Nilidanganywa kusoma PGM nitakuwa rubani, leo hii mpishi kwa Mhindi

Nilidanganywa kusoma PGM nitakuwa rubani, leo hii mpishi kwa Mhindi

Wakati nasoma A-level, Mkwawa High School (1999-2001) ulipita uvumi kuwa tunasoma PGM tunaandaliwa kuwa marubani lakini leo hii ninafanya kibarua kama mpishi kwa Mhindi Masaki.

Aisee elimu hii ovyo sana.

Ungeweka na kiwango chako cha ufaulu ingekuwa ni vizuri zaidi, kwa bila kujua ufaulu wako wa mtiahani wa mwisho wa form six, hii taarifa yako sio kamili na uwezekano wa kuptosha ni mkubwa kwa wasio na uelewa mzuri.
 
Hivi kwanini huwa husomi umetulia mtoto wa kisukuma? Unakurupuka tu! Nasema mwanafunzi akiwa serious na masomo hawezi kukosa kutimiza ndoto zake. Hakuna visingizio. Magenius wataonekana NECTA si vijiweni


Sijakurupuka hata kidgo..umesema mkianza kutoa K!nikakuanbia unejuaje mtoa mada ni ke?acha kukariri ww!..
 
Hata Tanzania Ones wapo mtaani wanasakata rhumba tuu, wala usiwaze.

Kinachomata ni pesa na sio kazi, wengi walio kwenye ajira rasmi hawana tofauti na wajasiriamali mkuu.


Kuna madogo wamesoma Alfa...Then wakaenda nje...ni wlaikia vichwa balaa ss hvi madalali wa mashamba!wasitutishe kbsaaaa!
Tutishane bank kwenye figures sio mavyeti!
 
binadamu tunamipango yetu na mungu ana mipango yake si kila unachotaka lazima kiwe, saa nyingine mungu anakupa kazi nyingine kukuepusha na majanga, pengine ungekuwa rubani ungedondoka na ndege kwenye msitu wa seloe
 
Siku hizi marubani ni waliosoma form four na kupata hata div four bila kujali kasoma nini kigezo uwe mtoto wa kishua, unaanza vikozi vidogo vidogo vya kuendesha chopa, unakwenda nairobi kidogo, unakwenda sauzi ukirudi unaanza vikampuni vidogo unapata uzoevu mwisho unaanza kuyarusha
 
Uliambiwa usome wewe ukacheza unafikiri nini? Lazima adhabu ya kutokusoma ikuandame. Ungalipata div one A physics, A maths ungeenda engineering tu. Angalia vyuo vya engineering vinavyohaha kutafuta wanafunzi. Rubani kwa taarifa yako ni dereva kama wa Passo ila yeye Passo yake inaruka angani.
Nenda kasome uone moto wake ndo utaelewa, msipende kutoa ufafanuzi kwa kitu hamkijui.
 
Sijakurupuka hata kidgo..umesema mkianza kutoa K!nikakuanbia unejuaje mtoa mada ni ke?acha kukariri ww!..
Kwenye comment yangu nilikuwa nakueleza wewe au unabisha wewe sie Ke? Uache kujifanya mjuaji. Ila unisamehe kama nawe uliangukia pua
 
Uliintergrate zero nini? Joke

Pole sana kwa kuukosa urubani Wa bombadia endelea kuwa rubani Wa msosi. Nami nilikuwa na ndoto kama zako japo sijaenda mbali sana Mimi ni rubani Wa kuku, bata na ndege wengine wafugwao..kutoka kutaka kuwa rubani Wa drimlaina mpaka rubani Wa Kuku nimehustle!
 
Back
Top Bottom