Ilichabangwa 4 kwa 1 na Simba, mwaka 1994, Mzee wa Kiminyio Madaraka Selemani alimtesa Kimanda kweli kweli, baada ya hapo Kimanda alikimbilia uarabuni, ni enzi za Yanga kandambili RIP MpondelaTimu kali kama hii utaifungaje kwa mfano?
Walikula mlungula wa Gulamali akiwa mfadhili Yanga ili kuupindua uongazi wakaandaliwa bakora na kutokanyaga jangwani kasoro Kimanda pekee, mwaka uliofuata timu yote ikavunjwa ikaundwa Yanga yoso ya akina Anwar Awadhi na Maalim Salehe RomarioTimu kali kama hii utaifungaje kwa mfano?
Nimekubali mchango wako!
Constantine Kimanda
Constatine Kimanda alikuwa ni beki wa kati au mkoba wa Yanga na timu ya taifa ya Burundi na sio Congo DRC.
Ilikuwa ni mwaka 1994 alipochezea Yanga ambapo alisajiliwa chini ya uongozi wa katibu mkuu wa wakati ule marehemu George Mpondela.
Alikuwa pamoja na marehemu Method Mogella ambae waliuzwa wote na Mpondela kwenye timu ya uarabuni ya Sharjah FC.
Yanga ya mwaka 1994 ilikuwa ni kali kwelikweli kina Steven Nemes Sekilojo Chambua, Mohamed Hussein au "Mmachinga", Nico Bambaga, Edibily Lunyamila, James Tungaraza "Boli Zozo", na Salvatory Edward.
Wengine akina Said Mwamba Kizota, marehemu Salum Kabunda "Ninja", Issa Athuman, Keneth Mkapa, Selemani Mkati, Rifati Said, Sanifu Lazaro, David Mjanja na Mwanamtwa Kihwelu.
Wachezaji wengine walikuwa ni Allly Yusuf "Tigana", Willy Martin, Ngadu Ramadhan, Joseph Lazaro, Willy Mtendamema.
Mwaka 1994 ndipo kulitokea mgogoro mkubwa kwenye klabu hii na kukazaliwa Yanga Asili na Yanga kampuni.
Hivyo Yanga kampuni chini ya Marehemu Mpondela ikaenda kufungwa goli 4-1 na Simba na baaada ya hapo wachezaji wote wa kikosi cha kwanza wakatimuliwa.
Kimanda ndiye aliefunga goli pekee la Yanga.
Baada ya mgogoro huo kipa Rifat Said alirudi Zanzibar, Edibily Lunyamila akaenda Malindi ya Zanzibar na Saidi Mwamba pamija na Steven Nemes wakahamia Simba.
Ndipo Kocha wa Yanga Tambwe Leya akaamua kusuka kikosi kipya cha Yanga kilichokuwa na wachezaji kama Anwar Awadh, Mzee Abdallah, Silvatus Ibrahim “Polisi”, Maalim Saleh “Romario”, Nonda Shaaban “Papii”, Bakari Malima na Kally Ongala.
Wengine akina Seki Chambua Salvatory Edward na wengine.
Vijana hawa waloitwa Black Stars ndiyo waloiwezesha Yanga kuja kucheza nane bora mwaka 1998 ya klabu bingwa Afrika na baadae mwaka 1999 wakanyakuwa ubingwa wa Afrika Mashariki.
Edibily Lunyamila na Mohamed Hussein.
Kimanda kwa sasa anaishi na kufanya kazi nchini Ubelgiji.
Alicheza mechi mbili, mechi ya kwanza Yanga ilishinda goli 2-0 magoli yote yalifungwa na marehemu James Tungaraza aka Boli Zozo .
Nimekumbuka kikosi cha kina eustas bajuala beki WA kushoto WA yanga mwaka 99 kiliwafunga nakivubo sports club villa kampala na kuchukua kombe la afrika mashariki na kati.
serikali ikatuma ndege kwenda kuchukua timu Uganda waziri mkuu sumaye akaipokea timu airport.
Huyo nimemsahau nikumbusheUnamkumbuka Beki Patrick Ntambwe
Na kocha alieipeleka yanga ligi ya mabingwa afrika ilipoanzishwa mwaka 1998 alikuwa TITO MWALUVANDAaliyeunda yanga mpya 97-2000 alikuwa kocha mzaire RAUL SHUNGU
Alikua ana rasta miaka ya 99/2002Unamkumbuka Beki Patrick Ntambwe
Bila kusahau Banza TshikalaUnamkumbuka Beki Patrick Ntambwe
R.i.p Mwalimu wangu TitoNa kocha alieipeleka yanga ligi ya mabingwa afrika ilipoanzishwa mwaka 1998 alikuwa TITO MWALUVANDA
Tshikala alikuwa raia wa nchi gani?Bila kusahau Banza Tshikala
Congo DRCTshikala alikuwa raia wa nchi gani?
Bila kusahau Banza Tshikala
Nasikia siku hizi ni mchungaji ana Kanisa lakeBila kusahau Banza Tshikala
Dah! Umenikumbusha huyu jamaa! Yaani alikuwa anajua hadi anaboa!Nimekuwa nikisikia sifa za mchezaji wa zamani wa Yanga, Costantine Kimanda kwamba alikuwa ni mchezaji wa aina yake. Najua humu kuna wakongwe sio mbaya mkatujuza kuhusiana na mchezaji huyu wa kipare aliyetamba miaka ya 90 Jangwani.
Yap nilisikia hiyo muda mrefu tuu,kama ilivyo Taribo West wa NigeriaNasikia siku hizi ni mchungaji ana Kanisa lake