Nikipata pesa sijengi msikiti/kanisa kwanza kwa sababu hizi

Nikipata pesa sijengi msikiti/kanisa kwanza kwa sababu hizi

safuher

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2019
Posts
11,837
Reaction score
17,412
Mtu akikamata vijisenti utaona anajenga msikiti/kanisa kuuuubwaaa kwao.

Jiji la dar lina nyumba za ibada (kanisa/msikiti)karibia kila kona na watu hawajai, ila jiji la dar hospitali zinajaa sana, foleni za maji zinajaa sana, shule zinajaa sana.

Mtu anajenga nyumba ya ibada kijijini kisha wanakuja kusali watu watano tu,wakati huo kijiji hiko hiko kwenye huduma za afya au shule kuna watu kibao.

Nikipata pesa sitojenga nyumba ya ibada kwanza kwa sababu hiyo iliyokuepo haijai na kama kujaa kwa siku moja moja.

Nitajenga shule kwa sababu zilizokuepo zinajaa wanafunzi hawatoshi.

Nitajenga zahanati kwa sababu zilizokuepo zinajaa wagonjwa hawapati matibabu bora.

Nitanunua vitanda kwa sababu vilivyokuepo havitoshi watu wanalala wawili wawili n.k

Nitanunua madawati kwa sababu wanafunzi wanakaa chini na kuchafuka huku wakiongeza gharama ya sabuni.

Nikijenga msikiti/kanisa nitapata thawabu kwa wanaokuja kuabudu pekee na ni wachache hao wanaoabudu.

lakini nikijenga shule, kununua madawati, kununua vitanda hospitali, kujenga zahanati hapa nitapata thawabu hata kwa wasiokuwa wana ibada kwa sababu zahanai, vitanda, madawati hayachagui dini zote wanatumia.

Nikinunua misahafu watakaosoma ni waislamu wachache lakini nikichimba kisima watatumia wakristo, waislamu na hata wapagani na Mungu atanilipa kwa kila mtu anayetumia huduma hiyo.

Kwa mantiki hiyo kujenga nyumba za ibada na kujenga huduma zajamii zinazotumiwa na dini zote kwangu naona kujenga huduma za jamii ndio bora zaidi kwa sababu huduma hizo zitatumiwa na dini zote.

Sisemi ni vibaya kujenga nyumba a ibada lakini ni vizuri zaidi kuanzisha huduma za jamii ambazo wana jamii wanateseka nazo.

Nenda vijijini hakuna msikiti/kanisa linalojaa kwamba watu wengine wakawa wanasali nje hakuna.

Lakini angalia shule za vijijini na zahanati,na huduma za maji hizo foleni ndio utagundua ni wapi uweke kipaumbele.

Kwa sasa katika dini jambo la muhimu ni kuwahimiza watu washike dini na waijue na sio kujenga nyumba za ibada wakati watu wanakufa njaa na kiu na magonjwa mbali mbali.
 
Kumbe kuna watu wana fikra za kujenga makanisa na misikiti wakipata hela?

Mi nikipata hela nabomoa misikiti na makanisa

Sijui ndio sababu sizipati?
Utazipata tu Mungu hana kinyongo kwamba asikupe kwa sababu ya nia yako ambayo inakusudi la kuharibu nyumba za ibada za wengine
 
Ukiona mtu anajenga Kanisa na Msikiti wakati watu hawana hata Kakiwanda kadogo kakuongeza thamani mazao yao huyo ni Mbinafsi anataka wabaki Masikini wakimuabudu.
Hahah inatakiwa ajikite kwenye mambo ambayo jamii inahitaji zaidi sio mambo anayoyahitaji yeye
 
Mtu akikamata vijisenti utaona anajenga msikiti/kanisa kuuuubwaaa kwao.

Jiji la dar lina nyumba za ibada (kanisa/msikiti)karibia kila kona na watu hawajai, ila jiji la dar hospitali zinajaa sana, foleni za maji zinajaa sana, shule zinajaa sana.

Mtu anajenga nyumba ya ibada kijijini kisha wanakuja kusali watu watano tu,wakati huo kijiji hiko hiko kwenye huduma za afya au shule kuna watu kibao.

Nikipata pesa sitojenga nyumba ya ibada kwanza kwa sababu hiyo iliyokuepo haijai na kama kujaa kwa siku moja moja.

Nitajenga shule kwa sababu zilizokuepo zinajaa wanafunzi hawatoshi.

Nitajenga zahanati kwa sababu zilizokuepo zinajaa wagonjwa hawapati matibabu bora.

Nitanunua vitanda kwa sababu vilivyokuepo havitoshi watu wanalala wawili wawili n.k

Nitanunua madawati kwa sababu wanafunzi wanakaa chini na kuchafuka huku wakiongeza gharama ya sabuni.

Nikijenga msikiti/kanisa nitapata thawabu kwa wanaokuja kuabudu pekee na ni wachache hao wanaoabudu.

lakini nikijenga shule, kununua madawati, kununua vitanda hospitali, kujenga zahanati hapa nitapata thawabu hata kwa wasiokuwa wana ibada kwa sababu zahanai, vitanda, madawati hayachagui dini zote wanatumia.

Nikinunua misahafu watakaosoma ni waislamu wachache lakini nikichimba kisima watatumia wakristo, waislamu na hata wapagani na Mungu atanilipa kwa kila mtu anayetumia huduma hiyo.

Kwa mantiki hiyo kujenga nyumba za ibada na kujenga huduma zajamii zinazotumiwa na dini zote kwangu naona kujenga huduma za jamii ndio bora zaidi kwa sababu huduma hizo zitatumiwa na dini zote.

Sisemi ni vibaya kujenga nyumba a ibada lakini ni vizuri zaidi kuanzisha huduma za jamii ambazo wana jamii wanateseka nazo.

Nenda vijijini hakuna msikiti/kanisa linalojaa kwamba watu wengine wakawa wanasali nje hakuna.

Lakini angalia shule za vijijini na zahanati,na huduma za maji hizo foleni ndio utagundua ni wapi uweke kipaumbele.

Kwa sasa katika dini jambo la muhimu ni kuwahimiza watu washike dini na waijue na sio kujenga nyumba za ibada wakati watu wanakufa njaa na kiu na magonjwa mbali mbali.
Bonge la idea. Lakini wenye mawazo mazuri hawapatagi hela!
 
Point yako mzuri, sema huwenda mtu akakuelewa vibaya kutokana na ulivyoiwasilisha.

Lakini nakubaliana na wewe ya kuwa, tunatakiwa kuweka huduma sahihi ambayo inahitajika na jamii husika na sio kuegemea upande mmoja au kuweka huduma fulani sehemu ambayo haihitajiki zaidi.

Na wala asije akadhani mwenye kudhania kuwa thawabu atazipata kwa kujenga nyumba ya ibada pekee au thawabu atazipata tu eti kwa kuwa amejenga zahanati.

Bali pia inatakiwa kuzingatia na kuweka huduma sahihi katika mahali sahihi.

kila jambo linaumuhimu wake.
 
Point yako mzuri, sema huwenda mtu akakuelewa vibaya kutokana na ulivyoiwasilisha.

Lakini nakubaliana na wewe ya kuwa, tunatakiwa kuweka huduma sahihi ambayo inahitajika na jamii husika na sio kuegemea upande mmoja au kuweka huduma fulani sehemu ambayo haihitajiki zaidi.

Na wala asije akadhani mwenye kudhania kuwa thawabu atazipata kwa kujenga nyumba ya ibada pekee au thawabu atazipata tu eti kwa kuwa amejenga zahanati.

Bali pia inatakiwa kuzingatia na kuweka huduma sahihi katika mahali sahihi.

kila jambo linaumuhimu wake.
Kwa sasa hivi kujenga huduma za jamii ni bora kuliko kujenga msikiti kwa mujibu wa hali za watu.

Ila kwa mujibu wa matakwa ya mtu inawezekana akaona kujenga msikiti au kanisa ndio bora zaidi kwa kuwa wau wanafanya ibada humo,sio tatizo.

Ukiangalia watu nenda kijijini waulize kati ya msikiti/kanisa na kuwajengea kisima cha maji safi ya kunywa kipi bora utaona majibu yao.

So kwa kuangalia mahitaji ya jamii basi huduma za jamii tuzipe kipaumbele sana kwa sababu watu wengi bado hata muamko wa dini ni mdogo.

Kwa sasa kwemye upande wa dini watu wajikite kuelimisha katika mitaa huku wananchi wakipata huduma za jamii safi.
 
Bonge la idea. Lakini wenye mawazo mazuri hawapatagi hela!
Aisee mimi nadhani jitihada na kuomba mungu na kuumiza kichwa njia ipi mtu itamtoa na sio kukaa ukivumbua id3as mbalimbali huku mtu hajishughulishi na chochote
 
Tafutaneni 1000 wenye mawazo kama yako, changeni Sh1000 kwa mwezi. Mwaka mmoja Sh12m.
Fanyeni shughuli za huduma za jamii.
 
Back
Top Bottom