Nilidhani wanaokimbia madeni wanafanya kusudi

Wewe Ni mimi
 
Kuna mtu nilikuwa namdai, amenizungusha hadi nikawa namuona boonge la tapeli. Kumbe mambo yamemwendea mrama vibayaaa mbaya. Mwenye nyumba tu anamdai kodi ya zaidi ya mwaka, mara mke akajifungua tena kwa kisu. Hajakaa sawa si akapata ajali ya boda boda, akavunjika miguu yote miwili, akawekewa vyumaπŸ™†
Na shughuli zake ni mpkaa atoke akahangaike, mke ni mama wa nyumbani tu.

Kuna wakati mambo yanakuendea mrama hadi unahisi duninai uliletwa kuhangaika ili uwe wa mfano.
 
Hii dunia Ina Maumivu na WATU HAWANA HURUMA nazungumza haya nimetembea na elbow crutches nimebaguliwa nimenyanyapaliwa Ila for this nimekua strong than normal psychological being...
 
Uzi mzuri sana huu unatukumbusha kumtegemea mungu saa zote na kutufanya tuwe wakomavu zaidi bila ya kupitia changamoto huwezi kujifunza au kupiga hatua kwenye maisha, ingawa kuna watu hawana utu mara nyingi mtu akipitia changamoto huitwa majina mbali mbali ya kukera na kudhalilisha na hukimbiwa na marafiki, na wapo watakaofurahia na kuhadithiana shida zako ,kwakweli dunia haina huruma,mungu ndio rafiki wa kweli
 
Sina mkuu nikikukopesha jua ukilipa umelipa usipo lipa ni sadaka..

Sipendeleagi usumbufu
Mimi huwa sikopeshi hela ambayo itaniuma
Nikikupa afu 5 afu 10 usipolipa fresh naona sadaka unajua haya maisha ukiwa huna ndo unaelewa kuna muda unaishi huna hata mbuni mfukoni.. kwahiyo unaelewa tu juu kwa juu ila kudai aisee siwwezi
 
Mimi huwa sikopeshi hela ambayo itaniuma
Nikikupa afu 5 afu 10 usipolipa fresh naona sadaka unajua haya maisha ukiwa huna ndo unaelewa kuna muda unaishi huna hata mbuni mfukoni.. kwahiyo unaelewa tu juu kwa juu ila kudai aisee siwwezi
Kwel mkuu sisi ndio tunaishi principal za YESU..

KOPESHA BILA KUTAZAMIWAA KULIPWA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…