Niliamka Asubuhi nikakutana na Taaarifa kwamba nimeteuliwa kuwa Jaji, sikuwahi kuwaza ni rahisi namna hii!

Niliamka Asubuhi nikakutana na Taaarifa kwamba nimeteuliwa kuwa Jaji, sikuwahi kuwaza ni rahisi namna hii!

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
Juzi nilikutana na mwanafunzi wangu ambaye kwa Sasa ni Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Tulijadili mambo tofauti Ila Moja ya kilichomfurahisha ni namna alivyoaminishwa ni vigumu kwake kuwa Jaji lakini Katika ugumu huo akajikuta jina lake lipo KWENYE vyombo vya habari ameteuliwa Katika nafasi hiyo.

Kwa eneo alilokuwa anafanyia kazi na kwa uzoefu wake kisheria kazi ya ujaji aliona ni ngumu na hata alipokabidhiwa anaamini ni moja ya kazi yenye hadhi tofauti na iliyofungamanishwa na ukosefu wa Uhuru wakufanya mambo mengi Ila inayohitaji uzoefu Katika kutenda haki.

Kwa maoni yake, mfumo wa upatikanaji Majaji nchini unaambatana na mambo mengi magumu akiyataja.
1. Ni mfumo usiojali siniority, kwamba leo wapo mahakimu wamesota na Wana uzoefu na sifa elimu lakini inapokuja uteuzi wa Jaji wanaweza wakaachwa wakachukuliwa watu nje kabisa ya mfumo wa Mahakama na ambao baadhi yao awajawahi kuamua kesi hata Moja. Hata ungekuwa competent namna gani Uhuru wako wakuwaongoza Hawa mahakimu na watendaji wa Mahakama unapokwa kutokana na wao kukuzidi experience, unafanya maamuzi lakini ushauri mpana unaupata kwa walio chini Yako.

2. Jaji anapoteuliwa nje ya mfumo wa Mahakama na akiwa hana jina huko alikotoka anaachwa bila kupewa ushirikiano, haya tunayaona yanatokea mahakamani ambapo majaji wanatoa maamuzi then KWENYE rufaa maamuzi yao yanachanwachanwa kama vile walio Mahakama ya rufaa walisoma vyuo tofauti. Hii sometimes inatokea Kwa kukosa ushirikiano au kujiona Mimi jaji najua Kila kitu.

3. Upo ushirikina KWENYE Utumishi wa umma, kuteuliwa kinyume kabisa cha utaratibu au kuteuliwa wakaachwa wenye uzoefu kumepelekea wenye imani za kishirikina kuzijaribu NAFSI za majaji na wapo majaji wamepofuka.

4. Mahakama Tanzania inakosa Uhuru Kwa sababu utaratibu wa kumpata Jaji unaweza fanywa gizani na wakumwondoa pia ukafanywa gizani. Siku mahakama ikiweka utaratibu nuruni tutapona.

Pamoja na surprise ya ujaji lakini mwanafunzi huyu anaeleza wazi kwamba hakuna mahakama inayoweza kushindana na serikali na ndio maana hata mAh ikitoa baadhi ya hukumu serikali upinga kuzitekeleza.

Mwisho aliomba nimweke kwenye maombi ikiwezekana astaafu bila kuamua kesi yoyote kuliko Kustaafu akiwa amehukumu kinyume kabisa na dhamira Yake
 
Mwambie ama mshauri ajiuzuru, ni rahisi tu.

Asituchafulie heshima na hadhi ya taaluma yetu.
Heshima gani kwenye taaluma hii iliyoingiliwa kisiasa?siku ambayo wataomba kuwa majaji na kufanyiwa USAILI ndio heshima utakuwepo,you EARN A RESPECT sio kulazimisha,watoto wako wakuheshimu sio kuwalazimisha wakuheshimu
 
Taaluma gani uliyonayo wakati hata kuandika huwezi , achilia kutojua kingereza.
Kwani haki inatolewa kwa kingereza? Mbona una akili fupi hivi?

Yani kukwambia wewe una kosa ama wewe huna kosa nenda nyumbani huwezi kuelewa hadi uambiwe kwa kingereza?
 
Sifa ya kuwa Jaji kikatiba ni uwe wakili kwa miaka 10 hii wengi wanayo plus uwe na miaka 45+ wapo pia. Ugumu labda kwenye kufikiriwa kuingizwa kwenye mchakato hadi kupata teuzi. Vijana wanaita 'connection'
 
Maana halisi ya kuteuliwa kuwa jaji Tanzania😁😁😁
AIgmal.jpg
 
Mchakato wa kumpata Jaji huchukua zaidi ya miezi 6!
huo muda hautoshi lakini sio Tanzania kwenye kile kipengere "Ikimpendeza Raisi" kwamba anaweza kuteuliwa hata Malaya au mskaji wake tu, vyeo vya kuteuawana ni aina flani ya rushwa na matumizi mabaya ya ofisi
 
🎵 Sasa bwana hakimu unaleta usiniority sijui masters kwenye uteuzi wa u judge

🎵Hukumu hajawai kuandika hata karatasi kumi ukafanya hata reference ya maandiko ambayo ni persuasive ili hata wasomi wanaosoma vyuo mbalimbali wakipata hukumu yako wanapata rejea unataka uwe judge kweli?

🎵 Yaana kesi zako za rejea ndio zile zile kila siku kwenye identificationa parade unarudia mwango manaa, kwenye trial within trial upo na tuwamoi v uganda na visual identity ni waziri amani mpaka tumeshakukari hutaki kufanya tafiti ya mambo mapya unataka kuwa judge kweli

🎵 Kesi zako ulizopewa kufanya extended jurisdiction zikikatiwa rufaa zinashindwa kila wakati unataka upewe u judge kweli?

🎵 Vile vitendo vinavyopingwa na pccb na wewe umo na dau lako linajulikana kabisa na namna ya kuingilika na maafisa masoko wako kwenye hilo wanafahamika unataka kuwa judge kweli?

🎵 Wewe unajifanya bold hata kwenye public interest eti unaringia theory ya independent of judiciary ?

🎵 Tabia yako nje ya doc inashindwa kukutofautisha wewe na mtu wa kawaida, tuko wote bar, tunagombania madem wote eti uteuliwe kuwa judge ? Hujui kuwa unavyoishi kuna watu wasioonekana wanafanya tathmini ya maisha yako na kukufnyia vetting kimyakimya?

🎵 If you want to fly with the Eagles stop swimming with the ducks!!
 
Awamu ya tano na hii ya sita zimeunajisi sana mhimili huu Mahakama. Yanayotendeka kwenye kesi ya kutunga ya Mbowe ni mfano hai wa jinsi tasnia ya sheria na mhimili wa Mahakama ulivyonajisiwa.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Ni huyu huyu Tiganga? Ndo unataka kusema yuko mbioni kujitoa kabla hajatoa hukumu? Maana maamzi yake yanaonekana kuchagizwa na Kidando!
 
Dada Bite, Beatrice Kamugisha , nimesoma, nimeguswa sana kwasababu kuna kitu niliwahi kukisema kuhusu majaji wetu na uwezo wao wa kutenda haki, huyu jaji mwanafunzi wako amekisema.

P.
 
Back
Top Bottom