Ibn Unuq found this usefullYani we jamaa, ni kama ikitokea umejenga fremu za biashara, then ukaona wapangaji wako wanapiga hela kuzidi kodi unayopata, utawafukuza ili hiyo biashara ufanye wewe, huwezi toboa namna hiyo mkuu maisha hayapo hivyo. Kwanza umesema biashara yake haifanani na yako, pia ulivyomkubalia, hamkukubaliana kwamba hatakiwi kufanikiwa sana. Unaumiaje roho mwingine kufanikiwa mkuu? Sio kwamba hii ndo itasababisha asikuibie?
Kama vipi mpe kiwango akuchangie kodi kila mwezi upunguze makali ya kodi ya fremu.
Biashara ilianza kushuka baada au kabla ya kumruhusu? Tuanzie hapa kwanza. Kama ni kabla, kumpunguzia kipato huyo jamaa hakutakuongezea wewe. Na kama ni baada, basi huenda biashara yake inahujumu biashara yako kwa namna moja au nyingine.naingiza faida ya laki 3 hadi 4, Kabla biashara haijashuka ilikuwa ni Laki 8+
Kuna jamaa yangu alikua mfanyakaazi wakiwanda Cha kutengeneza cosmetics akiwa na cheo kikubwa tu akawa na access yakuona formula zote zinazotumika kutengeneza cosmetics. Baada ya muda wa miaka 4 nae akaanzisha kampuni ya kuuza Chemical na kusaidia kuboresha cosmetics za watu wengine wanazotaka kutengeneza zilizo Bora. Boss alivyogundua alimfukuza kazi. Hali yakua mfanyakaz kasomea hayo mambo.Yani we jamaa, ni kama ikitokea umejenga fremu za biashara, then ukaona wapangaji wako wanapiga hela kuzidi kodi unayopata, utawafukuza ili hiyo biashara ufanye wewe, huwezi toboa namna hiyo mkuu maisha hayapo hivyo. Kwanza umesema biashara yake haifanani na yako, pia ulivyomkubalia, hamkukubaliana kwamba hatakiwi kufanikiwa sana. Unaumiaje roho mwingine kufanikiwa mkuu? Sio kwamba hii ndo itasababisha asikuibie?
Kama vipi mpe kiwango akuchangie kodi kila mwezi upunguze makali ya kodi ya fremu.
Hapa ni chura kapigwa teke, huwezi kuzuia watu kukua, kikubwa accept challenge, boresha mbinu so as to stay at the top of the game, wa kwanza ni wa kwanza siku zote.Kuna jamaa yangu alikua mfanyakaazi wakiwanda Cha kutengeneza cosmetics akiwa na cheo kikubwa tu akawa na access yakuona formula zote zinazotumika kutengeneza cosmetics. Baada ya muda wa miaka 4 nae akaanzisha kampuni ya kuuza Chemical na kusaidia kuboresha cosmetics za watu wengine wanazotaka kutengeneza zilizo Bora. Boss alivyogundua alimfukuza kazi. Hali yakua mfanyakaz kasomea hayo mambo.
Msaidizi wa kuuza bidhaa zako dukani unataka akuze biashara yako ?; Nadhani watu manachukulia biashara poa...., Kumbuka hii ni bongo ya madalali na wachuuzi, it's not rocket science (If she/he can do outstanding abaki hapo kwako anafanya nini..., unaongelea anakaa kama picha...., wewe picha za kwenu zinafanya mauzo.... au unalimpa pesa ya marketing na sales ?ooh stop that bulshits[emoji34]. so nimemueka kwenye duka awe kama picha au aoneshe meno yake? nimemuweka ili biashara ikue nacizidi kua bora iingize faida. siweki mfanyakazi kama picha kwamba mteja akija ye aamue if amuuzie au la. naweka mfanyakazi ili anisaidie kuuza, kuconvice customers na kutengeneza mazingira ya biashara yawe mazuri wateja wazidi kupenda na kuja. Thatsc why in interview unapewa maelezo ya kazi ilivo na vile boss (management) anaexpect, nwisho unaulizwa utaweza au tutafte mtu mwingine? akikubali , he/she must do exactly what he/she promosed, not otherwise. LAZIMA AHAKIKISHE BIASHARA INAKUA, Full stop!
Ninadhani si kwa ubaya. Kumbuka hakuna biashara inayoingiza faida tu. Ni vema huyo mhudumu pia alipie gharama fulani,mfano,kodi na gharama nyingine ili kusaidiana eneo na biashara zao zidumu. Lengo lilikuwa zuri,kumsogeza ili na yeye abadili maisha. Kama biashara imekaa vizuri,si vibaya ikarudisha kiasi fulani kwenye fremu. Wala huyo tajiri asifikirie kuila au kumfilisi,wakae mezani wayajenge.Kunjua roho mkuu,muache nae apate riziki kama hajaharibu kazi yako.
Mimi ninadhani awali ulikuwa na malengo mazuri na hata sasa bado una malengo mazuri. Ni uungwana unachofanya kutafuta namna bora ambayo haitamuumiza dogo.Uzi huu nimeweka jukwaa la biashara nategemea michango yenye tija. Tujue kutofautisha biashara na vituo vya kutoa misaada bure, msikiti, kanisa, n.k,
Kuna kaduka nilifungua, kwakuwa utumishi umenibana niliweka msaidizi anisaidie.
Biashara imeshuka lakini kibishi naendelea nayo
nikitoa gharama za frame nayolipia laki 5 kila mwezi (AISEE !!), mshahara, allowance, umeme, usafi, Tra, leseni, n.k. naingiza faida ya laki 3 hadi 4, Kabla biashara haijashuka ilikuwa ni Laki 8+
msaidizii aliwahi kuniomba aanze kuweka bdhaa zake, Nilichukulia poa kwasababu niliona bidhaa anazouza ni ndogo na ni nje ya biashara nayofanya, Nikamruhusu.
Mshahara naomlipa ni 150,000 kwa mwezi, allowance ya matumizi yake elf 70, jumla 220,000
Leo nilifika dukani hayupo kafunga, nina ufunguo wangu nikaingia, kuna kidaftari nilikiona kwenye draw.
Kapangiliaia vizuri sana hesabu zake, kila siku anafunga hesabu kwa faida ya elf 6 hadi 7, sometmes elf 8
Nilipiga picha fasta, nimefika home nimepiga hesabu, mwezi uliopita kaingiza faida 183,500
Kuna maamuzi kadhaa nataka nichukue
- Nimwambie awe anachukua faida asilimia kadhaa kwa biashara yoyote atayoifanya dukani kwangu
- Nisimlipe mshahara wake niwe nampa aloowance pekee, ajilipe mshahara kwenye faida
- Nimpe miezi kadhaa auze, baada ya hapo iwe biashara yangu
Ni jambo liliilonfanya nitafakari sana, nichukue maamuz yapi.
Kwa wale ambao mnaingiza mambo ya huruma, mle mlale
Swali zuri sana, laki na themanini tu roho inamuuma hivyo, je, faida ingekuwa laki 4 kwa mwezi si angemroga kabisa!Kwenye mategemeo yako faida yake ilitakiwa kuwa kama ngapi?
Wale wale, halafu nyie wote ni wanawake!Hao kuku wanaokuambia roho mbaya ukute hawajawahi hata kufanya biashara...
Ngoja nikuambie, Mimi kitambo nilikua nauza duka la mtu, hivyo hivyo nikaanza kuweka bidhaa zangu kisiri siri(MALENGO), akija mteja nachukua namba, nampigia namuelekeza duka letu jingine(ROHO MBAYA), sehemu niliyokua nauza mimi kodi ilikua chini hivyo Bei ikawa ipo chini pia, ila pale kwa Boss sababu ni potential nikawa napatumia kutangaza biashara yangu ila delivery nyingi zinafanyika kupitia kwangu, (ROHO MBAYA PLUS).
Baada ya hapo mauzo yakawa yapo chini, ila kwa sababu bado ile sehemu naihitaji, lakini pia nisimzunguke 100% mtu alieniamini, bila yeye kujua nikamshauri tuweke mzigo wa jumla, ambao najua mimi sina uwezo nao..
Akazama mfukoni tukashusha Kontena za kutosha,
BIASHARA IKAPANDA, akanishukuru sana kwa idea ile na Mimi nikapanda,
WIN WIN..
Wewe usihangaike na faida yake, hangaika na mauzo/faida yako, jipe muda, ukigundua inashuka sababu ya biashara yake, Mlipe kwa % au piga chini, ukiona inapanda(ilishuka kwa sababu nyingine) muache, hata akiingiza faida kama yako, kuna watu wana vismati, as long wote mnakula basi sawaaaaa..
Sasa wewe wasikilize hao ngiri eti roho mbaya, kesho ufunge biasha uje hapa wakugeuke...
Yaani nilipe kodi ya 500k, nikulipe 220k, nitoke kwenye faida ya 800k nije 300k, kwa sababu YAKO, nikuache eti kisa na wewe unatafuta? Nani asiyemtafutaji???
Kila mtu ashinde mechi zake.
Balance mambo yako twende sawa.
Haya papai...Wale wale, halafu nyie wote ni wanawake!