Niliagiza chakula, ilivyokuja bili nusura nikimbie niwaache watoto. Umewahi kukumbana na fedheha hii?

Niliagiza chakula, ilivyokuja bili nusura nikimbie niwaache watoto. Umewahi kukumbana na fedheha hii?

Mafundi gareji wanafikiri kumiliki gari ni utajiri. Nilienda gereji nikamueleza tatizo akasema andaa kama 60,000. Nikasema fanya kazi. Wakafungua kwenye miguu baadaye anasema wamekuta matatizo mengine. Jumla ikaja 380,000. Ilikuwa balaa. Kuacha gari gereji siwezi maana wizi mwingi. Mpangaji akaniokoa. kodi ilikuwa inaisha siku hiyo, kumpigia akatuma muamala chap😃. Nikalipa na kusepa. Sijarudi gereji hiyo tena.
Aaha juzi kati kimenikutaa kitu nimebeba kalaki kangu nikafanye service aisee Si fundi akasema afanye ni Gear box nikakubali kamaliza kila kitu bill inasoma 230k mafundi usiwazikilize hata siku moja fanya marekebisho ya kitu ulichoenda kufanya sepa.
 
Mkuu Nimecheka kwamba kuna mmoja kiherehere aliagiza pizza. Mimi kipindi nipo chuo weekend na mama watoto tumeingia supermarket tunafanya shopping sasa kuna shelf la wine tukafika sasa ile nachukua chupa ya wine lahaula upande wa shelf wote upo chini wine kadhaa zimepasuka walinifwata spidi kama mama anavyosikia kishindo alafu mtoto wake Akalia huko nje. Wakawa wanafoka kweli kwa hasira nikasema nipeni bill nitalipia. Nakumbuka mmoja akaniambia utaweza wife akamjibu Unatuchukulia kama wewe mfanyakazi supermaket. Wakatupa bill inasoma 645000/-. Uzuri pembeni kulikuwa na ATM ya NBC wife akaenda kutoa maana mfukon nilikuwa na 180000/- Tukawalipa Tukawafyonza Tukaondoka Zetu Ila ile pesa inaniuma mpaka Leo nadhan lile shelf walikuwa wamelitegesha sikuapply nguvu kubwa kuchukua chupa ya wine kiasi cha kuuangusha ule upande wa shelf
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
wife umepata wa kufanana naye
 
Bujumbura city center Havana lounge....nimekuja booke hazishiki bia flan Kama gines light...nkaagiza short za godons 3 wewe naona watu wannishangaaa nikasema labda wanamuona nakula ngumu sana...nkaletewa bili short moja faranga 7000...khaaa nikasema godons hii hii au henes sikuwa mnyonge nkalipa..Ila toka hapo kila nikitaka kuagiza foreign beer au gin lazima niulize Bei.... Wakati huo haba bongo short za godons NI 2000 au 1500
 
Qappp
Pole sana lakini umefaidi kupata somo hapo. Kati ya mambo nachukia ni kutumia fedha nyingi bila kupata ile kitu wanaita value for money.

Hadi saa naamini si sawa kula mlo unaozidi TZS 7000/- Juzi kati hapo nimekunywa chai na mayai mawili ya kukaanga wananiambia TZS 6,000/- nusura fujo itokee.
Nadhani wahudumu saazingine hutengeneza bei za maghumashi kwa kutumia udhaifu wa mteja kufakamia bidhaa bila kuuliza bei.
 
Ushauri wa busara sana huo.

Mi nshajifunza siku nyingi sana hayo mambo, tena kwa kitu kidogo tu soda.

Nimefika sehemu,... 'tupe soda'.. tukanywa mbili mbili kwa maongezi zaidi tukiwa watatu.

Kila kona bei ya soda inajulikana ni 500/-, nikatoa noti ya Sh. 5,000/-nikitumaini kurejeshewa 2,000/-.

Mhudumu naye akawa anasubiri buku, hadi nilivyoidai kwa sauti, ndonikaelezwa niongeze buku, yaani soda 350ml elfu, kwa lipi hasa!

Tangu siku hiyo ni mwiko kwangu kutumia huduma za watu bila kuuliza bei kwanza.
Nshawah zungumza na mtu as per your comment anasema lack of exposure nikamwambia sawa.....

Lakini soda hii ya 600 ni elfu nne sijui, it's ok hata kama ni advanced basi waone namna nzuri ya kueka bei

Au msosi.... Nikamwambia siwezi toa 30k kununua kuku ambaye siku Kuna kuku point Hawa wanachomwa vizuri kwa bei simple unaridhika!
 
kuna siku moja niliingia saluni mwanza hakika sikumbuki mtaa….tulikua huku kwenye harusi ya jamaa yangu,huwa sipendi kufanya mambo kwa mkumbo…huwa natamani kufanya mwenyewe tena kwa kujaribu vitu vipya….

ila nakumbuka niliingia kwanza saluni eti ina sehemu ya reception…mimi hapo hata akili hainichezi machale…saluni gani ina reception bhana😀

mara yule muhudumu kaniandikisha jina na vitu nimeingia navyo…kavaa khanga tu,mi hapo mawazo hata hayapo hapo…anachekacheka kama vile kanipenda na mii nikawa naongeza confidence.

akanipeleka huko kwa kunyoa kwanza….tulitembea kama vyumba vitano mbele,yaani wale jamaa niligundua ile berbershop wamekodi floor nzima ya ghorofa….kila kitu kinafanyiwa chumba chake…

mimi kwenye kunyoa huko kwanza nashangaa wananihudumia watu watatu tofauti

alianza dada akanivalisha ile kitambaa na kunichana nywele….akaja jamaa alaninyoa halafu akamaliza jamaa mwingine wa kuchonga pamoja na ndevu…..akaja dada yule wa reception mwingine akanihamisha chumba….huko nilikuta wadada tu wamekaa kwenye makochi na kila mtu kavaa nusu utupu….akamkabidhi mmoja aanze sasa niosha…alisema unafanya scrub au steamer…nikasema steamer…yaani hapo anauliza anakupapasa shingoni,basi akaanza puliza ule mvuke…nilikaa pale karibia dakika 45 ananihudumia mimi tu…sasa hapa ndio machale yakaanza kunicheza,hawa mbona wakarimu hivi hawaa

sasa baada ya hapo wakasema kucha nazo zifanyiwe marekebisho pamoja na massage ya kichwa na shingo….mimi haya yote najua ni bonus…

tukamaliza zoezi ndio wakampigia yule dada wa reception…akaja.

aisee bili ananisomea inakuja 72,000/=🥹🥹🥹🥹….aibu ndio sipendi,kwa confidence ile ile nikazama mfukoni nikatoa 75,000/=….sema walinigundua chuplichupli nadhani nilivyoshindwa kujizuia kudai 3000/= ndio mmoja akauliza kwani kaka wewe wa wapi…..

ile natoka ndio nakumbuka kusoma bango….ni hasfi sijui ile mule wanaenda waliopata zao mawe ya madini…

lakini ni kujikaza tu *****….kupendeza nilipendeza sana harusini.
 
Kama kipato chako ni cha kuunga unga au cha mawazo ni vyema unapoingia hotel kubwa kuuliza bei za vitu kwanza kabla ya kuagiza.
 
Back
Top Bottom