🤣🤣🤣🤣Hapo kwenye kumaliza chanjo umenivunja mbavu zangu....awekewe kijiti kwa lazima khaaaaa😹😹😹
Dada wewe si ndo umesema niache ugomvi jamani 🤣
Ila mwafula hapana.!! Kwani kaambiwa dunia aijaze peke yake??
Atamaliza chanjo wengine tukizaa watoto wapate polio bure 🤣
Ila wasukuma hawaishi vituko wallah😂
Ukiongezea na nauli ya Katarama kurudi usukumani, mshahara ushakata wote...
Afungwe kizazi 😹😹🤣🤣🤣🤣Hapo kwenye kumaliza chanjo umenivunja mbavu zangu....awekewe kijiti kwa lazima khaaaaa
Aaha juzi kati kimenikutaa kitu nimebeba kalaki kangu nikafanye service aisee Si fundi akasema afanye ni Gear box nikakubali kamaliza kila kitu bill inasoma 230k mafundi usiwazikilize hata siku moja fanya marekebisho ya kitu ulichoenda kufanya sepa.Mafundi gareji wanafikiri kumiliki gari ni utajiri. Nilienda gereji nikamueleza tatizo akasema andaa kama 60,000. Nikasema fanya kazi. Wakafungua kwenye miguu baadaye anasema wamekuta matatizo mengine. Jumla ikaja 380,000. Ilikuwa balaa. Kuacha gari gereji siwezi maana wizi mwingi. Mpangaji akaniokoa. kodi ilikuwa inaisha siku hiyo, kumpigia akatuma muamala chap😃. Nikalipa na kusepa. Sijarudi gereji hiyo tena.
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂Mkuu Nimecheka kwamba kuna mmoja kiherehere aliagiza pizza. Mimi kipindi nipo chuo weekend na mama watoto tumeingia supermarket tunafanya shopping sasa kuna shelf la wine tukafika sasa ile nachukua chupa ya wine lahaula upande wa shelf wote upo chini wine kadhaa zimepasuka walinifwata spidi kama mama anavyosikia kishindo alafu mtoto wake Akalia huko nje. Wakawa wanafoka kweli kwa hasira nikasema nipeni bill nitalipia. Nakumbuka mmoja akaniambia utaweza wife akamjibu Unatuchukulia kama wewe mfanyakazi supermaket. Wakatupa bill inasoma 645000/-. Uzuri pembeni kulikuwa na ATM ya NBC wife akaenda kutoa maana mfukon nilikuwa na 180000/- Tukawalipa Tukawafyonza Tukaondoka Zetu Ila ile pesa inaniuma mpaka Leo nadhan lile shelf walikuwa wamelitegesha sikuapply nguvu kubwa kuchukua chupa ya wine kiasi cha kuuangusha ule upande wa shelf
Shukrani aseeh big up bwasheeSina cha kuongezea Cha msingi mjomba amakinike na ulichoandika, basi
Nadhani wahudumu saazingine hutengeneza bei za maghumashi kwa kutumia udhaifu wa mteja kufakamia bidhaa bila kuuliza bei.Pole sana lakini umefaidi kupata somo hapo. Kati ya mambo nachukia ni kutumia fedha nyingi bila kupata ile kitu wanaita value for money.
Hadi saa naamini si sawa kula mlo unaozidi TZS 7000/- Juzi kati hapo nimekunywa chai na mayai mawili ya kukaanga wananiambia TZS 6,000/- nusura fujo itokee.
We umeenda sehemu iko ufukweni na laki 1 huku ukiwa na nyomi la vijana😁!? Bahati yako tu tajiri alifanya miujiza.
Siku nyingine usirudie kushobokea viwanja vya ufukweni kama huna walau million 1 kwenye account
Nshawah zungumza na mtu as per your comment anasema lack of exposure nikamwambia sawa.....Ushauri wa busara sana huo.
Mi nshajifunza siku nyingi sana hayo mambo, tena kwa kitu kidogo tu soda.
Nimefika sehemu,... 'tupe soda'.. tukanywa mbili mbili kwa maongezi zaidi tukiwa watatu.
Kila kona bei ya soda inajulikana ni 500/-, nikatoa noti ya Sh. 5,000/-nikitumaini kurejeshewa 2,000/-.
Mhudumu naye akawa anasubiri buku, hadi nilivyoidai kwa sauti, ndonikaelezwa niongeze buku, yaani soda 350ml elfu, kwa lipi hasa!
Tangu siku hiyo ni mwiko kwangu kutumia huduma za watu bila kuuliza bei kwanza.