Nikiangalia marafiki niliohitimu nao primary hadi naomba

Pole sana ndugu ila usikate tamaa siku yako ipo. Mimi haya mambo yalinitokea mwaka jana . lakini nashukuru mungu alijibu maombi yetu mimi na mke wangu. Jaribu tu kujenga urafiki na watu, asijifungie ndani masaa yote. Huwa unachukua muda kutembea sehemu mbali mbali piga story na watu .
 
My dad he is my role model.

Baba yangu alikuwaga na akili za kawaida darasani ,alipomaliza la saba miaka ile hakufaulu kutokana na uhaba wa shule wa miaka ile ndugu zake wakampeleka shule binafsi maana wazazi wake walikuwa wamefariki tayari alisoma form one na form two akaridhika akawambia Dada zake elimu ya secondary imemtosha maana lengo lake ilikuwa ni kufahamu kingereza .

Aliacha elimu ya sekondari akaenda kujiunga na chuo cha ufundi ,alijenga uaminifu kwa watu na kuitendea haki taaluma yake ya ujenzi .

Huwezi kuamini baba yangu anamiliki kampunin tatu za ujenzi ana magari ya biashara sio chini ya 20 garage kibao nyimba na mahotel kadhaa INA miradi ya biashara kawaajiri hata wale waliopiga kitabu zaidi.

Baba yangu cheti cha form four hana ila inapiga kazi zaidi ya maengineer waliosoma urusi
 

Ur better than them, nenda na mwendo huo huo.
 
Reactions: SDG
 
Maisha sio kushindana mkuu, kuna wangap walishia darasa la saba bado maisha yao ni magumu, mimi naamini kuwa jinsi ulivyo ndo ilipangwa iwe, kila mtu atakufa kifo chake ndo maisha yetu yalivyo
Pambana leo kesho yako iwe nzuri zaidi ya Jana yako na sio leo ya mwanadamu mwenzako
 
Ndio maisha yalivyo,tena usipoangalia wale uliokuwa hata ukiwazidi kiuwezo darasani ndio maisha yao yako juu hatari.Jipe moyo,mwamini Mungu,muombe akupe amani ya moyo na furaha kwani hivyo vyote walivyonavyo wataviacha hapahapa duniani.
 
Kila mja na riziki yake mkuu,inawezekana hata ungeishia hilo darasa la saba bado mpaka leo ungekuwa huna lolote,Mungu ndio hupanga lini na saa ngapi atakupatia,usilaumu,safari bado.shukuru kwa kila jambo kuna wengine hata hiyo elimu hawajaipata.
Umenena vema mkuu
 
mama yangu ni mhadhiri hapo udsm.. alituambia ukweli tangu tunasoma sekondari..

hataki mwanae yeyote asome kama yeye kama ana kichwa cha kufanya biashara..

yeye anasomesha mtoto hadi digrii tu zaidi ya hapo atakupa mtaji au kupush biashara yako.

kama unataka master au phd. jisomeshe mwenyewe sababu anasema ni ujinga kupoteza ada za master au phd kisha ukaajiriwe utegemee kuongezwa mshahara..

hataki maisha ya duni kwa kizazi chake kama aliyonayo yeye.. mshahara less than 5m huku ana mavyeti kibaooooo..

aliowapita darasani wengi wao ni matajiri wa kutupa...

yeye kaishia kufundisha watoto udsm tu huku hana financial freedom.



 
Tunaomba utuunganishe na babaako tumuombe kazi ili nasi tufanikiwe
 
Kuwa na subira, good things come to those who wait.
 
Reactions: SDG
Halafu unakuta wamekupita na vitu vidogo sana lakini kwasababu huna kitu unaona vitu vikuubwa.
 
kumbuka riziki mafungu saba ya kwako bad usiwe na harak
 
Reactions: SDG
ila ht mm nikiipigia hesabu miaka 2 ya a level, 3 ya chuo na 2 mingine ya kusugua bench kusubir kuajiriwa naona ningeitumia effectively nisingekuwa hapa nilipo leo,,ila famililaii sio kesi ni suala la muda tuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…