Nilishindwa kulala usiku baada ya kusoma 'Sheria mpya ya Usalama wa Taifa'. Nimeumia sana kama mwananchi wa kawaida

Nilishindwa kulala usiku baada ya kusoma 'Sheria mpya ya Usalama wa Taifa'. Nimeumia sana kama mwananchi wa kawaida

Sio hii. Deep state nawafahamu. Ni kikundi cha watu hata hawazidi 5 wakifika 10 wengine ni bosheni tu sio kundi kubwa kiasi hiki
Kiongozi hao wa5 wanaounda deep state ya nchi hii unawafahamu utuwekee majina yao hapa
 
Kwa nchi za wenzetu.. Vitengo vya usalama kidogo wana utu.. Kisha hata wakifanya kazi za hatari ikiwepo kueliminate mtu kunakuwa na mashiko..

Shida ni kwetu siasa ni nyingi...

Atakuja kuondolewa mtu wa kisiasa na sababu zisizo na kichwa wala miguu...

Raia wajiandae.. Yaani unapotezwa kiintelegensia.. Majibu yanatoka kwa usalama wa nchi... Afisa aliyehusika analindwa kisheria..

Wengi wa maafisa hawa wapo kichama na kishabiki na sio weledi wa kazi... Wataumiza watu wengi... Tusubiri
 
Tunapaswa kufanya maamuzi kwa kuzingatia maendeleo ya sayansi na teknolojia ktk kila nyanja..

Ni tatizo kubwa sana kuwa na wananchi walio juu ya sheria ikiwemo wenye mamlaka yeyote..

Kila mmoja wetu anapaswa kuwa chini ya sheria ikiwemo viongozi wakuu..

Muhimili wa mahakama pamoja na mapungufu una umahili na mfumo thabiti ktk utoaji haki kijinai hata madai..

Mfumo wa uendeshaji Mashitaka,Mfumo wa na sheria ya ushahidi vipo wazi katika kufanya upembuzi wa hatia ama kutokua na hatia kwa mshitakiwa yeyote awe mkubwa ama mdogo..

Kubwa zaidi ni mhimili wa mahakama kuwa huru zaidi hasa ktk uteuzi wa Jaji mkuu,Wasajiri,majaji,Mfuko huru wa fedha ktk kufanikisha mipango na mikakati yake pasipo kuingiliwa na Serikali..Hili litawaweka huru wasimamia haki kutoshurutishwa na wenye mamlaka juu ya hatima zao pindi wakifanya maamuzi kwa kuzingatia haki na si misukumo ya kisiasa,ubinafsi wa wenye mamlaka.

Kuweka kinga ni ruhusa ya uovu,uasi,uharibifu na machukizo makuu ktk amani,utulivu,usalama na ustahimilivu ktk taifa..

No one should be above the Law..No matter what is needed to be done,Should be done in accordance to the country Constitution and Laws..

Ktk hili ninaamini hata watumishi watiifu wa idara ni watiifu kwa Katiba yetu na sheria zetu hivyo hawawezi support mabadiriko yanayolawiti haki,utu,ubinadamu,Usawa na undugu..

Mwisho,Maafisa ni wajukuu zetu,Watoto zetu na ni binadamu kama wengine..wana mapungufu,mihemuko,udhaifu na changamoto (Ktk Elimu,Mapenzi,Siasa,jamii,Biashara,Sayansi,etc)…In a sense kwamba wapo kila sehemu ktk maisha yetu ya kila siku..Wapo Jeshini,Polisi,uhamiaji,Vyuoni,Mashuleni,Wafanyabiashara,Madaktari,Injinia’s,Bodaboda,wauza mchicha,machangudoa,wauza bar,wasafisha viatu,Makuri,Mafundi garage,Waiters…Wachungaji,Maaskofu..Masheikh..Ma house girls,N.k

Hatupaswi kuwapa mamlaka na nguvu isiozibitika kwa mifumo ya wazi kisheria..Hata wanajeshi Ambao ni wapiganaji kwa niaba ya wananchi wote wana mfumo wa utoaji haki kijashi (Mahakama za kijeshi)..Hii yote ni kudhibiti matumizi mabaya ya vyeo,mamlaka,madaraka na mafunzo au ujuzi..

Tanzania tunayoijenga tuijenge iwe ya neema na si majanga,hofu na wasiwasi considering bad perspective na experience juu ya wasiojulikana…

Nawapongeza maafisa wetu wa usalama wa taifa kwa kazi ngumu na kujitoa kwa viapo vigumu ili kuhakikisha nchi inakuwa salama kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama..Checks and balance is innevitable📌
 
Kwa nchi za wenzetu.. Vitengo vya usalama kidogo wana utu.. Kisha hata wakifanya kazi za hatari ikiwepo kueliminate mtu kunakuwa na mashiko..

Shida ni kwetu siasa ni nyingi...

Atakuja kuondolewa mtu wa kisiasa na sababu zisizo na kichwa wala miguu...

Raia wajiandae.. Yaani unapotezwa kiintelegensia.. Majibu yanatoka kwa usalama wa nchi... Afisa aliyehusika analindwa kisheria..

Wengi wa maafisa hawa wapo kichama na kishabiki na sio weledi wa kazi... Wataumiza watu wengi... Tusubiri
Ni makada wa CCM wote
 
Ni vizuri wenye washkaji huko watambe 🤣 ukizingua nakutia nyavuni mkulungwa anamaliza show.

Glock45 click cluck muthafuqa😀
 
Mlisema jiwe ni DIKTETA sio!

Kula chuma hicho.
Watu walikuwa busy kueleza mabaya ya dikteta Jiwe kwa madai ya kwamba viongozi waliyopo sasa wajifunze wasirudie tena makosa kama ya Jiwe, ila kinachoendelea ni wazi viongozi waliyopo hakuna walicho jifunza.
 
Nimeona kama wasiojulikana wamewekwa rasmi kwenye mfumo wa kiutawala.

Kwanini?

Kwa sababu hakuna anayewafahamu maafisa usalama wa Taifa kwa uwazi. Wapo kwa kificho zaidi kama wasiojulikana. Hakuna anayefahamu mipaka ya maafisa wa usalama wa Taifa. Haijulikani wanaanzia wapi na kuishia wapi mipaka yao kimajukumu.

Mwekezaji mzawa ama wa kudumu anawezaje kuwekeza kwenye Nchi ambayo kuna mamlaka makubwa yasiyojulikana juu ya hatma yake kibiashara ama kimaisha ama uhai wake? Ni ngumu sana.

Wakuu, nimeogopa hili Taifa kuliko kawaida. Ni Taifa langu la kuzaliwa. Lakini siwezi tena kujivunia. Naogopa. Nadhani, busara ni kufanya utaratibu wa kuhamia Burundi, kule huenda kuna unafuu zaidi kuliko Tanzania.

Hawa huwezi kukabiliana nao kwa lolote lile. Utahatarisha maisha yako bila sababu. Wana mamlaka makubwa kuzidi hata ya Rais mwenyewe. Watakufanya lolote lile watakalo na huna la kuwafanya. Yaani, kitakachokuokoa ukijichanganya ni Mwenyenzi Mungu pekee ama huruma za tu za kibinadamu na si vinginevyo.

Unaweza tena kugombania nao demu? Thubutu.

Unaweza tena kujimbwafai ukiwa bar ukisema hii ni nchi yetu wote, usinitishe? Thubutu.

Unaweza tena kubishana Yanga na Simba kijiweni? Thubutu.

Unaweza tena kubishana ishu za Chadema na CCM kijiweni? Thubutu.

Nikiwa kama kiongozi wa Umma, kwa mfano: Kwa nini nisihakikishe mwanangu anaingia usalama wa Taifa ili apate kinga ya kudumu?

Hata hivyo, inasemekana mtaani waliojaa usalama wa Taifa ni watoto wa wakubwa. Inasemekana.

Je, huenda wakubwa na familia zao wameamua kujiwekea kinga za kudumu kwenye Taifa hili? Mungu anayajua. Itakubidi, uishi kwa kujikunyata maana hujui nani ni nani na anatekeleza majukumu yapi ya usalama wa Taifa.

Pamoja na hayo, kama Baraza la Mawaziri wameona sheria hiyo ipo kamili basi tena na iwe kama watakavyo. Kila mwananchi aangalie namna ya kujihami.

Huenda ni hofu yangu kwa kuwa sijaelewa vizuri sheria yenyewe. Kama hivyo, basi na uzi huu uondolewe isilete taharuki kwa wengine wasioelewa kama mimi.

"Unapowekewa kinga ya kutoshitakiwa ni kama vile umeambiwa fanya makosa kwa kadri uwezavyo ili mradi unafanya kwenye line ya majukumu yako kikazi. Ni kama vile umeondolewa umakini wako kazini........yaani ni sawa na kama umeambiwa huna sababu ya kuwa makini kazini kwako kwa sababu hata ukikosea hakuna kitu utafanywa maana ni makosa kazini".

Eeehhh Mungu Baba ingilia kati Taifa hili.

Naomba kuwasilisha!

Pia soma: Muswada wa mabadiliko ya Sheria ya Idara ya Usalama wa Taifa unaoifanya iwe chini ya usimamizi wa Rais watua Bungeni
Hapa kuna shida kubwa ya kiungozi katika taifa letu. hii mbegu inayopandwa sasa kuna siku huko mbeleni tutaivuna wote pamoja kwa madhara sawa, na hao wanaodhani watakuwa salama baada ya kutungwa kwa sheria hizi. ikumbukwe hata Rwanda na Burundi hapo mwanzo mambo yalikuwa hivi hivi yaani kundi moja la watu kuona lina haki zaidi katika Taifa kuliko wengine na kujitungia sheria kedekede za kujilinda na hata ikibidi kuzima uhai wa wengine ili kubaki madarakani, lakini mwisho siku maangamizi yakatokea ambapo kila upande ulipoteza watu wengi kutokana na kuchukulia mambo for granted kama yanayoendelea hapa kwetu sasa hivi. Kuna watu wanadhani hii nchi ni ya kwao na kwamba pasipo wao kuwa madarakani bora nchi iwake moto. Kuna siku hizi sheria zitashindwa kuwalinda hata hao waliyozitunga na kuzibariki zitumike.
 
Sheria haifai kama ni kweli
Yaani mtu anaweza kukuua tu kwa wivu wa mapenzi kwa mfano,halafu aka fabricate ulikuwa unahatarisha usalama wa taifa na hawezi kushitakiwa kwa mauaji?
Ni hatari sana hii
Tatizo lipo hapo, ni vipi tutajua hakua kwenye majukumu yake?
 
Back
Top Bottom