KERO Nilifungua account ya CRDB lakini nilikutana na mambo ya ajabu mpaka nikatelekeza account baada ya miaka 4

KERO Nilifungua account ya CRDB lakini nilikutana na mambo ya ajabu mpaka nikatelekeza account baada ya miaka 4

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Kelela

Senior Member
Joined
Nov 7, 2020
Posts
191
Reaction score
308
CRDB BANK:
Nilifungua account ya CRDB lakini nilikutana na mambo ya ajabu mpaka nikatelekeza account baada ya miaka 4.

Niliwahi kufanyia miamala ya kutoa pesa kwenye ATM za CRDB ndani ya mwaka mmoja tu baada ya hapo ikawa kila nikenda kutoa pesa ATM ya CRDB kadi inagoma inasema "This Card May not be used in This ATM".

Kwa kuwa ilikuwa ni MasterCard nikawa naenda kutolea pesa kwenye ATM ya NMB na ikawa inatoa pesa bila shida yoyote kwa takribani miaka miwili nilikuwa natumia ATM za NMB kutoa pesa na kadi yangu ya CRDB BANK.

Mwaka wa NNe nikahamia sehemu ambayo benki ya CRDB ipo karibu, Nikasema ngoja nikajaribu tena kutoa pesa kwenye ATM ya CRDB, alafu ilikuwa ni pesa ya dharura nayo na ilikuwa saa 1 1 alfajiri, ile kuingiza kadi tu, kadi ikamezwa (ikatumbukia moja kwa moja, haikurudi tena).

Nikakaa baada ya siku 2 nikaenda kwenye lile tawi kuomba kadi yangu, ndani nikakaa foleni takribani lisaa limoja na nusu ndio nikapewa kadi yangu.

Baada ya kupatiwa kadi na wakati huo nimechoka sana kwa kusubiri mule ndani Benki, Nikasema ngoja nipitie ATM nitoe pesa kidogo.


Kufika kwenye ATM nimeweka kadi tu, Kadi ikamezwa tena, aisee hasira nilizopata hapo nikaingia Simbanking nikahamisha pesa zooote. Tangu siku ile (ilikuwa mwaka 2020) mpaka leo sijaenda kuchukua kadi na wala sijaitumia tena account mpaka walipoamua kuifunga wenyewe.

Kuna mwengine aliwahi kupata changamoto kama hii au ni mimi tu?
 
CRDB BANK:
Nilifungua account ya CRDB lakini nilikutana na mambo ya ajabu mpaka nikatelekeza account baada ya miaka 4.

Niliwahi kufanyia miamala ya kutoa pesa kwenye ATM za CRDB ndani ya mwaka mmoja tu baada ya hapo ikawa kila nikenda kutoa pesa ATM ya CRDB kadi inagoma inasema "This Card May not be used in This ATM".

Kwa kuwa ilikuwa ni MasterCard nikawa naenda kutolea pesa kwenye ATM ya NMB na ikawa inatoa pesa bila shida yoyote kwa takribani miaka miwili nilikuwa natumia ATM za NMB kutoa pesa na kadi yangu ya CRDB BANK.

Mwaka NNe nikahamia sehemu ambayo benki ya CRDB ipo karibu, Nikasema ngoja nikajaribu tena kutoa pesa kwenye ATM ya CRDB, alafu ilikuwa ni pesa ya dharura nayo na ilikuwa saa 1 1 alfajiri, ile kuingiza kadi tu, kadi ikamwezwa (ikatumbukia moja kwa moja, haikurudi tena).

Nikakaa baada ya siku 2 nikaenda kwenye lile tawi kuomba kadi yangu, ndani nikakaa foleni takribani lisaa limoja na nusu ndio nikapewa kadi yangu.

Baada ya kupatiwa kadi na wakati huo nimechoka sana kwa kusubiri mule ndani Benki, Nikasema ngoja nipitie ATM nitoe pesa kidogo.


Kufika kwenye ATM nimeweka kadi tu, Kadi ikamezwa tena, aisee hasira nilizopata hapo nikaingia Simbanking nikahamisha pesa zooote. Tangu siku ile (ilikuwa mwaka 2020) mapaka leo sijaenda kuchukua kadi na wala sijaitumia tena account mpaka walipoamua kuifunga wenyewe.

Kuna mwengine aliwahi kupata changamoto kama hii au ni mimi tu?
Nilikutana na changamoto kama hiyo Exim Bank, huo ndo ulikuwa mwisho wa ushirika wetu.
 
Kufika kwenye ATM nimeweka kadi tu, Kadi ikamezwa tena, aisee hasira nilizopata hapo nikaingia Simbanking nikahamisha pesa zooote. Tangu siku ile (ilikuwa mwaka 2020) mapaka leo sijaenda kuchukua kadi na wala sijaitumia tena account mpaka walipoamua kuifunga wenyewe.
Kingine ambacho hukufuatilia/ haukugundua: Ni makato makubwa pindi utoapo fedha kwa kadi ya benki tofauti katika ATM ya benki nyingine. Kama ulivyokuwa ukifanya unatumia atm za NMB badala ya CRDB. Hasara yake ni kubwa sana.
 
CRDB wamekaa kimchongo sana kama MOD wa JF tu..Nimeomba mastercard huu ni mwezi sasa eti bado inatengezwa utafkiri ni reli ya SGR
 
CRDB BANK:
Nilifungua account ya CRDB lakini nilikutana na mambo ya ajabu mpaka nikatelekeza account baada ya miaka 4.

Niliwahi kufanyia miamala ya kutoa pesa kwenye ATM za CRDB ndani ya mwaka mmoja tu baada ya hapo ikawa kila nikenda kutoa pesa ATM ya CRDB kadi inagoma inasema "This Card May not be used in This ATM".

Kwa kuwa ilikuwa ni MasterCard nikawa naenda kutolea pesa kwenye ATM ya NMB na ikawa inatoa pesa bila shida yoyote kwa takribani miaka miwili nilikuwa natumia ATM za NMB kutoa pesa na kadi yangu ya CRDB BANK.

Mwaka wa NNe nikahamia sehemu ambayo benki ya CRDB ipo karibu, Nikasema ngoja nikajaribu tena kutoa pesa kwenye ATM ya CRDB, alafu ilikuwa ni pesa ya dharura nayo na ilikuwa saa 1 1 alfajiri, ile kuingiza kadi tu, kadi ikamezwa (ikatumbukia moja kwa moja, haikurudi tena).

Nikakaa baada ya siku 2 nikaenda kwenye lile tawi kuomba kadi yangu, ndani nikakaa foleni takribani lisaa limoja na nusu ndio nikapewa kadi yangu.

Baada ya kupatiwa kadi na wakati huo nimechoka sana kwa kusubiri mule ndani Benki, Nikasema ngoja nipitie ATM nitoe pesa kidogo.


Kufika kwenye ATM nimeweka kadi tu, Kadi ikamezwa tena, aisee hasira nilizopata hapo nikaingia Simbanking nikahamisha pesa zooote. Tangu siku ile (ilikuwa mwaka 2020) mpaka leo sijaenda kuchukua kadi na wala sijaitumia tena account mpaka walipoamua kuifunga wenyewe.

Kuna mwengine aliwahi kupata changamoto kama hii au ni mimi tu?

Wewe jamaa una visa, mi pia kadi ilikuwa na shida hiyo. Nikatengeneza kadi nyingine.
 
Mimi kadi ilimezwa nikiwa safarini tena holiday nikaambiwa nifuatilie kwenye tawi napoelekea, wakanizungusha nikavumilia hadi nikaipata.

Mwaka juzi mtu anataka tufanye biashara pesa ndefu anafanya muamala ikagoma zaidi ya mara 5, nikaonekana mbabaishaji, akaabort mchongo nikakosa hela. Kuwapigia wanadai hakuna shida, nilikereka na kuanzia hapo nikawahama.
 
Mama wa kiarabu alini cut off wakati nasubiri jamaa amalize dirishani.

Nikamuuliza kulikoni akasema yeye ameitwa na teller.

Wakati tunabishana, SUMA akaja alaniuliza tatizo lako ni lipi? Nikawaambia, akasema nihame dirisha nikaanze upya.
Nikakataa, teller akaniita nikafanya muamala.

Wakati naondoka, yule mama aka cut off mbele ya jamaa, akakausha, nikawaambia huwezi kufanya hovyo.
SUMA akaniambia niondoke.

Sitaenda benki ya CDDB tena maishani mwangu. Na fedha zangu nitazukomba online.

Tawi ni la Temeke Stereo, last week.
Pia Wana kinda chembamba kinavaa ushungi, upo dirishani kina cut off na kupitisha forms zimejazwa n hela na vimemo.
Benki hovyo, tawi la hovyo kazi kuwakandamiza watu weusi.
Racism Tanzania IPO Benki. Tena ya wazi kabisa nimeshuhudia Mara nyingi.
 
Back
Top Bottom