Niliagiza chakula, ilivyokuja bili nusura nikimbie niwaache watoto. Umewahi kukumbana na fedheha hii?

Pale Kahawa cafe pembeni kushoto CHIPS KUKU ROBO 25,000, maji 3000 na juice 5000
Almanusura tuache mawigi na simu pona pona yetu ni huu mkopo wa Tigo Niwezeshe.

Hatutasahau
Hahhaa watu hawakawii kujua ni uongo, sijhi kama bado ile cafe ipo. Nimeingia tu jambo la kwanza weusi hakuna watasha tu, nikasema no sweat tupo wawili mm na AmKatarna mwenzio, haya lete chai wanatuletea ka birika kadogo tujisevie, vijani, sukari, kisu, uma na kijiko. Kisha silesi, kiazi cha asili, gimbi na vipisi sijui vya nn. Nikanywa ila njaa ipo pale pale, sijasikia chochote tumboni haya lete bill 25,000 per person watu wawili 50k.
Hela ilikuwepo bahat nzuri ila ni hiyo bei na vilivyoletwa haviendani.
Nikaprintiwa risti nikajuta nikaondoka
 
Hizi kadhia huwakumba Wakurupukaji kama wewe.
 
Yawezekana kweli pesa nyingi..Lakini kwakuspend zaidi ya watu 5 mbona figue ya kawaida.Ukija nextime utenge budget nzuri Mjomba.
 
Sisi tulikuwa na hela ya kuvunja kikundi laki 450, tukaenda hotel kubwa kuona menu tukaagiza vinjwaji tukasepa. Tukaenda sehemu nyingine tukaaagiza tunachotaka na salio likabaki. Tulikua 6.
Safi sana. Hakuna kuona aibu kuomba menu. Kama hutaki kuuliza basi mfuko wako uwe hauyumbi
 
Pole sana jamani.. juzi nilikua nimekaa kwenye kijiwe flan
ikaingia familia ya baba mama na watoto kama watatu.. watoto wapo very excited.. menu ilivyoletwa nikaona baba na mama wametizamana, watoto wakaanza kuchagua chakula,
Maskin baba akawanyanyua haooo wakaondoka🙌
Ile scene imeniongezea morali ya kusaka hela aisee.. kuna experience inafaa tuwape watoto wetu before waje wapewe na walimwengu.

2025 Mungu awasaidie wote Muingie sehemu mlidhani ni za hadhi ya juu zaidi yenu na ziwe kawaida tu kwenu.
 
Do not bite off more than you can chew.Maisha ya kuiga na kujifaragua matokeo yake ndio haya.Ungekufa na tai shingoni baada ya kuamua ulichoamua.Kulalama na kutafuta walioingia cha kike kama wewe haitakusaidia lolote.
Anajua km haitamsaidia chochote ila ameamua tu kushare na sisi ili wengine tuchukue tahadhari ni funzo pia na ni sehemu ya vichekesho kimtindo
 
Safi sana mkuu.
You will be back strong. Pesa inatafutwa ili itumike
 

Ulitumia card gani hiyo ya Bank inayo access malipo kwa njia ya Card (machine) ? Ambayo inatumika kuongoza mshahara wako?
 
Hahaha pole sana ila nimejifunza kitu kimoja Wafanyabiashara tuna rule moja "lipia ulichokitumia/unachokiona" probably tupo close saba na hii Scenerio kinachotuokoa Tunauliza Bei ili Tu Negotiate
 
Ulizia menu usione aibu........ Nauliza hata kama tandale uzuri mimi aibu na macho kubadilika rangi plus kuforce tabasamu sitaki kabisa hizo mbanga
Kwako blood Ibn Unuq
Kijana wangu secretarybird zerominus10

Mshaurini mjomba kama mjomba
Anaagizaje chakula kabla hajajui gharama zake cha ajabu anakimbia asa anakimbia nini?

Chanzo cha tatizo ni nani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…