Nilisoma shule ya msingi private day tunatoka saa saba na tulipasua freshi tu, siku hizi wanatoka jioni na kuhimiza boarding kuna kipi cha ziada?

Nilisoma shule ya msingi private day tunatoka saa saba na tulipasua freshi tu, siku hizi wanatoka jioni na kuhimiza boarding kuna kipi cha ziada?

gearbox

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2024
Posts
563
Reaction score
1,768
Hasa ukizingatia masomo ya shule ya msingi ni ya kawaida sana hayana mambo mengi, Sijaona ulazima wa kuwafanya watoto wadogo wasome utadhani wapo form 6.

Watoto wanabaki mpaka jioni, Shule zinahimiza watoto wabaki boarding, elimu ya msingi ni ya kukamiwa kiasi hicho?

Nakumbuka hapo zamani waliokuwa wanabaki shuleni ni darasa la nne na la saba tena ni kile kipindi mitihani inapokaribia.
 
wepesi wa elimu ya msingi isiyo na vitu vingi ukilinganisha na elimu inavyofanywa iwe complicated unabaki na viulizo vingi sana
 
Ma remedial kama zote...mtoto wa darasa la nne akae boarding kweli?
 
Nakumbuka darasa la kwanza tulikuwa tunaingia saa 2 kutoka saa tano. La pili saa sita hadi kumi. Full kuimba na kucheza. Hakuna cha tuition wala nini mpaka tunamaliza la saba.
Siku hizi shule zimekuwa biashara. Sijui boarding primary, weekend, kipindi cha likizo.
Wakimaliza mitihani wanasahau kila kitu loh.
 
Wazo jema sana,wazazi wanaingia gharama zisizo la lazima kama vile michango ya chakula na remedial.
Mtoto akitoka saa saba ataenda kula nyumbani na kufanya shughuli zingine.
Mamlanka husika ziangalie namna nzuri
 
Unakutana na katoto kwenye daladala usiku kanarudi nyumbani kutoka shule, kamechoka sana huku begi kubwa likiwa mgongoni, inasikitisha sana
 
Umenikumbusha kuna dogo nlkuwa nakaa kwao, sasa Ile wiki moja karibia necta form four akaenda kukaa getto na wanafunzi wenzake ety ili asichanganye mambo ya nyumbani na shule ili afaulu, eeeh bhana eee Mungu sio Lucas Mwashambwa dogo akala 0 yake safiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Hasa ukizingatia masomo ya shule ya msingi ni ya kawaida sana hayana mambo mengi, Sijaona ulazima wa kuwafanya watoto wadogo wasome utadhani wapo form 6.

Watoto wanabaki mpaka jioni, Shule zinahimiza watoto wabaki boarding, elimu ya msingi ni ya kukamiwa kiasi hicho?

Nakumbuka hapo zamani waliokuwa wanabaki shuleni ni darasa la nne na la saba tena ni kile kipindi mitihani inapokaribia.
Hakuna cha ziada ni kwa sababu wazazi wengi wapo busy kutafuta maisha kwa hiyo wanaona shuleni ndio angalau sehemu salama kwa watoto.
 
Japokuwa vijana wetu siku hizi wanachangamoto nyingi kuanzia kwenye malezi yetu sisi wazazi LAKINI kuna upigaji mwingi mno nyuma ya pazia ya hizo 'Remedials'
 
Back
Top Bottom