Uchaguzi 2020 Nilichoshuhudia kwenye kampeni za Tundu Lissu Sumbawanga, CHADEMA inafeli kwenye mikakati

Uchaguzi 2020 Nilichoshuhudia kwenye kampeni za Tundu Lissu Sumbawanga, CHADEMA inafeli kwenye mikakati

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Habarini wapiga kura wenzangu.

Jana nilipata fursa ya kuhudhuria mkutano wa Kampeni wa mgombea wa CHADEMA ndugu Tundu Lissu, kiukweli watu walijitokeza wengi sana kumlaki na walionesha ushirikiano kwa kumsindikiza kwa maandamano hadi hotelini kwake hiyo ni mida ya saa mbili usiku, polisi walijaribu kuwazuia bila mafanikio.

Wakati anaanza kujinadi alianza vizuri kwa utangulizi lakini kadiri mda ulivyoenda sikuona akinadi na kuwakumbusha sera yake kuu ya bima ya afya kwa wote na kui-connect na hali za maisha ya watu halikadharika jinsi hiyo sera ya bima ya afya ilivyomsaidia hata yeye kupona huko Ulaya, maana kiukweli ukiwatazama watu wengi walikuwa na nyuso za huruma na machozi kwamba hawaamini huyu bwana alipona kutokana na shambulio lake.

Sera ya bima ya afya, uhuru na maendeleo ya watu anatakiwa atembee nazo kila anapokwenda na ainadi tena kwa kutumia mfano wake mwenyewe maana inahusu hadi kuboresha sekta ya afya na Lishe moja kwa moja. Lakini pia niliwahi msikia kwamba ataitumia gesi na madini mengine kuwa dhamana ya kupata pesa za kugharamia bima ya afya kwa wote. Ilitakiwa aifafanue kwa utaratibu huu.

Alizungumzia hoja ya kuweka ukanda huru wa biashara hasa kwa mikoa hii ya mpakani lakini, hii hoja hakuweza kuifafanua kwa lugha nyepesi ili watu wa kawaida waelewe,mathalani wanavyoweza kunufaika na biashara huria ya mipakani,angetolea mfano wa Tunduma ambako kilo moja ya sukari kutoka Zambia na Malawi ni sh.2000 wakati hiyi hiyo sukari hairuhusiwi kuuzwa huku Sumbwanga,kwa nini pale iuzwe na hapa ikatazwe wakati mkoa huu pia unashea mipaka na Zambia?

Watu wangeelewa hoja ya ukanda huru wa biashara kwa mfano huo mwepesi ilhali sukari ya Tzn ni sh. 3000-3200/= kwa mkoa huu, nk nk. Lakini pia alitakiwa atumie fursa hii kuinadi sera yake ya kuondoa utitiri wa kodi na kuwa na makisio makubwa ya kodi ili kuwapa fursa wananchi kujiajiri na kufurahia kulipa kodi .

Tatu kwa Mikoa hii ya Nyanda za Juu Kusini kuanzia Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe na Rukwa shughuli kuu ni kilimo na biashara za kuvuka mipaka lakini hakuweka ufafanuzi wa namna atakavyowainua wakulima ambapo kwa ukanda huu ilifaa azungumzie pembejeo na mambo ya masoko na shughuli za ugani, sasa alizungumzia kidogo akiwa Chitete Momba tena akiwalenga zaidi watu wa Momba wakati ilitakiwa iwe hoja kuu ukanda wote huu.

Hapa ndipo angweza kueleza jinsi vikwazo na mageti yanayowekwa na serikali kuwanyonya wakulima, kupangiwa wanunuzi,kuzuiwa kuuza popote utakapopata soko na kusaidiwa pembejeo na kuwekewa bima za mazao bila kusahau pembejeo.

Kwa Iringa na Njombe angweza kuelezea jinsi ambavyo wafanyabiashara wa misitu na mazao yake wanavyolialia kwa tozo zaidi ya 20 maana waliwahi Mwambia rais alipokuwa ziarani Njombe sasa yeye ange-capitalize hizi kero na kuahidi kuzifuta na pia angeeleza jinsi mahusiano mabaya kati ya Tzn na Kenya yalivyowaathiri wakulima wa miti na horticulture maana soko lao kubwa ni Kenya.

Nne watu wa CHADEMA hawako makini au hawana taarifa sahihi za mabo ya kiuchumi maana huwezi kuwa unasema miradi ya reli haina tija kwa sasa(maendleo ya vitu) at the sama time unaahidi kujenga reli kati ya Mpanda-Sumbawanga-Tunduma. Huku ukisema CCM wameua reli ya Tabora-Kaliua-Mpanda wakati iko hai na inafanya kazi, huku ni kujichanganya na kukosa umakini na taarifa sahihi.

Kwanza sina hakika kama reli hii anayoahidi TL ni economically viable maana ukanda huu hauna mzigo mkubw kihivyo kiasi cha kuhitaji reli, pili ukanda huu una mipaka mingi na nchi jirani trade liberalization tu ndio inafaa na kuwawezesha watu kuzifikia nchi hizo jirani.

Mwisho Watu wa CDM hawana watu makini wanaoweza kuchambua takwimu za serikali, sera nk nk kama walivyo akina Zito, Lipumba, Bashe nk ,ni rai yangu watafute au wa-recruit watu wenye talent za uchambuzi watawasaidia sana kuweza kuchambua sera na takwimu za serikali na kuzihusianisha na maisha ya watu, akina ZZK wa ACT WAZALENDO waliweza kuonesha kwa kuichambua ilani ya CCM na utekelezaji wake na kuhitimisha kwamba CCM imetekeleza 31% tu ya ilani yake. Pili inatakiwa kabla ya mgombea wao kuhutubia wahakikishe wanatafuta kero stahiki za watu wa eneo husika ili zitumike kukoleza kwenye sera zao mama.

All in all kampeni ya jana kwa Mkoa wa Rukwa naona ilifanikiwa maana sio jambo la kawaida kwa watu wa mkoa huu kugeukia upinzani ghafla pengine ni kutokana na kupata wahamiaji wengi wa mikoa ya jirani kama Iringa, Mbeya na Songwe ambao wamewaambukiza tabia za kutoburuzwa na kudanganywa na CCM.

Karibuni kwa michango.
 
..ushauri wako ni mzuri.

..ilitakiwa watu walioko majimboni ndio wampe mgombea pointi za kuongea.

..mambo mengi uliyoshauri yangewezekana kama wasomi wazuri wangekuwa na uhuru wa kujiunga na vyama vya upinzani.

..tulifika mahali wananchi wamekuwa na uoga kushiriki ktk shughuli za wapinzani, au kuonyesha mapenzi kwa chama hicho.

..ukiwauliza cdm insiders kuhusu masuala haya uliyoibua majibu yao ni kwamba milango ya Chadema iko wazi, na wako tayari kupokea ushauri, tatizo wananchi wanaogopa misukosuko toka kwa wenye dola.
 
Lissu anajitahidi ila sera ya majimbo inamuangusha. Mfano, Gesi ya Mtwara siyo Mali ya jimbo la kusini? Kwa nini itumike kugharamia bima ya afya kwa wote na mafao ya wazee ilhali mapato ya Tanzanite na utalii kaskazini yatumike kwa kaskazini tu?
 
Hii ndiyo maana ya kauli mbiu ya - UHURU, HAKI na MAENDELEO...

Watu wawe huru kukosoa na kushauri ikilazimika hata wawacheke ama wawazomee viongozi wao wanapofanya mambo ya kijinga.....

Umemkosoa Tundu Lissu na Team Kampeni yake. Point taken, noted...

Hii ni tofauti sana na upande wa kampeni za Inzi wa kijani...

Jana Bukoba mgombea wa CCM kuguniwa na kuzomewa kidogo akatoa amri wote waliozomea wawekwe ndani lock up....!

Huyu haamini kabisa kuwa yeye ni binadamu na kuwa huwa anakosea pia. Hana uvumilivu kabisa hata katika mambo simple, natural na ya kawaida kabisa...!

Hafai kuwa kiongozi wa watu huyu...
 
Nimefurahishwa jinsi ulivyo positive kimtazamo. Mimi pia nilifatilia japo kwa kiasi ule mkutano wa Sumbawanga na Momba nikaona kabisa wasaidizi wa Lisu wanafanya uvivu kumtafutia taarifa sahihi.

Maana kwa kweli wafuasi anao na unaona kabisa wana hamu ya kumsikiliza.
 
Lissu anajitahidi ila sera ya majimbo inamuangusha. Mfano, Gesi ya Mtwara siyo Mali ya jimbo la kusini? Kwa nini itumike kugharamia bima ya afya kwa wote na mafao ya wazee ilhali mapato ya Tanzanite na utalii kaskazini yatumike kwa kaskazini tu?
Serikali za Majimbo haimaanishi kila jimbo litategemea resources zake tu. Pale ambapo mali zipo wanatakiwa wafaidike nazo, lakini kuna serikali kuu itakayokusanya kodi na pia kukusanya mapato kiasi fulani kutoka majimboni. Mapato hayo yataiwezeshesha serikali kupeleka kiasi fulani cha fedha hizo kwenye majimbo hasa yale yalioko nyuma na pia kuiwezesha serikali kuu kufanya kazi za serikali kuu.
 
Lissu anajitahidi ila sera ya majimbo inamuangusha. Mfano, Gesi ya Mtwara siyo Mali ya jimbo la kusini? Kwa nini itumike kugharamia bima ya afya kwa wote na mafao ya wazee ilhali mapato ya Tanzanite na utalii kaskazini yatumike kwa kaskazini tu?

..sera ya majimbo haimaanishi kwamba kila jimbo litakuwa kivyake-vyake.

..hivi kwa mtizamo wako ikitokea jimbo la kusini limevamiwa kijeshi ina maana wataachiwa wenyewe wapigane?

..lingine ukumbuke kwamba wewe kama Mtanzania una haki ya kuishi popote pale. kwa hiyo unaweza kuwa umezaliwa kusini lakini ukaenda kutafuta fursa kaskazini au pwani na hivyo kujikuta umekuwa mwenyeji wa kanda tofauti na ulipozaliwa.
 
All in all kampeni ya jana kwa Mkoa wa Rukwa naona ilifanikiwa maana sio jambo la kawaida kwa watu wa mkoa huu kugeukia upinzani ghafla pengine ni kutokana na kupata wahamiaji wengi wa mikoa ya jirani kama Iringa, Mbeya na Songwe ambao wamewaambukiza tabia za kutoburuzwa na kudanganywa na CCM.
 
Serikali za Majimbo haimaanishi kila jimbo litategemea resources zake tu. Pale ambapo mali zipo wanatakiwa wafaidike nazo, lakini kuna serikali kuu itakayokusanya kodi na pia kukusanya mapato kiasi fulani kutoka majimboni. Mapato hayo yataiwezeshesha serikali kupeleka kiasi fulani cha fedha hizo kwenye majimbo hasa yale yalioko nyuma na pia kuiwezesha serikali kuu kufanya kazi za serikali kuu.
Historia IPO kutuonya tusirudie makosa. Soma hii vita utajua jinsi serikali ya majimbo isivyotufaa kwa sasa.
The American Civil War (also known by other names) was a civil war in the United States from 1861 to 1865, fought between northern states loyal to the Union and southern states that had seceded to form the Confederate States of America.
Combatants: United States, Union
Participant: United States
 
Mimi naona yote uliyosema mgombea anayazungumza kwenye mikutano yake. Cha msingi ni kuelewa kuwa mda ni mchache kuyazungumza yote kwa kina.

Kwa hiyo anatakiwa kuwa brief and straight to points. Ndiyo maana wananchi wanamuelewa na kumuunga mkono kwa wingi.
 
Historia IPO kutuonya tusirudie makosa. Soma hii vita utajua jinsi serikali ya majimbo isivyotufaa kwa sasa.
The American Civil War (also known by other names) was a civil war in the United States from 1861 to 1865, fought between northern states loyal to the Union and southern states that had seceded to form the Confederate States of America.
Combatants: United States, Union
Participant: United States

..mwanzoni kulikuwa hakuna marekani, bali kulikuwa na colonies ambayo unaweza kuita majimbo.

..hizo colonies ndiyo ziliungana na kutengeneza marekani, lakini zikabadilishwa majina na kuitwa majimbo.

..tatizo la marekani linatokana na historia ya jinsi nchi yao, taifa lao lilivyoanzishwa, na mamlaka ambayo majimbo yalikuwa nayo.

NB:

..majimbo yako Ujerumani, Canada, etc etc na hakuna vita yoyote baina yake.
 
Habarini wapiga kura wenzangu.

Jana nilipata fursa ya kuhudhuria mkutano wa Kampeni wa mgombea wa CHADEMA ndugu Tundu Lissu, kiukweli watu walijitokeza wengi sana kumlaki na walionesha ushirikiano kwa kumsindikiza kwa maandamano hadi hotelini kwake hiyo ni mida ya saa mbili usiku, polisi walijaribu kuwazuia bila mafanikio.

Wakati anaanza kujinadi alianza vizuri kwa utangulizi lakini kadiri mda ulivyoenda sikuona akinadi na kuwakumbusha sera yake kuu ya bima ya afya kwa wote na kui-connect na hali za maisha ya watu halikadharika jinsi hiyo sera ya bima ya afya ilivyomsaidia hata yeye kupona huko Ulaya, maana kiukweli ukiwatazama watu wengi walikuwa na nyuso za huruma na machozi kwamba hawaamini huyu bwana alipona kutokana na shambulio lake.

Sera ya bima ya afya, uhuru na maendeleo ya watu anatakiwa atembee nazo kila anapokwenda na ainadi tena kwa kutumia mfano wake mwenyewe maana inahusu hadi kuboresha sekta ya afya na Lishe moja kwa moja. Lakini pia niliwahi msikia kwamba ataitumia gesi na madini mengine kuwa dhamana ya kupata pesa za kugharamia bima ya afya kwa wote. Ilitakiwa aifafanue kwa utaratibu huu.

Alizungumzia hoja ya kuweka ukanda huru wa biashara hasa kwa mikoa hii ya mpakani lakini, hii hoja hakuweza kuifafanua kwa lugha nyepesi ili watu wa kawaida waelewe,mathalani wanavyoweza kunufaika na biashara huria ya mipakani,angetolea mfano wa Tunduma ambako kilo moja ya sukari kutoka Zambia na Malawi ni sh.2000 wakati hiyi hiyo sukari hairuhusiwi kuuzwa huku Sumbwanga,kwa nini pale iuzwe na hapa ikatazwe wakati mkoa huu pia unashea mipaka na Zambia?

Watu wangeelewa hoja ya ukanda huru wa biashara kwa mfano huo mwepesi ilhali sukari ya Tzn ni sh. 3000-3200/= kwa mkoa huu, nk nk. Lakini pia alitakiwa atumie fursa hii kuinadi sera yake ya kuondoa utitiri wa kodi na kuwa na makisio makubwa ya kodi ili kuwapa fursa wananchi kujiajiri na kufurahia kulipa kodi .

Tatu kwa Mikoa hii ya Nyanda za Juu Kusini kuanzia Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe na Rukwa shughuli kuu ni kilimo na biashara za kuvuka mipaka lakini hakuweka ufafanuzi wa namna atakavyowainua wakulima ambapo kwa ukanda huu ilifaa azungumzie pembejeo na mambo ya masoko na shughuli za ugani, sasa alizungumzia kidogo akiwa Chitete Momba tena akiwalenga zaidi watu wa Momba wakati ilitakiwa iwe hoja kuu ukanda wote huu.

Hapa ndipo angweza kueleza jinsi vikwazo na mageti yanayowekwa na serikali kuwanyonya wakulima, kupangiwa wanunuzi,kuzuiwa kuuza popote utakapopata soko na kusaidiwa pembejeo na kuwekewa bima za mazao bila kusahau pembejeo.

Kwa Iringa na Njombe angweza kuelezea jinsi ambavyo wafanyabiashara wa misitu na mazao yake wanavyolialia kwa tozo zaidi ya 20 maana waliwahi Mwambia rais alipokuwa ziarani Njombe sasa yeye ange-capitalize hizi kero na kuahidi kuzifuta na pia angeeleza jinsi mahusiano mabaya kati ya Tzn na Kenya yalivyowaathiri wakulima wa miti na horticulture maana soko lao kubwa ni Kenya.

Nne watu wa CHADEMA hawako makini au hawana taarifa sahihi za mabo ya kiuchumi maana huwezi kuwa unasema miradi ya reli haina tija kwa sasa(maendleo ya vitu) at the sama time unaahidi kujenga reli kati ya Mpanda-Sumbawanga-Tunduma. Huku ukisema CCM wameua reli ya Tabora-Kaliua-Mpanda wakati iko hai na inafanya kazi, huku ni kujichanganya na kukosa umakini na taarifa sahihi.

Kwanza sina hakika kama reli hii anayoahidi TL ni economically viable maana ukanda huu hauna mzigo mkubw kihivyo kiasi cha kuhitaji reli, pili ukanda huu una mipaka mingi na nchi jirani trade liberalization tu ndio inafaa na kuwawezesha watu kuzifikia nchi hizo jirani.

Mwisho Watu wa CDM hawana watu makini wanaoweza kuchambua takwimu za serikali, sera nk nk kama walivyo akina Zito, Lipumba, Bashe nk ,ni rai yangu watafute au wa-recruit watu wenye talent za uchambuzi watawasaidia sana kuweza kuchambua sera na takwimu za serikali na kuzihusianisha na maisha ya watu, akina ZZK wa ACT WAZALENDO waliweza kuonesha kwa kuichambua ilani ya CCM na utekelezaji wake na kuhitimisha kwamba CCM imetekeleza 31% tu ya ilani yake. Pili inatakiwa kabla ya mgombea wao kuhutubia wahakikishe wanatafuta kero stahiki za watu wa eneo husika ili zitumike kukoleza kwenye sera zao mama.

All in all kampeni ya jana kwa Mkoa wa Rukwa naona ilifanikiwa maana sio jambo la kawaida kwa watu wa mkoa huu kugeukia upinzani ghafla pengine ni kutokana na kupata wahamiaji wengi wa mikoa ya jirani kama Iringa, Mbeya na Songwe ambao wamewaambukiza tabia za kutoburuzwa na kudanganywa na CCM.

Karibuni kwa michango.
Hapo tayari na wewe unasubiri usiku urushiwe vocha na viongozi au wanachama wa chama hiki ulichokisifia ili ujiunge bando na hatimae kesho uje uandike madudu mengine unayoona yatakusaidia tena kurushiwa bando na hao nilio wataja hapo juu
 
Lissu anajitahidi ila sera ya majimbo inamuangusha. Mfano, Gesi ya Mtwara siyo Mali ya jimbo la kusini? Kwa nini itumike kugharamia bima ya afya kwa wote na mafao ya wazee ilhali mapato ya Tanzanite na utalii kaskazini yatumike kwa kaskazini tu?
Sera ya majimbo ni nzuri Sana ni suala kuifafanua tuu maana kinachobadilika kulingana na mikoa ni kwamba hapa unaunganisha mikoa na kuwa na Jimbo moja kubwa,sijui watu neno Jimbo wanalitadirije wakilidikia.
Nachojua Mimi kutakuwa na mambo ya serikali kuu na serikali za majimbo/mikoa/kanda. Kwani watu wa Nyasa wakitumia gas kuendeleza sehemu hiyo Kuna shida gani maana kile ambacho nao hawana watakipata kwingine au serikali inaweza sema madini au mafuta ni Jambo la serikali kuu lakini special treatments kwa maeneo husika ni lazima
Hii mambo ya kapu moja inafanya matumizi mabaya ya fedha ikiwemo kuweka miradi isiyo ya kipaombele kwa wananchi
 
Lissu anajitahidi ila sera ya majimbo inamuangusha. Mfano, Gesi ya Mtwara siyo Mali ya jimbo la kusini? Kwa nini itumike kugharamia bima ya afya kwa wote na mafao ya wazee ilhali mapato ya Tanzanite na utalii kaskazini yatumike kwa kaskazini tu?
Sera ya majimbo ni nzuri Sana ni suala kuifafanua tuu maana kinachobadilika kulingana na mikoa ni kwamba hapa unaunganisha mikoa na kuwa na Jimbo moja kubwa,sijui watu neno Jimbo wanalitadirije wakilidikia.
Nachojua Mimi kutakuwa na mambo ya serikali kuu na serikali za majimbo/mikoa/kanda. Kwani watu wa Nyasa wakitumia gas kuendeleza sehemu hiyo Kuna shida gani maana kile ambacho nao hawana watakipata kwingine au serikali inaweza sema madini au mafuta ni Jambo la serikali kuu lakini special treatments kwa maeneo husika ni lazima
Hii mambo ya kapu moja inafanya matumizi mabaya ya fedha ikiwemo kuweka miradi isiyo ya kipaombele kwa wananchi
 
Hii ndiyo maana ya kauli mbiu ya - UHURU, HAKI na MAENDELEO...

Watu wawe huru kukosoa na kushauri ikilazimika hata wawacheke ama wawazomee viongozi wao wanapofanya mambo ya kijinga.....

Umemkosoa Tundu Lissu na Team Kampeni yake. Point taken, noted...

Hii ni tofauti sana na upande wa kampeni za Inzi wa kijani...

Jana Bukoba mgombea wa CCM kuguniwa na kuzomewa kidogo akatoa amri wote waliozomea wawekwe ndani lock up....!

Huyu haamini kabisa kuwa yeye ni binadamu na kuwa huwa anakosea pia. Hana uvumilivu kabisa hata katika mambo simple, natural na ya kawaida kabisa...!

Hafai kuwa kiongozi wa watu huyu...
Huyo bwana hafai kabisa sijui ni specie gani
 
Shida madhira ya wananchi ni mengi, hawezi gusa yote, ardhi pia imeporwa na Halmashauri
 
Habarini wapiga kura wenzangu.
Jana nilipata fursa ya kuhudhuria mkutano wa Kampeni wa mgombea wa CDM ndugu Tundu Lisu,kiukweli watu walijitokeza wengi sana kumlaki na walionesha ushirikiano kwa kumsindikiza kwa maandamano hadi hotelini kwake hiyo ni mida ya saa mbili usiku,polisi walijaribu kuwazuia bila mafanikio..

Wakati anaanza kujinadi alianza vizuri kwa utangulizi lakini kadiri mda ulivyoenda sikuona akinadi na kuwakumbusha sera yake kuu ya bima ya afya kwa wote na kuiconnect na hali za maisha ya watu halikadharika jinsi hiyo sera ya bima ya afya ilivyomsaidia hata yeye kupona huko Ulaya,maana kiukweli ukiwatazama watu wengi walikuwa na nyuso za huruma na machozi kwamba hawaamini huyu bwana alipona kutokana na shambulio lake.Sera ya bima ya afya ,uhuru na maendeleo ya watu anatakiwa atembee nazo kila anapokwenda na ainadi tena kwa kutumia mfano wake mwenyewe maana inahusu hadi kuboresha sekta ya afya na Lishe moja kwa moja.Lakini pia niliwahi msikia kwamba ataitumia gesi na madini mengine kuwa dhamana ya kupata pesa za kugharamia bima ya afya kwa wote.Ilitakiwa aifafanue kwa utaratibu huu

Alizungumzia hoja ya kuweka ukanda huru wa biashara hasa kwa mikoa hii ya mpakani lakini, hii hoja hakuweza kuifafanua kwa lugha nyepesi ili watu wa kawaida waelewe,mathalani wanavyoweza kunufaika na biashara huria ya mipakani,angetolea mfano wa Tunduma ambako kilo moja ya sukari kutoka Zambia na Malawi ni sh.2000 wakati hiyi hiyo sukari hairuhusiwi kuuzwa huku Sumbwanga,kwa nini pale iuzwe na hapa ikatazwe wakati mkoa huu pia unashea mipaka na Zambia? Watu wangeelewa hoja ya ukanda huru wa biashara kwa mfano huo mwepesi ilhali sukari ya Tzn ni sh.3000-3200/= kwa mkoa huu,nk nk.Lakini pia alitakiwa atumie fursa hii kuinadi sera yake ya kuondoa utitiri wa kodi na kuwa na makisio makubwa ya kodi ili kuwapa fursa wananchi kujiajiri na kufurahia kulipa kodi .

Tatu kwa Mikoa hii ya Nyanda za Juu Kusini kuanzia Iringa,Njombe,Mbeya,Songwe na Rukwa shughuli kuu ni kilimo na biashara za kuvuka mipaka,lakini hakuweka ufafanuzi wa namna atakavyowainua wakulima ambapo kwa ukanda huu ilifaa azungumzie pembejeo na mambo ya masoko na shughuli za ugani,sasa alizungumzia kidogo akiwa Chitete Momba tena akiwalenga zaidi watu wa Momba wakati ilitakiwa iwe hoja kuu ukanda wote huu.Hapa ndipo angweza kueleza jinsi vikwazo na mageti yanayowekwa na serikali kuwanyonya wakulima,kupangiwa wanunuzi,kuzuiwa kuuza popote utakapopata soko na kusaidiwa pembejeo na kuwekewa bima za mazao bila kusahau pembejeo.

Kwa Iringa na Njombe angweza kuelezea jinsi ambavyo wafanyabiashara wa misitu na mazao yake wanavyolialia kwa tozo zaidi ya 20 maana waliwahi Mwambia rais alipokuwa ziarani Njombe sasa yeye angecapitalize hizi kero na kuahidi kuzifuta na pia angeeleza jinsi mahusiano mabaya kati ya Tzn na Kenya yalivyowaathiri wakulima wa miti na horticulture maana soko lao kubwa ni Kenya.

Nne watu wa CHADEMA hawako makini au hawana taarifa sahihi za mabo ya kiuchumi maana huwezi kuwa unasema miradi ya reli haina tija kwa sasa(maendleo ya vitu) at the sama time unaahidi kujenga reli kati ya Mpanda-Sumbawanga-Tunduma.Huku ukisema ccm wameua reli ya Tabora-Kaliua-Mpanda wakati iko hai na inafanya kazi,huku ni kujichanganya na kukosa umakini na taarifa sahihi. Kwanz sina hakika kama reli hii anayoahidi TL ni economically viable maana ukanda huu hauna mzigo mkubw kihivyo kiasi cha kuhitaji reli,pili ukanda huu una mipaka mingi na nchi jirani trade liberalization tu ndio inafaa na kuwawezesha watu kuzifikia nchi hizo jirani.

Mwisho Watu wa CDM hawana watu makini wanaoweza kuchambua takwimu za serikali,sera nk nk kama walivyo akina Zito,Lipumba,Bashe nk ,ni rai yangu watafute au wa recruit watu wenye talent za uchambuzi watawasaidia sana kuweza kuchambua sera na takwimu za serikali na kuzihusianisha na maisha ya watu,akina ZZK wa ACT WAZALENDO waliweza kuonesha kwa kuichambua ilani ya ccm na utekelezaji wake na kuhitimisha kwamba ccm imetekeleza 31% tu ya ilani yake.Pili inatakiwa kabla ya mgombea wao kuhutubia wahakikishe wanatafuta kero stahiki za watu wa eneo husika ili zitumike kukoleza kwenye sera zao mama.

All in all kampeni ya jana kwa Mkoa wa Rukwa naona ilifanikiwa maana sio jambo la kawaida kwa watu wa mkoa huu kugeukia upinzani ghafla pengine ni kutokana na kupata wahamiaji wengi wa mikoa ya jirani kama Iringa,Mbeya na Songwe ambao wamewaambukiza tabia za kutoburuzwa na kudanganywa na ccm.Karibuni kwa michango.
Mkuu usihangaike kujua labda mipango ya Chama inafeli, siyo kweli!

Ukweli ni kwamba, kunatofauti kubwa Kati ya ilani ya Chadema na mapendekezo binafsi ya mgombea Uraisi wa Chama hicho

Nimejifunza mengi Sana kulingana na anayoyanadi mgombea Uraisi na Ilani ya Chama chake, nimekuja kugundua kuwa, Ilani ya Chama na anayoyanadi mh ni vitu viwili tofauti Kabisa, nahisi mgombea Kwa sababu pengine hakushiriki katika uandaaji wa Ilani ya Chama chake na hivyo ameamua kuipuuza

Kwa sababu Mimi nachojua, Ili ufanye kitu kinachoanza ni Ile mipango ya ufanikishaji wa mipango, Namsikiliza mgombea wa Urais wa Ccm, kila atakachokisema kipo kwenye Sera ya ilani Yao,

Tofauti na mwenzake wa Chadema, Unajua, unaweza kujikuta unacheka badala ya kuwaonea huruma wanaomshabikia eti kwamba ndiye tumfanye kuwa Raisi wetu

Natoa mfano mdogo tu wa Yale anayoyahuburi kuyafanya ambayo mengi Hayako kwenye ilani Yao,

Akifika mahali, na Kwa kuwa Ili ufike unakoenda kufanyia Kampeni utapita kwenye maeneo ambayo ki ukweli yanachangamoto Lau ya barabara, au ni maji au njia ya leri, sasa huyu mh, akiyaona hayo NDIYO inakuwa ajenda ya Yeye atafanya, lakini ilani imeyasema hayo?

Utasikia akisema, Mnaonaje wananchi, tukitengeneneza hapa kuwa ndio soko la Kimataifa, tukajenga viwanda vitakavyohudumia nchi jiarani zote na bidhaa zote zikawa zinspatikana hapa na zitakuwa zikitoka haahapa na kuzisambaza kwenye nji zooote zinazopakana nasi?? Wananchi oyoooooo!!!😂

Sasa swali la Kwanza, He bidhaa zitakazokuwa zinazalishwa Dar, Moro, Tanga na kwingineko haziwezi kuuuzwa nje ya nchi ispokuwa za eneo Hilo pekee?

Jingine, Kwanini ahadi zake ziwe ni za kufikirika? Unapokuja kuwauliza wananchi eti Mnaonaje wananchi hapa tukifanya hiki na kile, Je vitu Hivi vinaendana na mpango mkakati wa Chama Chao? Au zilongwa mbali zitendwa mbali,?

Kuhusu Bima ya Afya Kwa watu wote kuisahau kuinadi, Kwanza nahisi sio agenda ya Chama Kwa ujmla na pengine hata Yeye anapata shida kuielezea kwamba atatumia Mbinu ipi kufanikisha hili, udhaifu wa ahadi yake hii ni, pale anapozungumzia Yeye alipata Bima hizo kule Ubeligiji na kusifia nchi hiyo kuwawezesha watu wake kila mmoja kuwa na hiyo Bima asiweze kutwambia walitumia mfumo upi kufanikisha Bima hizo na ilimgharimu mwananchi Kwa kiasi gani huko? Je Sisi itatugharimu Kwa kiasi kipi ukilinganisha na Hali ya nchi yetu? Na kitu kingine, ukiona anakuwa msahaulifu Sana katika kunadi kile ambacho kitawafanya wanchi wakipende na ndio sababu ya hata Yeye achaguliwe na wananchi, basi ujue pia mambo yote anayoyanadi yanatoka mdomoni Tu na sio moyoni mkuu!!!

Na Kwa nini Bima hiyo mwenye kuiongelea ni Yeye pekee kwenye Chama na si mwingine yeyote? Hii inamana kwamba, hata hao viongozi wengine na wanachadema hawajaielewa

Kama sio hivyo, basi kunashida mahali kichwani kwake!! Akili zimeyumba

Chadema, tunaomba kila ahahadi zenu zitokane na Sera na Ilani yenu kuyathibitisha hayo, la sivyo huo ni uwongo
 
Chadema hamna kitu pale. Afadhali ulivyowapa makavu.
Sijawapa makavu nawapa njia Bora za kuboredha kampeni zao,huko chama Cha mbogamboga ni Kama kanisani kila kitu ni ndio mzee,by the way Mimi ni mpikakura wa Upinzani na nikilinganisha kampeni ya Lowasa na hii ya Tundu,hii iko Bora zaidi
 
Back
Top Bottom