Nijuzeni, Kwanini zisiwepo noti na sarafu zenye picha ya Jakaya Kikwete, Benjamin Mkapa na rais Magufuli? Ianzishwe na noti ya elfu hamsini

Sijui huwa mnakunywa nini?...eti Raisi ni muwakilishi wa Muumba, kwa hiyo kina Idd Amini, Hitler, Bokasa, Mobutu na wengine walimuwakilisha Muumba?
Hats hao Muumba aliwaweka madarakani ili atukuke,huwezi jua huenda vizazi vya nchi hizo vilikuwa na mako's Fulani ndiyo wakaletwa wa kuwaadhibu.pia Rejea maandiko Mungu aliandaa Wafalme ili kuondoa ufalme Fulani wote wake ila lengo atukuke
 
Kama vipi marais wote kwenye noti moja!

Noti ya 200 Cedis ya Ghana ina watu 6 upande mmoja,ukiiangalia utadhani "concert poster" ya WCB.
 
Kadiri uchumi unapokua noti kubwa kubwa zinapungua hela inakuwa sarafu manoti makubwa ni ishara ya uchumi mdogo na kuyumba
 
Asante kwa uchambuzi,lakini huoni rais kutokuwemo ktk noti ni kama tumemdhurumu haki yake,watu wangependa kuongozwa na rais wanaemuona kila Mara baada ya kuitumikia fedha inaleta nguvu Fulani kupokea ujira wako ukiiangalia noti unamuona na Rais
Kumbe shida yako sio Mkapa/Kikwete bali Magufuli aonekane kwenye noti
 
ebu ngojaaa hii ya rais kumwakilisha muumba umeipata wapi?
 
USD note zina sura za marais wangapi?
Watano mkuu
Dollar 1 George Washington
Dollar 2 Thomas Jefferson
Dollar 5 Abraham Lincoln
Dollar 20 Andrew jackson
Dollar 50 Ulysses Grant

Ila pia kuna dollar 10 Ambayo yupo Alexander Hamiliton First Secretary of treasury na Dollar 100 yupo Benjamin Franklin ambae alikuwa physician pia was amongst Founding Fathers miongoni mwa wale Saba akiwemo Hamiliton pia
 
Yeah sahihi. Hili swali nililenga mtoa mada ajifunze kupitia jibu lake.Wanaokaa mbele ya note mara nyingi ni waasisi au waliofanyia nchi mambo makubwa kipindi nchi husika inajijenga.Yamkini Rais wa sasa au awamu yoyote ile huko miaka ya mbele akaonekana ametufanyia kitu kikubwa kipindi chake kiasi cha kukumbukwa sana. Tutamuweka naye.Ila huu utaratibu wa kubadilisha note kipindi Rais mwingine akiingia madarakani,mtoa mada,haupo!
 
Asante kwa uchambuzi,lakini huoni rais kutokuwemo ktk noti ni kama tumemdhurumu haki yake,watu wangependa kuongozwa na rais wanaemuona kila Mara baada ya kuitumikia fedha inaleta nguvu Fulani kupokea ujira wako ukiiangalia noti unamuona na Rais
Vipi kama ujira wenyewe huna?

Vipi kama unayetaka kumuona ndo kakufanya usiwe na ujira?

Tushajua nia yako katika kutaka awamu gani ikae kwenye fedha,tulia watu wana hasira hela hamna.

Kama mnataka nguvu itumike,itumike katika kutengeneza ajira sio pesa.

Hakuna anaezulumiwa,ila pia itakuwa ni matumizi mabaya ya fedha za Umma,yan kila moaka 10 hela iwe na chapa mpya?

Inawezekana ila ni matumizi mabaya ya fedha za Umma
 
Unaweza kushangaa unalala na noti ya 10000 unaamka na noti ya buku...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…