😄😄Ndo maan hata nikitolewa kabla sijaagiza nauliza bei hat km sinunui mm nijue ninaubavu nikikimbiwa kulipa nitaweza 😄Una bahati Sana ungepewa adhabu ya kuosha vyombo mbele za wajomba zako 😂
Nilienda kutembea Dar es Salaam kwa dada yangu wakati wa sherehe hizi za christimass.
Basi tarehe 25/12 kama kawaida tulikwenda ibadani na kurudi nyumbani,kilichofuata ni maongezi tu ya kifamilia huku tukichoma nyama jioni na kunywa pombe pamoja na shemeji na marafiki zake.
Tarehe 26/12 nikataka na mimi onyesha msuli wangu kwa shemeji ili asinichukulie poa…Basi bwana nikawaambia leo niachieni hawa vijana nitoke nao out nao waone raha ya kuwa na mjomba,wako watoto wanne na dada wa kazi. jumla watano.
Basi wao wenyewe wakataja mahala wanataka kwenda…ni beach fulani hivi wamejenga vizuri sana na kuna michezo mingi sana ya watoto,vyakula na vinywaji.
Basi tukaondoka tukafika…kiukweli mimi nilidhani ni mahala naweza afford kulipia kila kitu na nilitenga 100,000/= nzima kwa ajili ya kutumbua.
Sasa kufika nikaambia kwanza vijana wapate chakula.Wakaagiza kila mmoja chipsi kavu pamoja na kuku nusu.Pia waliagiza juice freshi na kuna kamoja kiherehere kakaagiza pizza moja ya kushare wote…yule dada wa kazi kwa aibu za kikubwa aliagiza chipsi na mshkaki mmoja tu na juice.
Mahesabu yangu yalikua pale itakata kama 50,000/= hivi pamoja na michezo yao ile…wakamaliza kula,mimi mwenyewe nikaagiza bia zangu 5 pamoja na nyama choma ya mbuzi.
…..sasa game ikaanza karibia wanamaliza kula yule dada ndio akaniletea ile “menu”,lahaulaaaa
chipsi kavu-inasoma 6000/= mara 5
kuku nusu-inasoma 21,000/= mara 4
fresh juice-inasoma glass moja 6000/= mara 5
pizza moja-inasoma 35,000/=
mshkaki mmoja(niligundua wameandika fillet)-3500/=
nyama choma mbuzi—inasoma 25,000/= per portion
bia moja local ni 4000/= mara 5
kwa haraka haraka ilisoma kama 227,500/= kinyume kabisa na matarajio yangu.
Kwanza nilihisi baridi sana imenichapa sababu vitu vyote vishaagizwa na vingine vishaanza kutumika,watoto wanaenjoy sana na huwezi waambia kitu wakakuelewa.
Hapo wanasubiri washibe nikawalipe kila mmoja 5000/= ya kwenda kwenye michezo yao ya watoto…
Mimi bhana nikajitetea nataka kulipa kwa kadi…walete mashine,lengo langu hapa kubahatisha sababu ndio zilikua tarehe bosi anaingiza chochote kwenye account.
Ile kugusa tu pyaaaaa….nakuta sms inaingia umefanikiwa kulipia 227,500/= kwenda Utulivu beach resort,ikaja na sms ya muamala wa makato ya muamala kama 4000/= hivi.
Kwa kweli mood yote ilikata…kwa mshahara wangu hiko kiwango kilikua ni zaidi ya nusu yake mimi nimetumia kulipia watoto kula sehemu ambayo siyo level zangu….ila nikakaza kiume,ile kulipia kwa kadi nikaonekana doni sana pale.
basi na ile laki mkononi nayo nikaibunya mjini…..sahivi niko zangu kwenye katarama narudi zangu mkoani na somo.
Umewahi kutana na dhahama kama hii?!😂
hela ndogo sana hio kama upo above 30+.
kwahali hiyo hata mbususu ulipewa?Binti mmoja mkali enzi hizo dansa Fm marehemu sasa.
E bana katika kupiga sound,
Poa njoo mazoezini.
Nikazama huko sijui Chez ntemba Kino ndani mkwajuni studio.
Ile kufika demu kaja bia zao Heineken, sijakaa vizuri madansa wenzie nao hao km sita hivi.
Halafu hawaulizi ni salamu tu "aa shem pedeshee",
hapo supu , bia zinaenda Tu
Then hao waimbaji hawa wacongo wote hao km 12.
Walifakamia nyama bia, supu km hawana akili nzuri. alafu hao
Wakayeyuka😆.
Nilienda na kilo nikijua bajeti yetu wawili demu hamalizi.
Kuletewa bili "mama nene"🙆♂️
K
ilo 3+,
Nikamuita mshkaji aje arekebishe nae ana kilo tu si zaidi.
Duh ikabidi tuache simu, tukazirudia baada ya siku 2
Ndio ikatimia hela ya bill yote.
wala usiumie, siyo wewe, ni ukosefu wa pesa.Mimi juzi hapa tarehe 25 siku ya Christmas mida ya usiku jamaa yangu akaniambia tutoke out viwanja Usiku. Mda huo nilikuwa nishashiba vya kutosha nikasema hata nikienda viwanja sitaki nitumie zaidi ya elfu kumi. Basi tumeenda club moja kiingilio ilikuwa ni 5000,kila mtu akilipia Kiingilio chake,baada ya hapo nikaagiza KVANT ndogo nikaanza kupiga polepole huku nikiangalia watoto waziri wanavyo zungusha viuno.
Ilifika mda vibe likapanda nikasema nalala huko huko nakesha mpka asubuhi ndo niondoke,, ghafla dada zake na jamaa yangu wakaja pale club,wakaanza kucheza pale mezani kwetu,mda huo Niko tungi Sina hili Wala lile jamaa yangu akaniambia dada zake wanataka waondoke warudi nyumbani kwamba wechoka,,mm nikamwambia wao waende jamaa akaanza ku force kuwa hawezi kuenda akaniacha ikabidi nikubali tusepe,kufikia nje pale jamaa kuongea na dereva taksi akaambiwa wote kutubeba watano ni 15,000 huku ni sehemu ya Karibu sana,,basi nikapanda,tumefika mwisho madem wameshuka jamaa ananiambia Hana hela ya kulipa nimkope atanirudishia,duhhh iliniuma Sana Ila nikampatia,,Cha kishangaza mpka Leo hajanipa hio hela dahh iliniuma Sana aisee ile hela maana nilitaka kesho yake niende kwa dem wangu nimpe anunue kuku tu enjoy.
Walikuona umetoka pori sanakuna siku moja niliingia saluni mwanza hakika sikumbuki mtaa….tulikua huku kwenye harusi ya jamaa yangu,huwa sipendi kufanya mambo kwa mkumbo…huwa natamani kufanya mwenyewe tena kwa kujaribu vitu vipya….
ila nakumbuka niliingia kwanza saluni eti ina sehemu ya reception…mimi hapo hata akili hainichezi machale…saluni gani ina reception bhana😀
mara yule muhudumu kaniandikisha jina na vitu nimeingia navyo…kavaa khanga tu,mi hapo mawazo hata hayapo hapo…anachekacheka kama vile kanipenda na mii nikawa naongeza confidence.
akanipeleka huko kwa kunyoa kwanza….tulitembea kama vyumba vitano mbele,yaani wale jamaa niligundua ile berbershop wamekodi floor nzima ya ghorofa….kila kitu kinafanyiwa chumba chake…
mimi kwenye kunyoa huko kwanza nashangaa wananihudumia watu watatu tofauti
alianza dada akanivalisha ile kitambaa na kunichana nywele….akaja jamaa alaninyoa halafu akamaliza jamaa mwingine wa kuchonga pamoja na ndevu…..akaja dada yule wa reception mwingine akanihamisha chumba….huko nilikuta wadada tu wamekaa kwenye makochi na kila mtu kavaa nusu utupu….akamkabidhi mmoja aanze sasa niosha…alisema unafanya scrub au steamer…nikasema steamer…yaani hapo anauliza anakupapasa shingoni,basi akaanza puliza ule mvuke…nilikaa pale karibia dakika 45 ananihudumia mimi tu…sasa hapa ndio machale yakaanza kunicheza,hawa mbona wakarimu hivi hawaa
sasa baada ya hapo wakasema kucha nazo zifanyiwe marekebisho pamoja na massage ya kichwa na shingo….mimi haya yote najua ni bonus…
tukamaliza zoezi ndio wakampigia yule dada wa reception…akaja.
aisee bili ananisomea inakuja 72,000/=🥹🥹🥹🥹….aibu ndio sipendi,kwa confidence ile ile nikazama mfukoni nikatoa 75,000/=….sema walinigundua chuplichupli nadhani nilivyoshindwa kujizuia kudai 3000/= ndio mmoja akauliza kwani kaka wewe wa wapi…..
ile natoka ndio nakumbuka kusoma bango….ni hasfi sijui ile mule wanaenda waliopata zao mawe ya madini…
lakini ni kujikaza tu *****….kupendeza nilipendeza sana harusini.
😄😄Ndo maan hata nikitolewa kabla sijaagiza nauliza bei hat km sinunui mm nijue ninaubavu nikikimbiwa kulipa nitaweza 😄
Kuosha vyombo sio poa
Kabisa kuuliza mapema kunakuepusha na aibu ndogo ndogo😄😄Ndo maan hata nikitolewa kabla sijaagiza nauliza bei hat km sinunui mm nijue ninaubavu nikikimbiwa kulipa nitaweza 😄
Kuosha vyombo sio poa
Hahahaha asee wamekuonea, kidogo ninachojua huwa Kuna resident rates hata kwa hotel kubwa kubwa..Hahahaaa nimecheka, hivi shoppers plazza pale Dodoma ndo pakuniuzia breakfast 25,000 × 2 = 50,000 ~ wakati mm nilitegemea brekafast iwe 10,000]
wala usiumie, siyo wewe, ni ukosefu wa pesa.
ukishaonba nn kinafata::=walaji ni watoto na ndo waagizani ebo!! unataka uwashikishe menu afu iweje au kshike ww iweje uwakataze kula vya bei(nn maana ya matembezi hapo?)Kitu cha kwanza ukifika mahali , omba menu au kama hamna uliza bei kwa wahudumu !
Yaan mimi bora mnione bahiri ila ni muhimu sana !!
Unaweza umbuka vibaya sana !
Matembezi ni kitu kizuri kwa watoto hata mimi hupendelea kumpeleka Dogo na mama mahali wakapate chochote kitu inaongeza upendo !ukishaonba nn kinafata::=walaji ni watoto na ndo waagizani ebo!! unataka uwashikishe menu afu iweje au kshike ww iweje uwakataze kula vya bei(nn maana ya matembezi hapo?)
FATA KILICHOKUPELEKA [emoji23][emoji23]
Huyo cha mtoto Dar free market kuna mtu alikutana na za uso
Kabla sijampeleka Mtu sehemu naenda mwenyewe hiyo sehemu kuangalia na kuuliza bei, sitakagi hekeheka Mimi.... tangu niuziwe Ugali 30000 wakati Mfukoni nina 5000 nimejifunza
nmecheka sana sas ww ndugu utaagizaje chakula bila kusoma kwanz menu!!?Nilienda kutembea Dar es Salaam kwa dada yangu wakati wa sherehe hizi za christimass.
Basi tarehe 25/12 kama kawaida tulikwenda ibadani na kurudi nyumbani,kilichofuata ni maongezi tu ya kifamilia huku tukichoma nyama jioni na kunywa pombe pamoja na shemeji na marafiki zake.
Tarehe 26/12 nikataka na mimi onyesha msuli wangu kwa shemeji ili asinichukulie poa…Basi bwana nikawaambia leo niachieni hawa vijana nitoke nao out nao waone raha ya kuwa na mjomba,wako watoto wanne na dada wa kazi. jumla watano.
Basi wao wenyewe wakataja mahala wanataka kwenda…ni beach fulani hivi wamejenga vizuri sana na kuna michezo mingi sana ya watoto,vyakula na vinywaji.
Basi tukaondoka tukafika…kiukweli mimi nilidhani ni mahala naweza afford kulipia kila kitu na nilitenga 100,000/= nzima kwa ajili ya kutumbua.
Sasa kufika nikaambia kwanza vijana wapate chakula.Wakaagiza kila mmoja chipsi kavu pamoja na kuku nusu.Pia waliagiza juice freshi na kuna kamoja kiherehere kakaagiza pizza moja ya kushare wote…yule dada wa kazi kwa aibu za kikubwa aliagiza chipsi na mshkaki mmoja tu na juice.
Mahesabu yangu yalikua pale itakata kama 50,000/= hivi pamoja na michezo yao ile…wakamaliza kula,mimi mwenyewe nikaagiza bia zangu 5 pamoja na nyama choma ya mbuzi.
…..sasa game ikaanza karibia wanamaliza kula yule dada ndio akaniletea ile “menu”,lahaulaaaa
chipsi kavu-inasoma 6000/= mara 5
kuku nusu-inasoma 21,000/= mara 4
fresh juice-inasoma glass moja 6000/= mara 5
pizza moja-inasoma 35,000/=
mshkaki mmoja(niligundua wameandika fillet)-3500/=
nyama choma mbuzi—inasoma 25,000/= per portion
bia moja local ni 4000/= mara 5
kwa haraka haraka ilisoma kama 227,500/= kinyume kabisa na matarajio yangu.
Kwanza nilihisi baridi sana imenichapa sababu vitu vyote vishaagizwa na vingine vishaanza kutumika,watoto wanaenjoy sana na huwezi waambia kitu wakakuelewa.
Hapo wanasubiri washibe nikawalipe kila mmoja 5000/= ya kwenda kwenye michezo yao ya watoto…
Mimi bhana nikajitetea nataka kulipa kwa kadi…walete mashine,lengo langu hapa kubahatisha sababu ndio zilikua tarehe bosi anaingiza chochote kwenye account.
Ile kugusa tu pyaaaaa….nakuta sms inaingia umefanikiwa kulipia 227,500/= kwenda Utulivu beach resort,ikaja na sms ya muamala wa makato ya muamala kama 4000/= hivi.
Kwa kweli mood yote ilikata…kwa mshahara wangu hiko kiwango kilikua ni zaidi ya nusu yake mimi nimetumia kulipia watoto kula sehemu ambayo siyo level zangu….ila nikakaza kiume,ile kulipia kwa kadi nikaonekana doni sana pale.
basi na ile laki mkononi nayo nikaibunya mjini…..sahivi niko zangu kwenye katarama narudi zangu mkoani na somo.
Umewahi kutana na dhahama kama hii?!😂
Kuna sehemu nilienda nyoa na rafiki yangu na kupaki mikweche miwili jamaa yangu kapigwa 20000 na scrubing ila mimi sikunyoa, siku nyengine nimeenda wameona mkweche mmoja umekuja, ile nanyoa namaliza dada mmoja na mshepu wake kaka hamia kiti kile pale, nikwambia wife atamind nikiosha, nikakwepa mshale wa 20000 😂😂Nimecheka sana, eti kamoja kiherehere, mie nakumbuka nikiwa kikazi Dom mida ya saa 4 usiku nikaingia saloon nikwangue nywele, ile kumaliza bei kaniambia buku 5 na kunyoa kwenyewe ovyo, iliniuma hiyo buku 5