Nikasema leo niangalie huyu wanaesema Pele alikuaje enzi hizo. Kweli alikuwa nuksi

Sasa unadhani ubora Wa uwanja hauongezi ubora Wa mchezaji? Na unafikiri kwanini wanaboresha ubora Wa viwanja.

Niambie timu inavyocheza Mkwakwani in sawa Na inavyocheza Taifa Dar es Salaam?

Sent from my HUAWEI Y625-U32 using JamiiForums mobile app
Si ndomana nmekubal kua wachezaj wa bongo ni bora kuliko wote dunian.
 
Pov la nin sasa mkuu,hapa si majadiliano tuu,..uswahil mwiiing,kama unaona vp usichangie uzi

Mkuu Napoleone samahani aise kama nimekudisturb....but ukweli ndio huo,,, u know that huyo pele huwa namfananisha na cr7 tabia zake, kidogo zinaendana endana na uzee pia unachangia mtu analopoka hovyo. "Mtu anajitangazia kuwa yeye ni mfalme wa soka na hakuna kama yeye" huo tuite ni uchizi ama??? Huyo pele wako namzungumzia mkuu,, baada ya kuona mtoto wa kiargentina kampiga chini babu wa watu akaamua kutoa ya moyoni.....

  1. Messi
  2. ......No body
  3. Maradona
  4. Pele
  5. Alfredo
  6. Cruiff
  7. Zidane
  8. Requelme
  9. Cr7
  10. Puskas
  11. Di lima
 
Kweli kabisa. Kubeba kombe la dunia isiwe sababu ya kuwa best player ever. Waliobeba kombe la dunia wapo wengi sana.

Mkuu Labda umwekee orodha kamili kama ndio kigezo chake 😀😀

Iniesta
Xavi
Muller
Fabregas
Gotze
Ozil
Khedira

Mkuu wazoee tu wabongo....
Mti wenye matunda siku zote hupigwa mawe "MESSI"
Mti wenye matunda siku zote hupigwa mawe "MESSI"
mti wenye matunda siku zote hupigwa mawe "MESSI"


 
Ila messi ni habar nyingne,yaan anacheza kwenye ulimwengu wa mpira wa science na elim ya darasan lakin bado anatupia,..enz za hawa wa zaman,competition ilikua sio kubwa,so best player wa miaka hii na miaka ile,wana utafaut mkubwa
Nafikiri umeanza kuangalia mpira miaka ya hivi karibuni! Kwa taarifa, vipaji vilikuwa zamani sio sasa na ndio maana wachezaji waliotisha kama kile kikosi hatari cha Brazil cha 1970 walipochukua kombe la dunia mara tatu na kulichukua moja kwa moja hakijawahi kutokea kikosi bora kama cha wakati hule! Ndio maana hata hapa Tanzania hadi leo ukiondoa mwaka 1980 wakati Tanzania kwa mara ya kwanza na ya mwisho kushiriki African Cup of Nations tukiwa na kikosi cha akina Tenga hakuna wachezaji wa kiwango kile waliowahi kutokea hadi sasa. Sio mpira tu, kuja kwenye ngumi, kumbuka bondia aina ya Muhammed Ally, George Fomen, Freizer, Spinks na wengine wengi. Ndungu yangu kwa vipaji ilikuwa zamani ktk nyanja nyingi bila kusahau riadha ya akina Filbert Bayi na Juma Ikangaa nk lkn sasa hivi tunafuta tumpeleke nani msimu Olympic games.
 
Messi amepiga chini Pele kivipi? Tujadiri kwa busara.
 
Nimeangalia tena magoli ya pele, HAYANA skills, ni mazuri kwa kizazi hicho ila kwa kweli kwa sasa tuko advanced. Hayana nafasi.
Alafu wachezaji wa zamani hata hawajui kushangilia.
Ni kosa kubwa kumlinganisha Pele aliyebeba ndoo tatu za kombe la dunia na Messi. Kwanza hawa viumbe wameishi ktk nyakati tofauti kabisa. Mlinganishe Messi na mpinzani wake Cristiano Ronaldo sio Pele au Maradona ni kosa la ufundi sana.
 
Ni kosa kubwa kumlinganisha Pele aliyebeba ndoo tatu za kombe la dunia na Messi. Kwanza hawa viumbe wameishi ktk nyakati tofauti kabisa. Mlinganishe Messi na mpinzani wake Cristiano Ronaldo sio Pele au Maradona ni kosa la ufundi sana.
Ni mtazamo wako, kwangu naona kama alikuwa na skills za kawaida tu. Messi ronaldo na DINHO ni zaidi ya pele. Kuna uwezekano aliocheza nao hawakuwa na ujuzi sana wa kisoka.
 
CR7 ndio angeshindwa kucheza enzi hizo ila Messi kwa kina ya uchezaji wake ni ule mpira Wa mtaani kabisa ule ndugu,yule jamaa anavyorukaga vihunzi na si mlalamishi sana wala kujiangusha sana anngeweza kucheza hata ndondo za enzi hizo unacheza huku unapigwa mikwara na wacheza na mashabiki na bado mpinzani anayekukaba anahamasishwa akutie kidole.
 
Na pele,maradona na messi,ili kufuta ubishi
U can't compare Pele na Messi ndungu, ni sawa wewe tuku-compare na mzazi wako, different things. Hawa viumbe wameishi ktk nyakati tofauti kabisa. Pele amebeba ndoo tatu za kombe la dunia wakati wake, Messi hajabeba hata kombe moja hata la America ya kusini. Messi anacheza mpira Europe miaka yake yote, Pele hajawahi kucheza mpira Europe bali Latin America na USA. Hawa ni watu wawili tofauti, you can't compare them at all.
 
Ni mtazamo wako, kwangu naona kama alikuwa na skills za kawaida tu. Messi ronaldo na DINHO ni zaidi ya pele. Kuna uwezekano aliocheza nao hawakuwa na ujuzi sana wa kisoka.
Ukitaka kujua vipaji vya wanandinga njoo kombe la dunia. Messi ambaye hajachangia kutwaa kombe la Latin America wala Kombe la dunia huwezi kum-compare na Pele au Maradona hata kidogo. Messi akija timu ya taifa ana-struggle sana.
 
Suala la viwanja sio ishu. Mbona watu wanatupia tu uku uswazi na viwanja vibovu. Tena hakuna kiwanjia kilicho na kazi kufunga kama viwanja vya sasa. Zaman ukipiga ukadunda lazima liwe goli. Tena magoli ya Pele siyakubali tu nashangaa wanamuacha Chitaru wa Zambia.
 
Ukitaka kujua vipaji vya wanandinga njoo kombe la dunia. Messi ambaye hajachangia kutwaa kombe la Latin America wala Kombe la dunia huwezi kum-compare na Pele au Maradona hata kidogo. Messi akija timu ya taifa ana-struggle sana.
Kombe la dunia sio la mtu mmoja mmoja, ni timu work.
Kwani ngazi ya vilabu pele ana vikombe vingapi vyenye hadhi??
 
Messi hatoweza kucheza kiwanja kibovu wakati vizuri vipo. Sema we akili yako inakutuma ni ngumu Ku_score kiwanja cha mchangani wakati mtaani huku wanafungana magoli daily. Ujue suala la mchezaji kushindwa kucheza kiwanja kibovu ni Psychology tu. Messi hawez kucheza rough pitch hatomudu maana ameshajengwa kucheza pitch nzuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…