Nile chakula gani tofauti na wali na ugali kwa muda wa wiki mbili mfulizo?

Nile chakula gani tofauti na wali na ugali kwa muda wa wiki mbili mfulizo?

Hivyo nimemtajia yeye ambae hataki wali na ugali

Mi nilipokuwa najipunguza milikuwa nakula mayai, nyama (hadi kitimoto)
Maziwa ya aina zote (full cream milk)
Mboga za majani
Matunda nilikuwa nakula matango na maparachichi
Na nilikuwa nakula mboga zote za majani pamoja na kabichi
Ila nilikuwa nakula pia maharage na wali hii japo mara moja kwa miezi kama mitatu, hii nilishindwa kuacha kabisa sababu napenda mno na nilipunguza sana alcohol nilikuwa nakunywa red wine tu tena weekends na sio zote
Na nilipungua toka 89kg mpaka 64kg
Sasa hivi nimeongezeka kidogo nna 68 ila nataka nirudi 64kg mpaka kufika october mwaka huu

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Ok nimekuelewa, vipi mazoezi hayakuhusika pia ila diet tu!?!??

Nakubaliana nawe kwenye ulaji wa mboga za majani,matunda ila mie hupenda kuongeza mazoezi ili nipate majibu mazuri.

Huwa nikipunguza wanga napunguza pia na red meat nakuwa situmii kila mara..
 
Ok nimekuelewa, vipi mazoezi hayakuhusika pia ila diet tu!?!??

Nakubaliana nawe kwenye ulaji wa mboga za majani,matunda ila mie hupenda kuongeza mazoezi ili nipate majibu mazuri.

Huwa nikipunguza wanga napunguza pia na red meat nakuwa situmii kila mara..
Mi mazoezi sikufanya kabisa,
Nakula nyama sababu ndio chakula pekee ambacho kina viturubisho vingi vya kutosha mwilini, na kiukweli nyama ni tamu sana kuacha kula[emoji2][emoji2][emoji2]

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Mi mazoezi sikufanya kabisa,
Nakula nyama sababu ndio chakula pekee ambacho kina viturubisho vingi vya kutosha mwilini, na kiukweli nyama ni tamu sana kuacha kula[emoji2][emoji2][emoji2]

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Hahah kuhusu nyama..sina ugeni na wewe nakuelewa vizuri tu,ila mie huwa najitahdi tu sababu wanga+Nyama nyekundu = lehamu ya kutosha
 
Hahah kuhusu nyama..sina ugeni na wewe nakuelewa vizuri tu,ila mie huwa najitahdi tu sababu wanga+Nyama nyekundu = lehamu ya kutosha
Kuna mambo mengi sana hapo kwenye Lehemu ambayo inaonekana hujayafatilia kwa undani,
Trust me sio mbaya kama wanavyotuaminisha,
Ukiamua kufatilia hili kwa mapana na marefu utaelewa kuwa haina shida kihivyo


Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Hapo kuna mambo kadha wa kadha ya wewe kutuambia kabla ya kukushauri juu ya vyakula mbadala.

Mafano;

1. Je wewe ni jinsia gani?

2. Je umri wako ukoje?

3. Una familia?

4. Shughuli ya/zako ya/za kiuchumi zikoje?

Kwamba ni za kutumia misuli au akili au computer?

5. Unamotisha yoyote nyuma inayokupelekea kuweza kutambua aina ya vyakula?

Matharani ; uko na Mpango wa kupunguza uzito au ku mentain uzito ulonao n.k!

6. Je una changamoto yoyote ya kiafya inayokupelekea kujua vyakula fulani vya kufaaa?!

N.k!
 
Kuna mambo mengi sana hapo kwenye Lehemu ambayo inaonekana hujayafatilia kwa undani,
Trust me sio mbaya kama wanavyotuaminisha,
Ukiamua kufatilia hili kwa mapana na marefu utaelewa kuwa haina shida kihivyo


Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Naijua sana kwa undani wake,
Mie pia si mfuasi wa kuambiwa nyama ndio tatizo naelewa fika kuwa wanga ndio shida zaidi kuliko hata nyama..

Naelewa pia lehamu si mbaya mwilini ila kuna namna yake ya kuicontrol:Mfano ikiwa nyingi huweza kusababisha hatari ya shinikizo la juu la damu,pia magonjwa ya moyo hivyo basi lazima tujizatiti iiishie tu kwenye level ya Good Cholesterol..

Triglycerides....Hii ikiwa juu kwenye damu huweza sababisha hata Stroke,Diabetes:::: Sasa basi tunawezaje kuicontrol Total Cholestrol ili iwe vizuri katika kila level be it Low density Lipoprotein(LDL) au High density Lipoprotein(HDL)au Good Cholesterol!??

Mazoezi ni muhimu na kupunguza intake of Wanga kama tulivyokubaliana na red meat to be specific( kitimoto )na vyakula vingine vyenye fat ila tule kwa uangalifu....
 
Hapo kuna mambo kadha wa kadha ya wewe kutuambia kabla ya kukushauri juu ya vyakula mbadala.

Mafano;

1. Je wewe ni jinsia gani?

2. Je umri wako ukoje?

3. Una familia?

4. Shughuli ya/zako ya/za kiuchumi zikoje?

Kwamba ni za kutumia misuli au akili au computer?

5. Unamotisha yoyote nyuma inayokupelekea kuweza kutambua aina ya vyakula?

Matharani ; uko na Mpango wa kupunguza uzito au ku mentain uzito ulonao n.k!

6. Je una changamoto yoyote ya kiafya inayokupelekea kujua vyakula fulani vya kufaaa?!

N.k!
Maswali yote ni yamsingi ila yanajibu moja tu. Ni kutaka kubadilisha mfumo wa ulaji tu sio tangu kuzaliwa ugali wali vyaonekana kuwa vyakula vikuu huku kwetu uswahilini.
 
Naijua sana kwa undani wake,
Mie pia si mfuasi wa kuambiwa nyama ndio tatizo naelewa fika kuwa wanga ndio shida zaidi kuliko hata nyama..

Naelewa pia lehamu si mbaya mwilini ila kuna namna yake ya kuicontrol:Mfano ikiwa nyingi huweza kusababisha hatari ya shinikizo la juu la damu,pia magonjwa ya moyo hivyo basi lazima tujizatiti iiishie tu kwenye level ya Good Cholesterol..

Triglycerides....Hii ikiwa juu kwenye damu huweza sababisha hata Stroke,Diabetes:::: Sasa basi tunawezaje kuicontrol Total Cholestrol ili iwe vizuri katika kila level be it Low density Lipoprotein(LDL) au High density Lipoprotein(HDL)au Good Cholesterol!??

Mazoezi ni muhimu na kupunguza intake of Wanga kama tulivyokubaliana na red meat to be specific( kitimoto )na vyakula vingine vyenye fat ila tule kwa uangalifu....
Uko sahihi ila changamoto kubwa iliyopo sasa ni kuwa wana exaggerate sana siku hizi
Pia cholesterol hadi kufikia kiwango cha juu cha kinachoweza kukuletea madhara haiwezi kutokana na chakula,

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Wana jukwa salaam kwenu.

Imekuwa kawaida kwangu Mimi kula ugali na wali kama Chakula kikuu siku hadi siku. Sasa nimepata wazo la kuviweka kando kwa siku 14 bila kuvigusa

Hivyo naomba mniambie kwa hapa kwetu Tanzania ni Chakula gani mbadala naweza kutumia kwa hizo siku 14 na mwili ukabaki na nguvu zake zile zile
1.Jumapili
2.Jumatatu
3.Jumanne
4.Jumatano
5.Alhamisi
6.Ijumaa
7.Jumamosi
8.Jumapili

Natanguliza shukrani za dhati
1.Viazi vitamu-option ya kukaanga ama kuchemsha..siku 2 hizo

2.viazi ulaya-kukaanga,kuoka na mashed potatoes-siku 3 hizooo

3.tambi
4.Boga la kuchemsha
5.Chapati
6.ndizi mzuzu za kuchemsha na kukaanga -siku 2 hapoo
7.ndizi bukoba-za kukaanga na za kuweka kwenye mchemsho
8.mahindi ya kuchemsha
9.magimbi ya kuchemsha na futari
10.mihogo-ya kuchemsha,ya kukaanga na ya futari ya nazii

kama siku 15 hapo
then js serve kwa kubadili badili mboga of ur choice
 
Back
Top Bottom