmoja na akifanya kosa haguswi
 
Hivii TIPER Refinery yetu kule Kigamboni bado kipo? Mbona bado tunaagiza mafuta kutoka nje, kulikoni?
 
Nchi zilizojaa rushwa haziwezi piga hatua yoyote ya maendeleo. Sababu zitakuwa kulalamika kuhusu wazungu kwamba wanakwamisha maendeleo kumbe ukweli ni kwamba hatuna akili ya kujitawala.
Wachina wananyonga Hawa mafisadi ambao ccm inawalea Kwa kuwa wote wameoza na kunuka rushwa
 
Nadhani umeongea vizuri sana, kuna external forces huwezi kuzikwepa kwenye uchumi wa dunia.
Sasa si jamaa wanatupenda mno na kutupatia msaada hapa inakuwaje wasitupe msaada tukajitegemea kwa hili wenyewe tukaanza kuwauzia.
 
Mkuu asante sana kwa bandiko lako.

Mkuu gesi inayozungumziwa kwenye huo mkataba sio CNG bali ni LNG. CNG ni gesi asilia iliyoshindiliwa. LNG ni gesi asili iliyokatika kimiminika.

Lengo la kuibadilisha gesi asilia kuwa katika kimiminika ni kurahisisha usafirishaji. Ni rahisi zaidi kiuchumi kuisafirisha gesi asilia kwenda katika masoko ya mbali hasa huko ulaya ikiwa katika hali ya kimiminika kuliko ikiwa katika hali ya gesi.

Lakini ikisha kufika mahali inapopelekwa kuuzwa itatakiwa ibadilishwe tena na kuwa katika hali ya gesi ili iweze kuingizwa katika bomba ili iweze kutumika kupikia majumbani.

Naomba kukazia tena ili gesi asilia iweze kutumika majumbani inatakiwa kuwa katika bomba (PNG). PNG ni piped natural gas.
 
Ni udumavu wa akili wa watawala wa kiAfrica ,kwani mbona Dangote kajenga refinery , wewe unafikiri wazungu watakuja wakujebfde refinery ya malighafi zako ?
Ni wajibu wetu serikali itengeneze sera nzuri na kuencorage wazawa matajiri hata kuungana na kuanzisha refineries za malighafi zetu na kuacha utegemezi wa nje .
Watawala wa Afrika wanawaza kutawala milele na kuiba mali za uma basi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…