Du gidume nimecheka sana lkn ngoja tusubirie Plate Number tumalize ubishiNa nyimbo za kijerumani wapi na wapi mzee..tuacheni uongo..em tuma picha ikiwa na plate number..maana nimezoom kwenye screen naona miziki ya kidautch...
Aniwahishe hospital kvp wakat me nlkua mzima tyuuuh. AaaaahPengine alikuwa anakuwahisha hospitali halafu katikati ya safari ukapata nafuu[emoji4]
Huyo jamaa hazijui Xtrail achana nae. Ukiona gari namba "A" inadunda kama mpya elewa hiyo gari ni nzuriMafundi wabongo ndiyo wakijinga...kawaulize Wajapani......wakishindwa kutengeneza kitu hawataki kukubali kuwa wameshindwa...wanaaza kusingizia kuwa hakifai.....
Ingekuwa ni gari ya kijinga ungeshasikia recall huko kiwandani na leo hii kusingekuwepo na Xtrail Generation ya tatu..
MZee unataka kumaliza kisahaniSubi. STI.. yaani hapo hizo vx v8 tunasumbuama sio zinanisumbuaView attachment 1643021
Bado elimu kuhusu cc za magari inabidi itolewe sana,sasa una kagari ka cc 2000 unaweka ligi na la cc 2500 mpaka 3000 unampita yeye anakuangalia unajisifu,sema hao uliowapita hawajaamua kukaza roho walikuwa wanakuangalia tu.Heshima kwenu wakuu.
Wiki iliyopita niliamua kuifanyia nissan dualis majaribio ya mbio barabarani.( nilikua natafuta ligi kwa udi na uvumba)
Nilitenga hela ya faini 150,000.00 kwa safari ya kutoka Dsm to Singida. Ilipigwa 100,000 nikabaki na 50,000.
Nilianza ligi na Vanguard, crown, subaru. Crown alikuwa ni mjeshi yeye anapita tuu
Ila hadi tunaingia morogoro crown na subaru tumeziacha nyuma sana.
Kufika Moro, vanguard na mimi na Nissan patrol (DFP)
Vanguard mziki ulimshinda akakaa nyuma nahisi aliogopa trafiki,
Nilifika Mbande ilibidi nikachungulie dereva wa Nisan Patrol ni nani, yule mzee anaendesha gari kama pikipiki anaovertake sehemu hatari balaa
Alikuwa anakimbia aseee, huyu ndio alinipa challenge kwakuwa alikuwa haniachi 500m.
Nissan Dualis ni mnyama sana, hata nikisema nipate gari, narudi kwa Dualisi tena.
Hongereni sana trafiki mnafanya kazi ipasavyo.
Akituma nitag mkuu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] muongo..sbr atume izo picha....M5 mpower V8 mchezo nini..
Hivi top speed ya 320km/h unaifahamu mkuu?Waliondesha Mercedes waulizeni hasa zile za 320/kph. Mtambo huo. Ukikimbia kifua kinagusa chini!
Me ndhani uanzishwe uzi maalumu wa kuelimisha watu maana ya CC, HP, power to weight ratio, Uhusiano uliopo kati ya CC na HP ni upi..?Bado elimu kuhusu cc za magari inabidi itolewe sana,sasa una kagari ka cc 2000 unaweka ligi na la cc 2500 mpaka 3000 unampita yeye anakuangalia unajisifu,sema hao uliowapita hawajaamua kukaza roho walikuwa wanakuangalia tu.
Kuna gari nyingi zipo na CC 2000 zinakamua zenye CC 3500 na kuendelea.Me ndhani uanzishwe uzi maalumu wa kuelimisha watu maana ya CC, HP, power to weight ratio, Uhusiano uliopo kati ya CC na HP ni upi..?
Wakati gani mtu atambe na CC zake kuubwa na ni wakati gani Mwenye HP kubwa atambe...
Bado tuna safari ndefu...
Elimu ya CC na Hp ikikaa vizuri nadhani watu hawatakaa wakibishana tena kuhusu mambio..
Kwa mfano Mazda RX 8 kama sikosei, ina Cc zisizozidi 1300 lakini hizo CC 2500 za kwenye Brevis au Crown hazifui dafu kwa hiyo Mazda....
Nissan GTR yenye VQ35 ina CC 3500 mpaka 3700....Hizo V8 zitasoma namba tu hapa
Hapo ndiyo linakuja suala la HP na Power to weight ratio...
Kwa hiyo usije ukawa na CC kuubwa ukadhani ndiyo kila kitu..
Nissan dualis inakuja na gear box ya cvt (yaan continuous variable transmission) gear box hii ubalishaji wake wa gear ni tofauti na normal automatic gear box.. so with cvt gari inachanganya fasta na hata wakati wa ku overtake huwazi... Changamoto na angalizo... Cvt gearbox za nissan ni very weak kwakua hazijawa designed for high engine torque (yaan kukanyaga gas pedal mpaka chini ili gari ichangamye fast) zimekua designed for fuel efficiency.. so be careful maana uta kuja kuharibu gearbox yako prematurely..Mmenichekesha sana na comment zenu looh.
Kiufupi napenda sana kundesha gari na napenda ligi ila kuna muda hjwa nasema je likitokea la kutokea.......!! Naanza kiwakumbuka wote waliokwishaniambia wananipenda, nafikiria vile watakuwa wanalia kwa uchungu nikiwa nimekufa kwa ajali......
Basi narudisha kisigino nyuma naanza kwenda mwendo wa kibalozi km 80 pale inapobidi, na 50 mpaka 30 pale nnapotakiwa kutii.
Na safari za nje ya Dar nikiwa naendesha binafsi huwa naifanya sehemu ya starehe, ambapo mwendo usio na ligi unaniondolea stress za kuovertake na kukaza tako [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
[emoji16][emoji16]Dualis Qashqai sio gari. Endeleeni kujadili ujinga huo
Umesahau kuwa Engine Capacity ya VX V8 ni kubwa sana na acceleration yake in 30 seconds is remarkable.Leave alone confortability sasa barabarani huwa tunaziita ndege ya chiniHujakutana na VX V8 mkuu? Hawa jamaa wanatembea aise. Unaichapa mashine 190kph halafu bado wanakuchapa kama umesimama sina ham nao. Unakaza pedal mpaka tako lakini ndio kwanza inazidi kupotea
Zipo , ila sio nyingi. Nyingi ni 260/kphHivi top speed ya 320km/h unaifahamu mkuu?
Hebu angalia benz models ambazo zinafikia top speed hio na uniambie unaziona hizo gari ziko ngapi hapa bongo mkuu.