Niliagiza chakula, ilivyokuja bili nusura nikimbie niwaache watoto. Umewahi kukumbana na fedheha hii?

Hotel zenye bei utazijua kwa muonekano tu

Watu wanazigharamia kwa hiyo bei lazima ziwe juu

Zipo hotel nzuri na za bei kubwa Dar hiyo hela tulikula watu wawili tu Cape Town fish market kama sijakosea jina

Ila kama huna cash ya maana na kadi juu wala usihangaike
 
Shemeji yako akija kwenu anaweza kuwatoa out nyie? Au atajifanya kila kitu hatumii kuanzia bia nk nakujifanya busy na watu wengi wa kutembelea, usirudie tena kujipendekeza.
 
Mikipo ya mtandaoni inaokoa jahazi mara nyingi
 
Ingekuwa bonge la aibu, hao watoto mpaka utu uzima wao wangekuwa wanakumbuka icho kituko cha mjomba wao
 
Aisee ukiwa na tupesa kidogo unaweza pata jeuri kumbe we ni pimbi tu mbele ya wenye nazo. Tatizo hapo lilianzia kwa wewe kuamini una laki moja mfukoni na ukaamini ni kubwa ukadharau hata kufata procedure za siku zote. Pole mkuu.
 
Ulishangaa mbona wakarimu mno kuliko sehem zingine 😂
 
Dah mimejisikia vibaya sana kusoma hii comment....
 
😂😂😂😂 Sema WAJOMBA watakukumbuka ndugu yetu wala usiwazee
 
Dah mimejisikia vibaya sana kusoma hii comment....
Unajua kuna watu wanahisi hizi ni habari za kutunga….lakini wanasahau kwamba haya ni matukio ya kawaida sana kutokea.

tunatofautiana tu uwezo kwa kushare katika lugha ambayo mwingine ataelewa,lakini wengine wanaona vichekesho…wala siyo vibaya,kikubwa ni kujifunza

mimi sijashare hii habari ili nilalamike,hata kidogo…nishapigwa na matukio mengi makubwa kuliko hata haya na maisha yanaenda vizuri kabisa.

somo ni kwamba tutafute pesa…kumbe bado hazitoshi.
 
Mimi juzi hapa tarehe 25 siku ya Christmas mida ya usiku jamaa yangu akaniambia tutoke out viwanja Usiku. Mda huo nilikuwa nishashiba vya kutosha nikasema hata nikienda viwanja sitaki nitumie zaidi ya elfu kumi. Basi tumeenda club moja kiingilio ilikuwa ni 5000,kila mtu akilipia Kiingilio chake,baada ya hapo nikaagiza KVANT ndogo nikaanza kupiga polepole huku nikiangalia watoto waziri wanavyo zungusha viuno.
Ilifika mda vibe likapanda nikasema nalala huko huko nakesha mpka asubuhi ndo niondoke,, ghafla dada zake na jamaa yangu wakaja pale club,wakaanza kucheza pale mezani kwetu,mda huo Niko tungi Sina hili Wala lile jamaa yangu akaniambia dada zake wanataka waondoke warudi nyumbani kwamba wechoka,,mm nikamwambia wao waende jamaa akaanza ku force kuwa hawezi kuenda akaniacha ikabidi nikubali tusepe,kufikia nje pale jamaa kuongea na dereva taksi akaambiwa wote kutubeba watano ni 15,000 huku ni sehemu ya Karibu sana,,basi nikapanda,tumefika mwisho madem wameshuka jamaa ananiambia Hana hela ya kulipa nimkope atanirudishia,duhhh iliniuma Sana Ila nikampatia,,Cha kishangaza mpka Leo hajanipa hio hela dahh iliniuma Sana aisee ile hela maana nilitaka kesho yake niende kwa dem wangu nimpe anunue kuku tu enjoy.
 
Yule dem alikuwa anameza savannah kama maji, aligaiza six pack ikaisha, akaagiza ya pili akanywa tano, moja akabeba,,,, plus kuku akala,,, weka na bia zangu na msosi bili ilisoma around 140k, mm mfukoni nilikuwa na 87k tu ,,,, ! ! Unaumbuka mchana kweupe, sim banking ilinisaidia !! Na sikumla, nilikuja kumla a year later, nilihama ule mkoa kikazi !
 
Mimi juzi hapa tarehe 25 siku ya Christmas mida ya usiku jamaa yangu akaniambia tutoke out viwanja Usiku. Mda huo nilikuwa nishashiba vya kutosha nikasema hata nikienda viwanja sitaki nitumie zaidi ya elfu kumi. Basi tumeenda club moja kiingilio ilikuwa ni 5000,kila mtu akalipa Kiingilio chake,baada ya hapo nikaagiza KVANT ndogo nikaanza kupiga polepole huku nikiangalia watoto wazuri wanavyo zungusha viuno.
Ilifika mda vibe likapanda nikasema nalala huko huko nakesha mpka asubuhi ndo niondoke,, ghafla dada zake na jamaa yangu wakaja pale club,wakaanza kucheza pale mezani kwetu,mda huo Niko tungi Sina hili Wala lile jamaa yangu akaniambia dada zake wanataka waondoke warudi nyumbani kwamba wamechoka,,mm nikamwambia wao waende jamaa akaanza ku force kuwa hawezi kuenda akaniacha ikabidi nikubali tusepe,kufika nje pale jamaa akaongea na dereva taksi akaambiwa wote kutubeba watano ni 15,000 huku ni sehemu ya Karibu sana,,basi nikapanda,tumefika mwisho madem wameshuka jamaa ananiambia Hana hela ya kulipa nimkope atanirudishia,duhhh iliniuma Sana Ila nikampatia,,Cha kishangaza mpka Leo hajanipa hio hela dahh iliniuma Sana aisee ile hela maana nilitaka kesho yake niende kwa dem wangu nimpe anunue kuku tu enjoy.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…