Niliingia kwenye mahusiano na binti wa miaka 19

Niliingia kwenye mahusiano na binti wa miaka 19

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2018
Posts
2,754
Reaction score
4,975
Habari zenu wakuu,

Nimekuwa na mahusiano na binti mmoja,Ambaye tulikutana akiwa na miaka 18 nikiwa nimemzidi miaka 12 tukaishi naye pamoja (pika pakua) mpaka alipotimiza miaka 19 mapema mwaka huu.Naweza kumsifia kuwa ni binti ambaye hakuwa na makuu wala tamaa maana alinikubali na maisha yangu hata nikiwa sina sawa nikiwa nacho sawa pia alikuwa mchapakazi na mwenye kujituma sana katika kutafuta.

Siku za karibuni alipata ujauzito ila mahusiano yaliingia dosari baada ya kugundua kuwa alisaliti. Pia aina ya mawasiliano aliyokuwa akifanya na wanaume tofauti tofauti hayakuwa na afya kwa mahusiano. Roho iliniuma sana, Pamoja na ujauzito aliokuwa nao Nilimrudisha kwao nikamueleza kwamba hata huo ujauzito sina uhakika kama ni wangu. Amekuwa akilia na kubembeleza kuomba msamaha kusisitiza ujauzito ni wa kwangu, Yupo radhi hata DNA ihusishwe.

Sasa nimekuja kwenu kuomba ushauri,

Je, kwa umri huo kuna uwezekano wa kubadilika huko mbeleni?

Je, Ikiwa ujauzito ni wangu kweli (ninahisi hivyo baada ya kujihakikishia) itakuwaje?

Je, Ni kawaida kwa mabinti wa umri huo kuchepuka kwamba baada ya umri fulani atatulia?

Je, Nikubaliane kwamba mtoto apate malezi ya mzazi mmoja ? (japo roho inaniuma kuona mtoto wangu ataishi mbali na baba yake na sikutegemea nitawahi kuwa na mtoto wa nje)

Je, Malezi ya mtoto pasipo na wazazi wawili hayatakuwa na madhara kwa mtoto?

Nawasilisha.

UPDATE
Nimeendelea kuhudumia ujauzito na kwa jinsi tunavyozungumza anaonyesha kujutia mno kitendo alichokifanya na hata kulia na kutoa machozi kabisa akiomba msamaha.Sasa wakuu hii inaweza kuwa ni kutokana na ujauzito tu aliokuwa nao ndio unapelekea afanye hivyo au ni majuto kweli kutoka moyoni?

Nawasilisha
 
Habari zenu wakuu,

Nimekuwa na mahusiano na binti mmoja,Ambaye tulikutana akiwa na miaka 18 nikiwa nimemzidi miaka 12 tukaishi naye pamoja (pika pakua) mpaka alipotimiza miaka 19 mapema mwaka huu.Naweza kumsifia kuwa ni binti ambaye hakuwa na makuu wala tamaa maana alinikubali na maisha yangu hata nikiwa sina
Wee jamaa shenzi Sana baada umeshaharibu future life ya mtoto wa watu sasa unataka hiyo mimba aipeleke wapi ????

Mbaya zaidi kwa age hiyoo ni sawa umebakaaa tuu
 
Je, Nikubaliane kwamba mtoto apate malezi ya mzazi mmoja ? (japo roho inaniuma kuona mtoto wangu ataishi mbali na baba yake na sikutegemea nitawahi kuwa na mtoto wa nje)

Je, Malezi ya mtoto pasipo na wazazi wawili hayatakuwa na madhara kwa mtoto?
Kwanini umwache mtoto alelewe na mtoto mwenzake peke yake wakati wewe mtu mzima upo badala ya kuendelea kuchukua jukumu la kulea watoto wote wawili? She's 18; what did you expect?!! Au unadhani umri wa kuonja onja unakuwa kwa wavulana peke yao?!
 
Habari zenu wakuu,

Nimekuwa na mahusiano na binti mmoja,Ambaye tulikutana akiwa na miaka 18 nikiwa nimemzidi miaka 12 tukaishi naye pamoja (pika pakua) mpaka alipotimiza miaka 19 mapema mwaka huu.Naweza kumsifia kuwa ni binti ambaye hakuwa na makuu wala tamaa maana alinikubali na maisha yangu hata nikiwa sina sawa nikiwa nacho
Wewe huwezi kuchomoka umesha nogewa na huyu bint wa 19, umekuja kutusanifu tu, ila jua mwanamke wanafanana tabia wote miaka kwao haina uwiano na matendo yao. Na pili mwana mke abadilikagi isipo kua anaficha au kupumzisha tabia yake mbaya, ila huiibua badaye.
 
Vibinti vya umri kati ya 17 - 22 waga vipumbavu sana na ku cheat ni rahisi! Vina mambo mengi mno ukiwa navyo kwenye relationship..

Wewe mchukue na ishi nae make ushamjaza so usimharibie feature yake..
Mbona naona kama hivi binti wadogo wengi wana mapenzi ya kweli, vikikupenda vimekupenda kweli, Maana wanakua hawajaumizwa bado na wanaume

Hlf wengi wanaona fahari kutoka na wanaume waliowazidi umri Times9
 
Habari zenu wakuu,

Nimekuwa na mahusiano na binti mmoja,Ambaye tulikutana akiwa na miaka 18 nikiwa nimemzidi miaka 12 tukaishi naye pamoja (pika pakua) mpaka alipotimiza miaka 19 mapema mwaka huu.Naweza kumsifia
Msamehe kwa sasa. Hutapata mtu perfect.
 
Mkuu aliesema NO PAIN ... NO GAIN .. hakua punguani ,haya mambo pasipo kukuumiza hata kinyesi utakiona pilau ,
Nakukumbusha tu kuwa JASIRI HAACHI ASILI...,
HATA KAMA SIO LEO UTAKUJA KUKUMBUKA NINACHOKUELEZA.
 
Kwanini umwache mtoto alelewe na mtoto mwenzake peke yake wakati wewe mtu mzima upo badala ya kuendelea kuchukua jukumu la kulea watoto wote wawili? She's 18; what did you expect?!! Au unadhani umri wa kuonja onja unakuwa kwa wavulana peke yao?!
Tatizo sio kulea tatizo alinisaliti hivyo nimeona nimuweke mbali kwanza.
 
Vibinti vya umri kati ya 17 - 22 waga vipumbavu sana na ku cheat ni rahisi! Vina mambo mengi mno ukiwa navyo kwenye relationship..

Wewe mchukue na ishi nae make ushamjaza so usimharibie future yake..
Usiangalie future yake tu angalia na future yangu pia.Kuishi na binti ambaye ameshafanya usaliti na kumfanya kuwa mke wa ndoa hapo baadaye unaona ni sawa?
 
Back
Top Bottom