Samahanini ndugu zangu,kwa dharula nyingi kiasi cha kushindwa kumalizia kisa changu,naomba niendeleee...
Baada ya mpnz wangu kunambia kuwa alikuwa anaumwa tumbo,nlikata simu nikalala. .
Asubuhi nilipoamka tu,cha kwanza niliwasha PC yangu,nikaingia fb,nikaingiza jina la jamaa aliyekuwa mpnz wangu,nikamuona na kumtumia friend request,aka accept,nikaanza kuchart na jamaa,
Baada ya kuwasiliana na jamaa kwa muda tulani,nilimuomba namba zake tukaanza kuwasiliana.
Baada ya siku kadhaa nikamwambia jamaa kuhusiana na mahusiano baina yetu watatu,jamaa alionyesha kukasirika sana,akadai amekuwa ktk mahusiano na mpnz wangu kwa zaidi ya Mwaka mmoja,tukakubaliana kumuumbua huyu binti...
Nilimpigia simu mpnz wangu,nikamuomba aje nyumbani,muda mfupi baadaye alifika.
Alipofika nilijitahidi sana kuficha hasira zangu,nilianza kuzungumza naye kwa upole kabisa,nlianza kwa kumuuliza swali,
Mm:Mary mpnz wangu,kwa ukweli kabisa kutoka moyoni,naomba niambie una wapenzi wangapi?
Mdada:jamani hivi kweli wewe ni wa kuniuliza swali kama hilo kweli!!!?(machozi yakaanza kumtoka),kwa hiyo unaniona mm malaya???