Nilikuwa sahihi kwa huyu kocha uchwara Pep Guardiola

Nilikuwa sahihi kwa huyu kocha uchwara Pep Guardiola

marcoveratti

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2017
Posts
1,019
Reaction score
1,824
Nimerejea tena kuitazama post yangu ya tarehe 2 June mwaka huu. Niliipa kichwa cha habari, "PEP GUADIOLA NI KOCHA WA KAWAIDAA MNOOO".

nilitoa mtazamo wangu kuhusu hyu kocha uchwara anae chukuliwa kama 50 cent wakati ana hadhi ya 20%
zimepita siku sabini toka niandike yale na nilipingwa sana na nikahisi labda nilikosea.
Nilianza kuhisi hivo ila siku niliyoona Man City ikiondolewa UEFA na Lyon ndio nika pigia mstari mawazo yangu.

Ilinibidi nisubiri muda upite, ili nitafakari vema kabla ya kuandika haya. Isiwe tu ni hisia za kunichania mkeka zimenikasirisha na kuamua kumhukumu[emoji1783]. Ila baada ya muda mrefu wa kutafakari, nimekubali tu kubadili mawazo. Huenda Pep Guardiola si kocha wa daraja la juu kama dunia inavomchukulia. Inawezekana.

Msimu wa nne mfululizo anashindwa kuivusha Man City robo fainali ya UEFA. Subiri kwanza, hii ndiyo timu iliyotumia fedha nyingi zaidi kusajili Ulaya kwa miaka minne iliyopita. Wamewazidi hadi PSG kwa pauni 200 milioni. Mafanikio makubwa aliyonayo ni mataji mawili ya ligi. Hivi kweli waarabu wanavunja benki kila msimu kumpa kila mtu anayemtaka kwa ajili ya mataji ya ligi? Sidhani.

Mara zote Pep alizoondoshwa UEFA, ameondoshwa na timu zilizotumia punje tu ya bajeti ya usajili aliyotumia yeye. Monaco, Liverpool, Tottenham na Lyon. Hakuna hata moja hapo inayoisogelea bajeti ya usajili ya Man City. Naelewa kuna kuteleza, ila kweli kuteleza kwa miaka minne? Sidhani.

Najua nitatajiwa mafanikio yake na Barcelona. Alichukua treble katika msimu wa kwanza na mataji 6 katika msimu wa pili akiwa na vijana tu aliowapandisha kutoka La Masia. Ni kweli, ila uliwahi kujiuliza wale vijana nani aliwapika? Guardiola aliwafundisha kwa miezi 9 tu kabla ya kukabidhiwa timu kubwa. Aliwatengeneza lini? Kazi nzima aliifanya Frank Rijkaard, ila hakuna anayemkumbuka.

Watu wanamuimba Pep tu, ila yeye alichofanya ni kuvuna tu shamba walilopanda wengine. Ndiyo maana kwa sasa, nimechagua kumuweka daraja tofauti. Asifananishwe hata na Klopp, alichukua ubingwa wa Ujerumani na Dortmund iliyojaa wavulana. Ameibadilisha Liverpool kwa bajeti ndogo tu, zaidi amefanikiwa nayo sana, sidhani kama Guardiola anaweza kufanya hayo. Ni maoni tu.
IMG-20200818-WA0132.jpg
 
Km hujui soka ukar pemben ww hv unajua Guadiola alimkataa ronaldhino alipopdwa barca na ktk miaka ile wengi waliamin tonaldhino ndio alikuwa bora lkn Guadiola alimkataa

Hv unajua bila Guadiola Messi asingekuwa staa yy ndie aliesema namtaka messi avae namba 10

Twende uwanjan sasa Guadiola ndio muasisi wa soka la TIKI TAKA possession na pass za hapa na pale kukaba kwa ushirikiano na kufunga magoli yenye akili
 
Valdez, Puyol, xavi, Iniesta,
Rijkaad alichukua barca ikiwa ovyo yeye ndio alianza kutengeneza
kama unamaanisha kutengeneza hao wachezaji basi ilikuwa ni Kazi ya Van Gaal, wote kina Puyol, Valdez, Xavi, Iniesta etc walitolewa Academy na LVG na kuletwa timu ya wakubwa, Huyu mzee aliwapiga benchi hadi kina Rivaldo na Kugombana na Bodi kwa ajili ya hao watoto.

15243304290496.jpg
 
Km hujui soka ukar pemben ww hv unajua Guadiola alimkataa ronaldhino alipopdwa barca na ktk miaka ile wengi waliamin tonaldhino ndio alikuwa bora lkn Guadiola alimkataa
Hv unajua bila Guadiola Messi asingekuwa staa yy ndie aliesema namtaka messi avae namba 10
Twende uwanjan sasa Guadiola ndio muasisi wa soka la TIKI TAKA possession na pass za hapa na pale kukaba kwa ushirikiano na kufunga magoli yenye akili
Shida ya mahaba akili huwa haifanyi kazi hata 0.0%, mihemuko ndiyo iliyokuendesha kuandika hii hoja uchwara sababu ya hisia/mahaba toka moyoni wala si akili halisi toka katika ubongo.
 
Km hujui soka ukar pemben ww hv unajua Guadiola alimkataa ronaldhino alipopdwa barca na ktk miaka ile wengi waliamin tonaldhino ndio alikuwa bora lkn Guadiola alimkataa
Hv unajua bila Guadiola Messi asingekuwa staa yy ndie aliesema namtaka messi avae namba 10
Twende uwanjan sasa Guadiola ndio muasisi wa soka la TIKI TAKA possession na pass za hapa na pale kukaba kwa ushirikiano na kufunga magoli yenye akili
Heheheheheh mwasisi wa soka la tiki taka
 
Km hujui soka ukar pemben ww hv unajua Guadiola alimkataa ronaldhino alipopdwa barca na ktk miaka ile wengi waliamin tonaldhino ndio alikuwa bora lkn Guadiola alimkataa
Hv unajua bila Guadiola Messi asingekuwa staa yy ndie aliesema namtaka messi avae namba 10
Twende uwanjan sasa Guadiola ndio muasisi wa soka la TIKI TAKA possession na pass za hapa na pale kukaba kwa ushirikiano na kufunga magoli yenye akili
Pia alivyofika man city aliendelea kung'ang'ania kumpanga sterling wakat alkuwa n mchezaj anaekosakosa sana magori ,lakin baadae alkuwa mfungaj mzur tu
 
Km hujui soka ukar pemben ww hv unajua Guadiola alimkataa ronaldhino alipopdwa barca na ktk miaka ile wengi waliamin tonaldhino ndio alikuwa bora lkn Guadiola alimkataa

Hv unajua bila Guadiola Messi asingekuwa staa yy ndie aliesema namtaka messi avae namba 10

Twende uwanjan sasa Guadiola ndio muasisi wa soka la TIKI TAKA possession na pass za hapa na pale kukaba kwa ushirikiano na kufunga magoli yenye akili
Tiki taka? mzee haupo serious
 
Ila kwa ile mechi ya Lyon huwez kumulaum kocha,walcheza vzur lakin bahat haikuwa kwao tu
Lawama moja kwa moja zinamuangukia kocha hivi Bernado Silva na Mahrez walikuwa wanafanya nini benchi na Gabriel Jesus alikuwa anafanya nini uwanjani
Mara mia ukatumia false number nine kuliko kumtumia natural kama Gabriel Jesus
 
Km hujui soka ukar pemben ww hv unajua Guadiola alimkataa ronaldhino alipopdwa barca na ktk miaka ile wengi waliamin tonaldhino ndio alikuwa bora lkn Guadiola alimkataa

Hv unajua bila Guadiola Messi asingekuwa staa yy ndie aliesema namtaka messi avae namba 10

Twende uwanjan sasa Guadiola ndio muasisi wa soka la TIKI TAKA possession na pass za hapa na pale kukaba kwa ushirikiano na kufunga magoli yenye akili
Guardiola muasisi wa tiki taka? Kwani wewe unazungumzia mpira au nini ndugu yangu?

Guradiola ni kocha wa kawaida. Sasa hivi anahitaji wachezaji 5 kwaajili ya msimu ujao. Huyu kocha kwa ile timu aliyonayo bado anaona anahitaji watu 5?

Lyon na wengine wataendelea kuwaumbua makocha feki kama hawa.
 
Tiki taka? mzee haupo serious
Guardiola muasisi wa tiki taka? Kwani wewe unazungumzia mpira au nini ndugu yangu?

Guradiola ni kocha wa kawaida. Sasa hivi anahitaji wachezaji 5 kwaajili ya msimu ujao. Huyu kocha kwa ile timu aliyonayo bado anaona anahitaji watu 5?

Lyon na wengine wataendelea kuwaumbua makocha feki kama hawa.
Naona mmehoji kuhusu Tiki taka kwa mshangao kama vile ni kitu kigeni.

Ni kweli Guardiola anatumia mfumo wa tiki taka kufundisha, yaani mpira wenye pasi nyingi fupi fupi na na kukaba kwa pressing ili kumiliki mpira wakati mwingi wa game.

Muasisi wa tiki taka football ni Barca legend Johan Cruyff ambaye aliifundisha Barca miaka ya mwishoni mwa 80 hadi 1996 kama sikosei.

Mfumo huo ulirithiwa na Luis van Gaal na baadaye Frank Rijkaard, kabla ya Guardiola ambaye naye aliendelea kuutumia na kuumodify hadi leo hii anaendelea nao.
 
Back
Top Bottom