Nilichogundua shida maofisini kwenye utoaji wa huduma hazipo kwa Mabosi, zipo kwa wasaidizi

Nilichogundua shida maofisini kwenye utoaji wa huduma hazipo kwa Mabosi, zipo kwa wasaidizi

Wengi wao huwa wana upeo mdogo mno wa akili + hekima! Wewe ukitaka kuwapatia ukifika tuu anza na kumpongeza hata kama kavaa malunyalunya utaona anatoa ushirikiano! Wote wana tatizo moja michongo mingi ya mabosi wao wanaiona sasa wanapoambulia patupu hasiri huwa ni kwa kila mtu!
🤣🤣🤣Ndo maana unakuta ps asubuhi tu kanuna kinoma mpaka unashangaa
 
Husika na mada hapo juu tunawaomba MA-PS (Baadhi), huko MAOFISINI mtuhudumie kwa upendo na kwa haraka, nimefanya utafiti kidogo nimegundua kumbe mabosi wana moyo wa kutuhudumia Ila wanakwamishwa na masekretari wao.

Mfano;
1. Ps unamsalimia hakujibu kwa makusudi.
2. Ps anakataa usionane na boss umwambie shida yako.
2. Ps anakaa na file lako mpaka siku 3 bila kumpelekea Boss.
3. Ps anakununia bila sababu
4. Barua yakuandika dk20 anasema uende baada ya siku 3
IKUMBUKWE, KUHUDUMIA WATU KWA MOYO NA UPENDO NI IBADA, Badilikeni.
Hujui unafiki wa mabosi wewe, umeshapata wa kumtupia lawama, ndio bosi anavyotaka.
 
Ukiona wafanyakazi wa chini wana shida jua bosi ndie ana shida zaidi

Kazi ya bosi ni kusimamia utendaji kazi kwa wafanyakazi walio chini yake

Wakiwa wabovu huyo bosi mbovu hakustahili kuwepo kwenye hiyo nafasi anapaswa kuondolewa awekwe mwingine atakayekuwa na uwezo wa kusimamia wafanyakazi wa chini watoe huduma nzuri
 
Hujui unafiki wa mabosi wewe, umeshapata wa kumtupia lawama, ndio bosi anavyotaka.
Mm naona ni tabia ya mtu tu, kwamba boss anataka hvo ili kuwakatisha tamaa wateja wasiwe wanakuja kupata huduma kwake ili awe huru kuchat sidhan
 
Ukiona wafanyakazi wa chini wana shida jua bosi ndie ana shida zaidi

Kazi ya bosi ni kusimamia utendaji kazi kwa wafanyakazi walio chini yake

Wakiwa wabovu huyo bosi mbovu hakustahili kuwepo kwenye hiyo nafasi anapaswa kuondolewa awekwe mwingine atakayekuwa na uwezo wa kusimamia wafanyakazi wa chini watoe huduma nzuri
Sometimes ofs ipo mbali Sana na boss, na ps kala age balaa Ila ndo hvo Ni mwendo wa nyodo na dharau kwa wateja mwanzo mwsho.
 
wadada wengi wao ni wabaya sana wakiwa wanafanya kazi sekta yoyote au offisi yoyote hospitalini magereza suma polisi hata biashara ya mtu awe anauza simu duka la mtu huwa wanajiona sana sana hili nimeliona hasa hasa tanzania tu, ukienda nchi zingine wadada wanahudumia vizuri sana
 
wadada wengi wao ni wabaya sana wakiwa wanafanya kazi sekta yoyote au offisi yoyote hospitalini magereza suma polisi hata biashara ya mtu awe anauza simu duka la mtu huwa wanajiona sana sana hili nimeliona hasa hasa tanzania tu, ukienda nchi zingine wadada wanahudumia vizuri sana
Yah! Customer care kwao ni zero kabisa wamejaa majiono na dharau badala ya kufanya kazi kwa uaminifu na wakishaambiwa ni wazuri basi watabaki wanamaintain uzuri wao hata kazi hawafanyi ipasavyo.
 
wadada wengi wao ni wabaya sana wakiwa wanafanya kazi sekta yoyote au offisi yoyote hospitalini magereza suma polisi hata biashara ya mtu awe anauza simu duka la mtu huwa wanajiona sana sana hili nimeliona hasa hasa tanzania tu, ukienda nchi zingine wadada wanahudumia vizuri sana
Mixer awe na mahusiano na boss wakešŸ˜„šŸ˜„ utaona Moto, utajiuliza hii Ni ofs ya umma au nyumba ya wanandoa?🤣
 
Sometimes ofs ipo mbali Sana na boss, na ps kala age balaa Ila ndo hvo Ni mwendo wa nyodo na dharau kwa wateja mwanzo mwsho.
Swala la umbali sio

Boss kukubali ubossi kipingele kimojawapo ni je una uwezo wa kusimamia walio chini yako.kwenye ofisi busy na mazingira yeyote?

Mabodi wengi hutumbuliwa sababu ya kutowasimamia hao watu wa chini
Wanabaki kujifamyia watakavyo

Hilo sio tatizo lao kabisa ni la bosi anayewasimamia hana mbinu xz kuhakikisha wanatoa huduma nzuri ziwe za upole au kikatili

Sababu kutoa huduma mbovu kwa mtumishi wa chini ni kukatili cheo cha bosi aonekane hafai kwenye cheo chake

Dawa ya moto ni moto

Ningekuwa mimi ndio boss wao hao watoa huduma mbovu wangenikoma au zangu ama zao
 
Husika na mada hapo juu tunawaomba MA-PS (Baadhi), huko MAOFISINI mtuhudumie kwa upendo na kwa haraka, nimefanya utafiti kidogo nimegundua kumbe mabosi wana moyo wa kutuhudumia Ila wanakwamishwa na masekretari wao.

Mfano;
1. Ps unamsalimia hakujibu kwa makusudi.
2. Ps anakataa usionane na boss umwambie shida yako.
2. Ps anakaa na file lako mpaka siku 3 bila kumpelekea Boss.
3. Ps anakununia bila sababu
4. Barua yakuandika dk20 anasema uende baada ya siku 3
IKUMBUKWE, KUHUDUMIA WATU KWA MOYO NA UPENDO NI IBADA, Badilikeni.
kuna masjala ya mkurigenzi manispaa ya moshi aisee wale baadhi ya wamama wana gubu sijawahi ona!!!!
 
Swala la umbali sio

Boss kukubali ubossi kipingele kimojawapo ni je una uwezo wa kusimamia walio chini yako.kwenye ofisi busy na mazingira yeyote?

Mabodi wengi hutumbuliwa sababu ya kutowasimamia hao watu wa chini
Wanabaki kujifamyia watakavyo

Hilo sio tatizo lao kabisa ni la bosi anayewasimamia hana mbinu xz kuhakikisha wanatoa huduma nzuri ziwe za upole au kikatili

Sababu kutoa huduma mbovu kwa mtumishi wa chini ni kukatili cheo cha bosi aonekane hafai kwenye cheo chake

Dawa ya moto ni moto

Ningekuwa mimi ndio boss wao hao watoa huduma mbovu wangenikoma au zangu ama zao
Upo sahihi kabisa mkuu. ....boss inabidi uwasimamie subordinates wako uhakikishe wanatoa huduma kwa haraka na kwa ufanisi pia
 
Mimi kupitia roho mbaya ya Yule mama nilipewa zawadi ya shamba heka moja ndani ya Mkoa mmoja wapo wa kanda ya ziwa.

Yule mama ni mtumishi mwenzangu, Kilichotokea nilikuwa napita kwenye korido la ofisi nikakutana na Bibi age imeenda ana documents zote zinazohitajika mkononi.

Mimi: Mama Shikamoo!!

Mama: Marhaba mwanangu, naomba unisaidie.

Mimi: Nini Shida mama.

Mama: Mwanangu nimekuja kumdhamini mtoto wangu ana kesi apa, nimeambiwa nimuone mama Fulani ndo atanisaidia Ila amenisimamisha hapa masaa mawili, Nisaidie mwanangu nimekuja na Mzee yupo nje nae miguu inamsumbua Sana.

Mimi: Naomba nione Documents mama (Ananipa nasoma soma zote zimekamilika)
Mama naomba nifate.

Namfata muhusika mama Fulani (Mtumishi mwenzangu) Namuhoji huyu mama mbona ameambiwa akuone ww ndo utaweza kumsaidia amekaa Hapo kwenye korido zaidi ya masaaa mawili naomba umsaidie basi. (Yupo busy anachezea simu uku ananijibu uyo Bibi msumbufu nilimwambia alete pamoja barua za utambulisho kutoka serikali za mitaa ziligongwa muhuri kwenye passport size na nakala ya kitambulisho cha NIDA)

Mimi: Mbona kila kitu kipo sawa barua za mwenyekiti zipo, nakala ya kitambulisho cha NIDA kipo na Documents nyingine za muhimu hizi hapa. Naomba msaidie ana mgonjwa uko nje anamsubiri na wametoka kijiji cha mbali.

Mama Flani( Mtumishi Mwenzangu): Sawa, Ila muda umeisha waambie waje kesho

Mimi: ( Naangalia saa Bado Dk 30 muda wa KAZI uishe.) Nachukua maamuzi ya haraka naingia ofisini Kwa Boss wangu moja kwa moja nikiwa na Documents za Yule Bibi namuelezea Kwa upana anaelewa. Anazipitia Documents anaridhia, zinagongwa muhuri na saini. Kibali cha dhamana kinatoka. Naambiwa mwambie Bibi Angie ndani.
Naenda kumuita anasikilizwa Mimi nipo pembeni. Boss anatoa order ya dhamana Kwa mtuhumiwa.

Haraka Sana ndani ya Dk 20 kijana anaachiwa Kwa dhamana. Bibi anamchukua kijana wake wanaondoka baada ya kuagana.

Narudi ofisini kwangu ili nijiandae kutoka sababu muda wa kazi umeisha. Mara nasikia mlango wa ofisi unagongwa namwambia apite kumbe ni Yule kijana wa Yule mama aliyeachiwa Kwa dhamana.

Kijana: Kaka samahani Mzee na mama wamenituma nije nikuombe namba ya simu na wanashukuru Sana Kwa msaada uliowapa.
(Nampatia kijana namba. Tunaagana wanaondoka.)

Zinapita wiki mbili naenda likizo. Baada ya likizo ya Mwezi mzima narudi Job.

Siku hiyo nipo nyumbani napigiwa simu namba ngeni. Nauliza Nani mwenzangu!!

Najibiwa Mimi Mama Fulani ulitusaidia siku zile kesi ya kijana wetu. Hata hivyo kesi iliisha salama na kijana alishaachiwa. Tulikutafuta tukaambiwa upo likizo. Vipi umesharudi Baba angu?

Mimi: Asante mama, nilisharudi kazini.

Mama Fulani: Baba, Mzee anaomba jumamosi upatapo nafasi uje kijiji Fulani ukifika ulizia Kwa boda boda wakulete Kwa Mzee Fulani, Usiniangushe Baba angu Mzee atafurahi mno kukuona.

Mimi: Sawa mama nitajitahidi kufika. (Tunaagana)

Siku ya tukio napanda gari kutoka mjini Hadi uko kijijini (mwendo wa saa NNE) nafika naulizia Kwa Mzee Fulani ni wapi? Boda ananipeleka.

Nafika, baada ya salamu na maongezi mafupi. Chakula kinaletwa Lahaula!! nimechinjiwa jogoo na wali Safi. ( Nakula nashiba)

Nawashukuru pale, Mzee anajadiliana na mkewe mara kijana anatumwa akamuite mtendaji wa kijiji, na mjumbe WA nyumba kumi sijakaa Sawa na majilani wameitwa.

Naambiwa Kuna kikao pale nisiwe na hofu, natambulishwa naambiwa wao Kama familia wameamua kunikatia sehemu ya shamba lao heka moja Kwa ajili ya shukrani na utu wangu kwao.

Mkataba unaandikwa pale , naoneshwa majirani zangu tuliopakana mipaka ya shamba, mashahidi wanasaini. Nakabidhiwa nalala zangu nao wanabaki na zao. Tunaagana naondoka kurudi Nyumbani.

Ukweli ni kwamba: Taasisi nyingi za serikali kupata huduma bila kusumbuliwa au kuhangaishwa ni ndoto. Wengi hupata huduma nzuri kutegemea kujuana na mtu Flani au laah iwe Tu imetokea mtoa huduma ana moyo wa kipekee.

Kitu kibaya zaidi usiombee uhudumiwe na hawa mama zetu au dada zetu, ni zaidi ya mateso. Dharau, kujishaua, Mateso, Kiburi yaani sijui hata kwann inakuwaga hivyo.

Customer Care Kwa Bongo Bado Sana.
Ni Mungu Tu.
 
Husika na mada hapo juu tunawaomba MA-PS (Baadhi), huko MAOFISINI mtuhudumie kwa upendo na kwa haraka, nimefanya utafiti kidogo nimegundua kumbe mabosi wana moyo wa kutuhudumia Ila wanakwamishwa na masekretari wao.

Mfano;
1. Ps unamsalimia hakujibu kwa makusudi.
2. Ps anakataa usionane na boss umwambie shida yako.
2. Ps anakaa na file lako mpaka siku 3 bila kumpelekea Boss.
3. Ps anakununia bila sababu
4. Barua yakuandika dk20 anasema uende baada ya siku 3
IKUMBUKWE, KUHUDUMIA WATU KWA MOYO NA UPENDO NI IBADA, Badilikeni.
ps wanakuwa na kiburi sana kwasababu washaona sehemu za siri za maboss wao na ukiwazingua ujue umemzingua boss, au la, ps wana siri nyingi za uhalifu wa boss wao hivyo hata akifanya fyongo boss hawezi kuwafanya chochote kuogopa watamwaga mboga. ukiweka vipimo hivyo utakuwa wote ni walewale tu, boss hadi ofisi nzima. ndo mambo ya utafutaji hayo hadi boss anajikuta amekuwa mtumwa wa ps.
 
Halmashauri ya mbulu mji niwape maua yao kuanzia mkurugenzi mpaka wafanyakazi wa chini yake,jamani yule baba sijui kama huwa anapumzika vyema jamani,ni anajua matakwa ya binadamu
Yule baba na ofisi yake wanafanya kazi jamani
Na utashangaa wale ps ni aged kidogo he and she wanachapa kazi balaa
 
Halmashauri ya mbulu mji niwape maua yao kuanzia mkurugenzi mpaka wafanyakazi wa chini yake,jamani yule baba sijui kama huwa anapumzika vyema jamani,ni anajua matakwa ya binadamu
Yule baba na ofisi yake wanafanya kazi jamani
Na utashangaa wale ps ni aged kidogo he and she wanachapa kazi balaa
Hongera zao... watumishi wote wangejitoa hivyo hzo lawama zisingekuwepo Ila bado Kuna sehem ma ps wanawakatili Sana wananchi wanaendekeza Sana delay zisizo za msingi
 
Back
Top Bottom