Niliagiza wine ya kupima lita tano toka Dodoma, Iliyoletwa nahisi ni gongo au konyagi iliyozimuliwa maana bongo feki kila kona

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
11,793
Reaction score
22,552
Bongo kila kitu ni kuchakachua tu!

Iwe maji ya kunywa feki kibao, iwe sigara feki, iwe makalio ya wanawake nayo feki mtupu, bikira nazo feki, unga feki, hata kwenye kandanda nako siku hizi michongo mtupu n.k

Sasa sijui tukimbilie wapi, nimeagiza wine nikaambiwa ni alter wine!
Aisee nimejaribu kuitia mdomoni radha yake ni tofauti sana na nilivyozoea!
kwanza inachoma balaa kuanzia kooni hadi kwenye utumbo!

Yaani ukiibunda mdomoni inaunguza utumbo inavyotembea hadi tumboni!

Nahisi hii wine nimepigwa wallah sidhani kama ni ALTER WINE kweli!

Nimempa wife aonje kagida nusu glass tu hoi kalewachakali!

Bongo nimewavulia kofia kwa feki alooh!

Nilijua feki ni maji tu kumbe hadi kwenye pombe!
Nyau sana wote wanaotufanyia hivi!
Na sitaimwaga!
 
Pole sana
Tanzania ukihitaji chochote nenda kwenye source mfano kiwandani ila hizi habari za wakala lazima wakupige.

Miaka inavyozidi kwenda ndivyo tunavyozidi kudharaulika maana wizi umekuwa ni kazi na ni kitu cha kujisifia kwa mtanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kazi kweli kweli
 
Kuna wine safi sana, nyingine miyeyusho.

Kuna Four cousins hii ya SA
Image pia ni nzuri ina taste safi.

Nyingine sizielewi sana.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nimecheka balaaa. Jitajidi ku Trace wapi alipo itoa alokuagizia
 
wine ni kali brooπŸ˜‚πŸ˜‚, kama ulitaka tam tam ungesema wangekupa ambayo haija fanyiwa aging
 
dane wine na dompo siku hizi wana ujazo wa lita 5, watumie hao wana jina zuri sokoni tayari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…