Nilichanjwa dawa ya kupendwa na wasichana

Nilichanjwa dawa ya kupendwa na wasichana

Mngurimi

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2020
Posts
819
Reaction score
790
Katika maisha yangu tangu utotoni hadi wakati huu wa ujana wangu nimekuwa karibu sana na mambo ya imani za kishirikina. Haimaanishi kama mimi ni mchawi wala mganga wa kienyeji ila tu ukaribu na watu wanaonizunguka unafanya niweze kushiriki mambo haya wakati mwingine kwa kupenda au kwa kutokupenda.

Nilipofikisha umri fulani hivi wa kubalehe kama mjuavyo huwa ni wakati ambao sexual desire inaanza kumpata sana mtu. Kama binadamu wengine na mimi nilipatwa na hali hii sambamba na zile ndoto nyevu kila nikilala (I think you know).

Siku moja mimi na jamaa yangu fulani hivi tukawa tukiwaza namna gani ya kuwadaka warembo wakali waliokuwa wakitusumbua pale mtaani. Jamaa kwao kulikuwa na duka la kuuza bidhaa za matumizi ya kawaida, akaingia dukani akachukua (naweza kusema aliiba) shilingi elfu 10 ya bluu kwa wakati huo. Basi bwana, tukanyooka moja kwa moja hadi kwa mtaalamu mmoja na azma yetu kubwa tupate dawa ya wasichana not otherwise.

Mganga mwenyewe alishangaa kwa umri ule mdogo tuliokuwa nao eti tunataka dawa ya kupendwa. Mganga hakuwa na cha kuongeza wala kukataa hasa baada ya kuona ile noti ya msimbazi, akaingia kwenye vibuyu vyake akachukua dawa fulani hivi nyeusi akachanganya na asali kisha akaanza kumchanja rafiki yangu. Mimi nilikuwa naogopa kuchanjwa ila kwa uzito na shauku ya kupata watoto wazuri ilibidi niridhie.

Wakati akiendelea na kutupa tiba alitoa tahadhari akasema hii dawa ni hatari kwa sababu tunaweza kuharibu masomo yetu au kupata magonjwa ya zinaa. Sisi hatukujali tukasema tupo makini na tunajitambua. Nakumbuka ile dawa ilikuwa inachanjwa kwenye ulimi, kwenye goti na juu ya kidole cha mwisho cha mguu. Hapo tukawa tayari na tukarudi zetu kitaa, sharti kubwa siku hiyo ilikuwa ni kuacha kuoga tu.

Baada ya siku kadhaa kwenye majaribio ndiyo niliamini kuwa watu wana dawa, yaani sikuwahi kutongoza msichana akatae, nakumbuka darasani nilipita na watoto wote wakali japo kuna wawili walikuwa wabishi ila baadaye walitoa mzigo.

Mwenzangu yeye ndiyo alikuwa chinja chinja na uzuri wake habagui kiwe kisu au mong'o yeye hajali. Hata pale tulipogonganisha wasichana huwezi kuamini walikuwa waleti noma na wanaweza kuwa hata marafiki. Baada ya miaka kadhaa mwenzangu akapata kisonono cha hatari, hapo ndiyo nikaogopa na kuanza kuhisi hata mimi naweza kuugua magonjwa hatari.

Kuna siku nikiwa shule walikuja watu wageni fulani na walikuwa wanapima UKIMWI. Mimi sikuwahi wala sikutaka kupima kwa hofu ila lilikuja kundi la wadada takriban 7 wakilazimisha nikapime. Ilikuwa ni ngumu sana ila kwa aibu na hofu kubwa nilipima na ninashukuru sana nilikuta nipo salama. Tangu hapo niliacha kabisa nikawa mwoga japo dawa ilikuwa ipo mwilini.

Lengo la uzi huu ni kuwapa ushauri tu wale wanaotaka au wanaocheza michezo kama hii kuwa makini au kuepuka kabisa. Hakuna faida ya uzinzi na uasherati tofauti na kujichosha huku ukipoteza pesa zako. Kesi za mimba na kuumia Kisaikolojia nazo huwezi kuzikwepa. Mimi kwa sasa sitaki na wala sina time na hata dawa yenyewe niliizindua na ninashukuru sasa najiona mpya. Mwenzangu yeye alishaoa na ana watoto wawili, tukikutana huwa tunajikumbusha ule ujinga tunaaza kucheka tu.

Hakika hii dunia ina mambo mengi sana😀

Kutoka kwa K.L
 
"Hakuna faida ya uzinzi na uasherati tofauti na kujichosha huku ukipoteza pesa zako"

Mada nzima nimekuelewa hapa na ndio maana nimetuliza kibamia changu..
Lkn kuna roho wa nani nani sijui huko anateta nami ananiambia "unafikiri ukikaa tu utakuja kupata watoto kama kina bill gate"..😂😅

Bwana na asimame upande wangu..
 
Ha ha ha sawa sawa.... Mi nlitaka nkaitafute, ko unamwambia niache sio

Moja kati ya athari ya dawa za kishirikina huwa inafikia wakati zinaishiwa nguvu, wakati mwingine unaweza kuharibu masharti au ukavuka sehemu zenye miiko ya kuua dawa mfano, mito, milima au miti mikubwa.

Pia ukihiari unaweza kuiua na hata mtu akiwa mchawi akahiari mwenyewe anaweza kuacha ila asipohiari humtoi
 
Back
Top Bottom