Uchaguzi 2020 Nilichoshuhudia kwenye kampeni za Tundu Lissu Sumbawanga, CHADEMA inafeli kwenye mikakati

Uchaguzi 2020 Nilichoshuhudia kwenye kampeni za Tundu Lissu Sumbawanga, CHADEMA inafeli kwenye mikakati

Habarini wapiga kura wenzangu.

Jana nilipata fursa ya kuhudhuria mkutano wa Kampeni wa mgombea wa CHADEMA ndugu Tundu Lissu, kiukweli watu walijitokeza wengi sana kumlaki na walionesha ushirikiano kwa kumsindikiza kwa maandamano hadi hotelini kwake hiyo ni mida ya saa mbili usiku, polisi walijaribu kuwazuia bila mafanikio.

Wakati anaanza kujinadi alianza vizuri kwa utangulizi lakini kadiri mda ulivyoenda sikuona akinadi na kuwakumbusha sera yake kuu ya bima ya afya kwa wote na kui-connect na hali za maisha ya watu halikadharika jinsi hiyo sera ya bima ya afya ilivyomsaidia hata yeye kupona huko Ulaya, maana kiukweli ukiwatazama watu wengi walikuwa na nyuso za huruma na machozi kwamba hawaamini huyu bwana alipona kutokana na shambulio lake.

Sera ya bima ya afya, uhuru na maendeleo ya watu anatakiwa atembee nazo kila anapokwenda na ainadi tena kwa kutumia mfano wake mwenyewe maana inahusu hadi kuboresha sekta ya afya na Lishe moja kwa moja. Lakini pia niliwahi msikia kwamba ataitumia gesi na madini mengine kuwa dhamana ya kupata pesa za kugharamia bima ya afya kwa wote. Ilitakiwa aifafanue kwa utaratibu huu.

Alizungumzia hoja ya kuweka ukanda huru wa biashara hasa kwa mikoa hii ya mpakani lakini, hii hoja hakuweza kuifafanua kwa lugha nyepesi ili watu wa kawaida waelewe,mathalani wanavyoweza kunufaika na biashara huria ya mipakani,angetolea mfano wa Tunduma ambako kilo moja ya sukari kutoka Zambia na Malawi ni sh.2000 wakati hiyi hiyo sukari hairuhusiwi kuuzwa huku Sumbwanga,kwa nini pale iuzwe na hapa ikatazwe wakati mkoa huu pia unashea mipaka na Zambia?

Watu wangeelewa hoja ya ukanda huru wa biashara kwa mfano huo mwepesi ilhali sukari ya Tzn ni sh. 3000-3200/= kwa mkoa huu, nk nk. Lakini pia alitakiwa atumie fursa hii kuinadi sera yake ya kuondoa utitiri wa kodi na kuwa na makisio makubwa ya kodi ili kuwapa fursa wananchi kujiajiri na kufurahia kulipa kodi .

Tatu kwa Mikoa hii ya Nyanda za Juu Kusini kuanzia Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe na Rukwa shughuli kuu ni kilimo na biashara za kuvuka mipaka lakini hakuweka ufafanuzi wa namna atakavyowainua wakulima ambapo kwa ukanda huu ilifaa azungumzie pembejeo na mambo ya masoko na shughuli za ugani, sasa alizungumzia kidogo akiwa Chitete Momba tena akiwalenga zaidi watu wa Momba wakati ilitakiwa iwe hoja kuu ukanda wote huu.

Hapa ndipo angweza kueleza jinsi vikwazo na mageti yanayowekwa na serikali kuwanyonya wakulima, kupangiwa wanunuzi,kuzuiwa kuuza popote utakapopata soko na kusaidiwa pembejeo na kuwekewa bima za mazao bila kusahau pembejeo.

Kwa Iringa na Njombe angweza kuelezea jinsi ambavyo wafanyabiashara wa misitu na mazao yake wanavyolialia kwa tozo zaidi ya 20 maana waliwahi Mwambia rais alipokuwa ziarani Njombe sasa yeye ange-capitalize hizi kero na kuahidi kuzifuta na pia angeeleza jinsi mahusiano mabaya kati ya Tzn na Kenya yalivyowaathiri wakulima wa miti na horticulture maana soko lao kubwa ni Kenya.

Nne watu wa CHADEMA hawako makini au hawana taarifa sahihi za mabo ya kiuchumi maana huwezi kuwa unasema miradi ya reli haina tija kwa sasa(maendleo ya vitu) at the sama time unaahidi kujenga reli kati ya Mpanda-Sumbawanga-Tunduma. Huku ukisema CCM wameua reli ya Tabora-Kaliua-Mpanda wakati iko hai na inafanya kazi, huku ni kujichanganya na kukosa umakini na taarifa sahihi.

Kwanza sina hakika kama reli hii anayoahidi TL ni economically viable maana ukanda huu hauna mzigo mkubw kihivyo kiasi cha kuhitaji reli, pili ukanda huu una mipaka mingi na nchi jirani trade liberalization tu ndio inafaa na kuwawezesha watu kuzifikia nchi hizo jirani.

Mwisho Watu wa CDM hawana watu makini wanaoweza kuchambua takwimu za serikali, sera nk nk kama walivyo akina Zito, Lipumba, Bashe nk ,ni rai yangu watafute au wa-recruit watu wenye talent za uchambuzi watawasaidia sana kuweza kuchambua sera na takwimu za serikali na kuzihusianisha na maisha ya watu, akina ZZK wa ACT WAZALENDO waliweza kuonesha kwa kuichambua ilani ya CCM na utekelezaji wake na kuhitimisha kwamba CCM imetekeleza 31% tu ya ilani yake. Pili inatakiwa kabla ya mgombea wao kuhutubia wahakikishe wanatafuta kero stahiki za watu wa eneo husika ili zitumike kukoleza kwenye sera zao mama.

All in all kampeni ya jana kwa Mkoa wa Rukwa naona ilifanikiwa maana sio jambo la kawaida kwa watu wa mkoa huu kugeukia upinzani ghafla pengine ni kutokana na kupata wahamiaji wengi wa mikoa ya jirani kama Iringa, Mbeya na Songwe ambao wamewaambukiza tabia za kutoburuzwa na kudanganywa na CCM.

Karibuni kwa michango.
Wazingatie Ushauri ili wafanikiwe, Wakiendelea na Kampeni za kuipigia kampeni NEC na Majibizano kwa wagombea wengine, wataishia kunawa tu. Wao wawaambie wananchi wa kila ukanda watawafanyia nini, wakipewa ridhaa
 
Mleta mada!!!
Mambo mengi uliyoyasema ndugu Tundu Antiphas Lissu ameyaelezea Vizuri kwenye kampeni zake. Alipokuwa njombe mjini na hata makambako na mufindi, nilifanikiwa kuangalia live kampeni zake , aliongelea vizuri tozo za zao la mbao na alisema wao watafanyaje

Alipokuwa mbeya na Songwe amesema vizuri sana juu ya Kuip a kipaumbele mikoa ya Nyanda za juu kusini, aliongelea Uhuru wa watu kuuza mazao yao sehemu wanazoona zinabei nzuri, alisema kuhusu kuifanya kanda ile kuwa sehemu kuu ya biashara kwa nchi yetu na nchi za sadc.

Inabidi ufahamu kuwa mgombea kwa siku anafanya mikutano rasmi 4 maeneo tofauti na pia anafanya mikutano mingine isiyo rasmi mingi akiwa njiani. Kwa sababu muda ni mchache ni ngumu sana kwa yeye kuelezea kila kitu in detail kwa sababu ya muda.

Hii ndo mana mgombea wa Chadema anahamasisha sana kuwe na midahalo kwa sababu kwenye mdahalo ndo mgombea anaeleza in detail Sera zake
 
Ushauri ni kitu kizuri, na wahusika wataamua kama wachukue kipi, waache kipi! Nafikiri wagombea wa ubunge na udiwani, wafanye research ya eneo analokwenda mgombea Urais , kabla TAL hajasimama, wao waeleze kero za jimbo, afu TAL azijibu kwenye hotuba yake!
 
..ushauri wako ni mzuri.

..ilitakiwa watu walioko majimboni ndio wampe mgombea pointi za kuongea.

..mambo mengi uliyoshauri yangewezekana kama wasomi wazuri wangekuwa na uhuru wa kujiunga na vyama vya upinzani.

..tulifika mahali wananchi wamekuwa na uoga kushiriki ktk shughuli za wapinzani, au kuonyesha mapenzi kwa chama hicho.

..ukiwauliza cdm insiders kuhusu masuala haya uliyoibua majibu yao ni kwamba milango ya Chadema iko wazi, na wako tayari kupokea ushauri, tatizo wananchi wanaogopa misukosuko toka kwa wenye dola.
Nimezisikia kampeni za Lissu za Leo Kirando Nkasi, Majimoto Kavuu na Mpanda, zimefuata ushauri wa mleta mada 100%. Wagombea wa majimbo husika wamesimama wakatoa kero za majimbo yao kisha zikafafanuliwa na mgombea Urais. Nkasi wamejibiwa CHADEMA watakavyofanya ili wavuvi wasichomewe nyavu, wakulima wapewe soko huria la mazao yao, Kavuu wameambiwa hakuna ng'ombe wa mfugaji atakayetaofishwa na serikali kwa kuingia kwenye hifadhi kwa bahati Mbaya, Mpanda wamehakikishiwa soko huria la Tumbaku na Asali.
 
Habarini wapiga kura wenzangu.

Jana nilipata fursa ya kuhudhuria mkutano wa Kampeni wa mgombea wa CHADEMA ndugu Tundu Lissu, kiukweli watu walijitokeza wengi sana kumlaki na walionesha ushirikiano kwa kumsindikiza kwa maandamano hadi hotelini kwake hiyo ni mida ya saa mbili usiku, polisi walijaribu kuwazuia bila mafanikio.

Wakati anaanza kujinadi alianza vizuri kwa utangulizi lakini kadiri mda ulivyoenda sikuona akinadi na kuwakumbusha sera yake kuu ya bima ya afya kwa wote na kui-connect na hali za maisha ya watu halikadharika jinsi hiyo sera ya bima ya afya ilivyomsaidia hata yeye kupona huko Ulaya, maana kiukweli ukiwatazama watu wengi walikuwa na nyuso za huruma na machozi kwamba hawaamini huyu bwana alipona kutokana na shambulio lake.

Sera ya bima ya afya, uhuru na maendeleo ya watu anatakiwa atembee nazo kila anapokwenda na ainadi tena kwa kutumia mfano wake mwenyewe maana inahusu hadi kuboresha sekta ya afya na Lishe moja kwa moja. Lakini pia niliwahi msikia kwamba ataitumia gesi na madini mengine kuwa dhamana ya kupata pesa za kugharamia bima ya afya kwa wote. Ilitakiwa aifafanue kwa utaratibu huu.

Alizungumzia hoja ya kuweka ukanda huru wa biashara hasa kwa mikoa hii ya mpakani lakini, hii hoja hakuweza kuifafanua kwa lugha nyepesi ili watu wa kawaida waelewe,mathalani wanavyoweza kunufaika na biashara huria ya mipakani,angetolea mfano wa Tunduma ambako kilo moja ya sukari kutoka Zambia na Malawi ni sh.2000 wakati hiyi hiyo sukari hairuhusiwi kuuzwa huku Sumbwanga,kwa nini pale iuzwe na hapa ikatazwe wakati mkoa huu pia unashea mipaka na Zambia?

Watu wangeelewa hoja ya ukanda huru wa biashara kwa mfano huo mwepesi ilhali sukari ya Tzn ni sh. 3000-3200/= kwa mkoa huu, nk nk. Lakini pia alitakiwa atumie fursa hii kuinadi sera yake ya kuondoa utitiri wa kodi na kuwa na makisio makubwa ya kodi ili kuwapa fursa wananchi kujiajiri na kufurahia kulipa kodi .

Tatu kwa Mikoa hii ya Nyanda za Juu Kusini kuanzia Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe na Rukwa shughuli kuu ni kilimo na biashara za kuvuka mipaka lakini hakuweka ufafanuzi wa namna atakavyowainua wakulima ambapo kwa ukanda huu ilifaa azungumzie pembejeo na mambo ya masoko na shughuli za ugani, sasa alizungumzia kidogo akiwa Chitete Momba tena akiwalenga zaidi watu wa Momba wakati ilitakiwa iwe hoja kuu ukanda wote huu.

Hapa ndipo angweza kueleza jinsi vikwazo na mageti yanayowekwa na serikali kuwanyonya wakulima, kupangiwa wanunuzi,kuzuiwa kuuza popote utakapopata soko na kusaidiwa pembejeo na kuwekewa bima za mazao bila kusahau pembejeo.

Kwa Iringa na Njombe angweza kuelezea jinsi ambavyo wafanyabiashara wa misitu na mazao yake wanavyolialia kwa tozo zaidi ya 20 maana waliwahi Mwambia rais alipokuwa ziarani Njombe sasa yeye ange-capitalize hizi kero na kuahidi kuzifuta na pia angeeleza jinsi mahusiano mabaya kati ya Tzn na Kenya yalivyowaathiri wakulima wa miti na horticulture maana soko lao kubwa ni Kenya.

Nne watu wa CHADEMA hawako makini au hawana taarifa sahihi za mabo ya kiuchumi maana huwezi kuwa unasema miradi ya reli haina tija kwa sasa(maendleo ya vitu) at the sama time unaahidi kujenga reli kati ya Mpanda-Sumbawanga-Tunduma. Huku ukisema CCM wameua reli ya Tabora-Kaliua-Mpanda wakati iko hai na inafanya kazi, huku ni kujichanganya na kukosa umakini na taarifa sahihi.

Kwanza sina hakika kama reli hii anayoahidi TL ni economically viable maana ukanda huu hauna mzigo mkubw kihivyo kiasi cha kuhitaji reli, pili ukanda huu una mipaka mingi na nchi jirani trade liberalization tu ndio inafaa na kuwawezesha watu kuzifikia nchi hizo jirani.

Mwisho Watu wa CDM hawana watu makini wanaoweza kuchambua takwimu za serikali, sera nk nk kama walivyo akina Zito, Lipumba, Bashe nk ,ni rai yangu watafute au wa-recruit watu wenye talent za uchambuzi watawasaidia sana kuweza kuchambua sera na takwimu za serikali na kuzihusianisha na maisha ya watu, akina ZZK wa ACT WAZALENDO waliweza kuonesha kwa kuichambua ilani ya CCM na utekelezaji wake na kuhitimisha kwamba CCM imetekeleza 31% tu ya ilani yake. Pili inatakiwa kabla ya mgombea wao kuhutubia wahakikishe wanatafuta kero stahiki za watu wa eneo husika ili zitumike kukoleza kwenye sera zao mama.

All in all kampeni ya jana kwa Mkoa wa Rukwa naona ilifanikiwa maana sio jambo la kawaida kwa watu wa mkoa huu kugeukia upinzani ghafla pengine ni kutokana na kupata wahamiaji wengi wa mikoa ya jirani kama Iringa, Mbeya na Songwe ambao wamewaambukiza tabia za kutoburuzwa na kudanganywa na CCM.

Karibuni kwa michango.
Mleta mada nafikiri wewe ni neutral, hupelekwi na uvyama - Kwa nini nasema hivyo: umemrekebisha Mgombea wa CHADEMA at the same time umewapa point za kuegemea CCM watakapoenda kukampaini mikoa hiyo.
Very good
 
Nimezisikia kampeni za Lissu za Leo Kirando Nkasi, Majimoto Kavuu na Mpanda, zimefuata ushauri wa mleta mada 100%. Wagombea wa majimbo husika wamesimama wakatoa kero za majimbo yao kisha zikafafanuliwa na mgombea Urais. Nkasi wamejibiwa CHADEMA watakavyofanya ili wavuvi wasichomewe nyavu, wakulima wapewe soko huria la mazao yao, Kavuu wameambiwa hakuna ng'ombe wa mfugaji atakayetaofishwa na serikali kwa kuingia kwenye hifadhi kwa bahati Mbaya, Mpanda wamehakikishiwa soko huria la Tumbaku na Asali.
Na kaifafanua vizuri sera ya Majimbo akiwa Mpanda Mjini simply kabisa
 
Lissu anajitahidi sana hasa ukizingatia mazingira magumu ya upinzani chini ya serekali ya awamu ya tano.
 
Lissu anajitahidi sana hasa ukizingatia mazingira magumu ya upinzani chini ya serekali ya awamu ya tano.
Kibaya zaidi hawa mbuzi jike wa kijani wamewabana wapinzani kwenye kutafuta vyanzo vya pesa ili kuendesha kampeni wakati wao wanafursa ya kutumia hata pesa za umma kimagumashi maana tunawaona wanakuja maofisi wanapewa mafuta nk maana hawa wakuu wa taasisi ni wanachama wao.
 
Ni punguani tu ndie atakae shindwa kumwelewa Lissu narudia ni punguani

Sent from my BLL-L22 using JamiiForums mobile app

Mkuu yawezekana tuko mapungwani wengi mnoo, kwa kuwa Chadema ni chana kina jiita ni cha wasomi, uchambuzi wa kinachofanywa na Chadema ni vizuri utumie HYPOTHESIS ANALYSIS/ SYNTHESIS ANALYSIS kwa kila hatua.

Kila wakifanyacho kina kataa katika analysis hii, yeyote mwenye uwezo wa kutumia analysis hii ajaribu halafu atufahamishe.

Mwanasiasa mzuri ni sawasawa na Mwl yeyote mzuri :
- - jee unaweza ku connect na ama wafuasi wako?
- - jee unaweza ku connect na wanafunzi wako?

Unapotuma ujumbe kwa watu wako jee unashuhudia mzuka ?

Sio lazima uwe na elimu kubwa sana kuweza kufikisha ujumbe na ukawapa mzuka iwe wanafunzi au washabiki wako.

Na baada ya kutoa ujumbe , ukawapandisha mzuka, wataenda kulala huku wakiendelea kuamini ujumbe uliotamka kwa muda mrefu ?.

Kwa hiyo Kufanya au kutofanya vizuri kwa Tundu Lissu kutathibitishwa tarehe 29/10/2020.
 
Habarini wapiga kura wenzangu.

Jana nilipata fursa ya kuhudhuria mkutano wa Kampeni wa mgombea wa CHADEMA ndugu Tundu Lissu, kiukweli watu walijitokeza wengi sana kumlaki na walionesha ushirikiano kwa kumsindikiza kwa maandamano hadi hotelini kwake hiyo ni mida ya saa mbili usiku, polisi walijaribu kuwazuia bila mafanikio.

Wakati anaanza kujinadi alianza vizuri kwa utangulizi lakini kadiri mda ulivyoenda sikuona akinadi na kuwakumbusha sera yake kuu ya bima ya afya kwa wote na kui-connect na hali za maisha ya watu halikadharika jinsi hiyo sera ya bima ya afya ilivyomsaidia hata yeye kupona huko Ulaya, maana kiukweli ukiwatazama watu wengi walikuwa na nyuso za huruma na machozi kwamba hawaamini huyu bwana alipona kutokana na shambulio lake.

Sera ya bima ya afya, uhuru na maendeleo ya watu anatakiwa atembee nazo kila anapokwenda na ainadi tena kwa kutumia mfano wake mwenyewe maana inahusu hadi kuboresha sekta ya afya na Lishe moja kwa moja. Lakini pia niliwahi msikia kwamba ataitumia gesi na madini mengine kuwa dhamana ya kupata pesa za kugharamia bima ya afya kwa wote. Ilitakiwa aifafanue kwa utaratibu huu.

Alizungumzia hoja ya kuweka ukanda huru wa biashara hasa kwa mikoa hii ya mpakani lakini, hii hoja hakuweza kuifafanua kwa lugha nyepesi ili watu wa kawaida waelewe,mathalani wanavyoweza kunufaika na biashara huria ya mipakani,angetolea mfano wa Tunduma ambako kilo moja ya sukari kutoka Zambia na Malawi ni sh.2000 wakati hiyi hiyo sukari hairuhusiwi kuuzwa huku Sumbwanga,kwa nini pale iuzwe na hapa ikatazwe wakati mkoa huu pia unashea mipaka na Zambia?

Watu wangeelewa hoja ya ukanda huru wa biashara kwa mfano huo mwepesi ilhali sukari ya Tzn ni sh. 3000-3200/= kwa mkoa huu, nk nk. Lakini pia alitakiwa atumie fursa hii kuinadi sera yake ya kuondoa utitiri wa kodi na kuwa na makisio makubwa ya kodi ili kuwapa fursa wananchi kujiajiri na kufurahia kulipa kodi .

Tatu kwa Mikoa hii ya Nyanda za Juu Kusini kuanzia Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe na Rukwa shughuli kuu ni kilimo na biashara za kuvuka mipaka lakini hakuweka ufafanuzi wa namna atakavyowainua wakulima ambapo kwa ukanda huu ilifaa azungumzie pembejeo na mambo ya masoko na shughuli za ugani, sasa alizungumzia kidogo akiwa Chitete Momba tena akiwalenga zaidi watu wa Momba wakati ilitakiwa iwe hoja kuu ukanda wote huu.

Hapa ndipo angweza kueleza jinsi vikwazo na mageti yanayowekwa na serikali kuwanyonya wakulima, kupangiwa wanunuzi,kuzuiwa kuuza popote utakapopata soko na kusaidiwa pembejeo na kuwekewa bima za mazao bila kusahau pembejeo.

Kwa Iringa na Njombe angweza kuelezea jinsi ambavyo wafanyabiashara wa misitu na mazao yake wanavyolialia kwa tozo zaidi ya 20 maana waliwahi Mwambia rais alipokuwa ziarani Njombe sasa yeye ange-capitalize hizi kero na kuahidi kuzifuta na pia angeeleza jinsi mahusiano mabaya kati ya Tzn na Kenya yalivyowaathiri wakulima wa miti na horticulture maana soko lao kubwa ni Kenya.

Nne watu wa CHADEMA hawako makini au hawana taarifa sahihi za mabo ya kiuchumi maana huwezi kuwa unasema miradi ya reli haina tija kwa sasa(maendleo ya vitu) at the sama time unaahidi kujenga reli kati ya Mpanda-Sumbawanga-Tunduma. Huku ukisema CCM wameua reli ya Tabora-Kaliua-Mpanda wakati iko hai na inafanya kazi, huku ni kujichanganya na kukosa umakini na taarifa sahihi.

Kwanza sina hakika kama reli hii anayoahidi TL ni economically viable maana ukanda huu hauna mzigo mkubw kihivyo kiasi cha kuhitaji reli, pili ukanda huu una mipaka mingi na nchi jirani trade liberalization tu ndio inafaa na kuwawezesha watu kuzifikia nchi hizo jirani.

Mwisho Watu wa CDM hawana watu makini wanaoweza kuchambua takwimu za serikali, sera nk nk kama walivyo akina Zito, Lipumba, Bashe nk ,ni rai yangu watafute au wa-recruit watu wenye talent za uchambuzi watawasaidia sana kuweza kuchambua sera na takwimu za serikali na kuzihusianisha na maisha ya watu, akina ZZK wa ACT WAZALENDO waliweza kuonesha kwa kuichambua ilani ya CCM na utekelezaji wake na kuhitimisha kwamba CCM imetekeleza 31% tu ya ilani yake. Pili inatakiwa kabla ya mgombea wao kuhutubia wahakikishe wanatafuta kero stahiki za watu wa eneo husika ili zitumike kukoleza kwenye sera zao mama.

All in all kampeni ya jana kwa Mkoa wa Rukwa naona ilifanikiwa maana sio jambo la kawaida kwa watu wa mkoa huu kugeukia upinzani ghafla pengine ni kutokana na kupata wahamiaji wengi wa mikoa ya jirani kama Iringa, Mbeya na Songwe ambao wamewaambukiza tabia za kutoburuzwa na kudanganywa na CCM.

Karibuni kwa michango.
Sera ya majimbo imewagusa sana watu mikoani
 
Sera ya majimbo imewagusa sana watu mikoani
Hii ni kiboko ya wapuuzi wanotumia pesa hovyo kwa kujipendelea kwao au kutumia pesa vibaya kama kufanya biashara za kununua wapinzani,kuhonga ,kugawakkawa pesa za umma hovyo au kuwanyima wengine maendeleo kwa kisingizio cha sijui hawajamchagua nani kutoka mboga mboga huu ni upuuzi mkubwa maana kodi tutoe wote na rasilimali za maeneo yetu zivunwe lakini eti tunyimwe kisa pesa zoote ziko mfuko mkuu.
Sera hii itakomesha mambo ya sijui rais alete stend mara rais katua bilioni kadhaa stupid
 
Back
Top Bottom