Nihifadhi wapi akiba yangu ya fedha ili nipate faida ya angalau asilimia 10 kwa mwaka?

Nihifadhi wapi akiba yangu ya fedha ili nipate faida ya angalau asilimia 10 kwa mwaka?

Habari ndugu zangu,

Mimi nataka kuanza kuwekeza pesa zangu za ziada lakini sijui nihifadhi wapi ambako nitajitengezea angalau faida ya asilimia 10 kwa mwaka!

Naomba msaada kwa anayejua
Mkuu ushauri wangu
1. Wekeza kwenye hati fungani. Hii ni low risk investment ila inataka mtaji mkubwa ili uweze kuona faida ya maana.
2. Wekeza kwenye ardhi hasa kama unaishi maeneo ya Dar. Hakuna sehemu ambayo ardhi ya Dar inashuka thamani. Hapa risk yake ni kuwa makini wakati wa manunuzi usije ukaingia mikononi mwa matapeli.
3. Cryptocurrency. Hii high risk investment lakini ulipaji wake ni mkubwa sana. Kwa mwaka unaweza kupata faida hata mara 100 ya uwekezaji wako. Hii ni nzuri kwa mtu mwenye lengo la kuwekeza kwa muda mrefu kwani kuna kipindi coin zinashuka sana thamani kabla ya kupanda kwa fujo. Uwekezaji huu unakubidi utafute maarifa sahihi kwanza na kujiridhisha kabla ya kuwekeza.
 
Nunua viwanja vya bei nafuu. Siku ukihitaji hela yako unaviuza kwa cha juu kidogo. Na ni rahisi kuuza

Usinunue vya bei ghali vinauzika kwa mbinde sana
Tatizo la viwanja vya bei rahisi havijapimwa. Muhimu ni kuwa makini na matapeli usije ukauziwa kiwanja cha mtu.
 
Tafuta Vijana waaminifu watano (5) esp. Me. ingia nao Mkataba wa Biashara (Biashara ndogo-ndogo less than 300,000/=) na marejesho yawe ni kila mwezi 10%. Chunguza/Jifunze kwa waendesha bodaboda. Kila wiki 40,000/= au kila siku 7,000/= au shughuli inayofanana na hizo. Wengine hutumia fedha yako kufanya biashara na kile kinachopatikana huchukua cha juu na ww wanakupa albaki.

Tafuta Vijana waaminifu watano (5) esp. Me. ingia nao Mkataba wa Biashara (Biashara ndogo-ndogo less than 300,000/=) na marejesho yawe ni kila mwezi 10%. Chunguza/Jifunze kwa waendesha bodaboda. Kila wiki 40,000/= au kila siku 7,000/= au shughuli inayofanana na hizo. Wengine hutumia fedha yako kufanya biashara na kile kinachopatikana huchukua cha juu na ww wanakupa albaki.!!!🤪
Hii njia sishauri. Inabidi uache kazi ufanye kazi kweli. Kuwafuatilia wakulipe kwa wakati na wasikudhulumu.
 
Mkuu kama bado hujafanikiwa mi nafanya kazi benki flani kubwa hapa nchini naomba uni pm nikuelekeze njia nzuri ya kuwekeza pesa zako hata kama hautowekeza katika benki yetu
 
Mkuu kama bado hujafanikiwa mi nafanya kazi benki flani kubwa hapa nchini naomba uni pm nikuelekeze njia nzuri ya kuwekeza pesa zako hata kama hautowekeza katika benki yetu
Ebu tuoe ushauri million 40 tuwekeze wapi
 
Mkuu kama bado hujafanikiwa mi nafanya kazi benki flani kubwa hapa nchini naomba uni pm nikuelekeze njia nzuri ya kuwekeza pesa zako hata kama hautowekeza katika benki yetu
Mkuu kama hutojali tuwekee hapa ili tufaidike wengi.
 
Mkuu kama hutojali tuwekee hapa ili tufaidike wengi.

Sahihi kabisa
Mambo ya kuitana PM kuna kaharufu flani kanakuja na kukataa
Ila Vizuri share na Wote kama mtoa mada alivyouliza kwa wote ni public knowledge tuu

Au unataka ukamsokote kwa pembeni
 
Mkuu kama bado hujafanikiwa mi nafanya kazi benki flani kubwa hapa nchini naomba uni pm nikuelekeze njia nzuri ya kuwekeza pesa zako hata kama hautowekeza katika benki yetu
Mkuu tafadhali*share* kwetu wote ...ni ombi lakini!
 
Utt inakidhi hitaji lako, kama wachache wengine walivyoshauri huko juu. Uzuri wake hata haifix muda, yaani kwamba eti lazima fedha zikae si chini ya kipindi fulani. Kipindi ni hiari yako.
 
Back
Top Bottom