Nilitabiri Denis Kibu atakuja kucheza Ulaya na kuwafunga midomo

Nilitabiri Denis Kibu atakuja kucheza Ulaya na kuwafunga midomo

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Kutokana na sintofahamu na tetesi zinazoendelea kuhusiana na Denis Kibu (mpaka leo sielewi kwa nini watu wanamuita Kibu Denis badala ya Denis Kibu lakini hilo tuliache kwa leo), nimekumbuka kauli yangu niliyowahi kuitoa kuhusu future yake. Niliwahi kusema kuweni na akiba ya maneno, kuna siku mtamkuta Kibu anacheza Ulaya.

Huu uzi umebadili direction sana naona hadi watu wamechanganyikiwa 🤣😂🤣 Siku mkisikia Kibu ameuzwa Belgium uzi utafufuka tena.

Ni kweli Kibu siyo mchezaji mwenye ile unaita kipaji asili cha kina Chama au Aziz Ki ila kitu kimoja ambacho atakupa kila siku atakayoingia uwanjani ni juhudi za asilimia 100. Katika mpira wa sasa ambao mbinu za mchezo na nguvu zina nafasi kubwa kuliko umahiri binafsi wa mchezaji, Kibu ana nafasi kubwa ya kucheza. Kibu anacheza vizuri tu EPL hata kama siyo katika timu kubwa.

Nimalizie kwa kusema, kama kachukua pesa ya Simba akatoweka atakuwa kazingua sana na hapo inaonyesha jinsi management za wachezaji wa Kitanzania zinavyokosa weledi. Kiufupi alikosa washauri wazuri.
 
Za ndaani kabisa kibu d katorokea Norway

IMG-20240723-WA0014.jpg
IMG-20240723-WA0015.jpg
IMG-20240723-WA0013.jpg
IMG-20240723-WA0012.jpg
 
Hizi Timu doto na kulwa janja janja sana inawezekana hata huo Mkataba hawajaweka na pesa ajalipwa Wachezaji wanatunza siri sana kwa hizi Timu zetu ni vile wengi tumevamia mpira juzi tu...
Kweli kabisa sema hizi team zinamiliki Mashabiki wanaoziamini kuliko kuamini wachezaji hali ambayo huwaacha wachezaji bila mtetezi
Zenyewe ni mikwara tu
 
Hizi Timu doto na kulwa janja janja sana inawezekana hata huo Mkataba hawajaweka na pesa ajalipwa Wachezaji wanatunza siri sana kwa hizi Timu zetu ni vile wengi tumevamia mpira juzi tu...
Umemsikilza Meneja wake lakini? Kibu haidai chochote Simba, amekamilishiwa mkataba kwa 100%
 
Umemsikilza Meneja wake lakini? Kibu haidai chochote Simba, amekamilishiwa mkataba kwa 100%
Hizi Timu zinakua na mikataba miwili miwili ili kuwaibia Wafanyakazi wake na TFF wapo kimya..mchezaji akitaka kuondoka kwa ridhaa yake hawataki hata kama mkataba unamruhusu wao mara nyingi wanataka ndio wakuache au wakukopeshe..
 
Kweli kabisa sema hizi team zinamiliki Mashabiki wanaoziamini kuliko kuamini wachezaji hali ambayo huwaacha wachezaji bila mtetezi
Zenyewe ni mikwara tu
Timu ndio chanzo cha migogoro ya Mikataba yote hao washabiki hawajiulizi kwa nini inatokea kwenye usajiri wa Timu zao tu na si kwingine ni vile wanabebwa na TFF lakini kama TFF wangekua wanajisimamia haya mambo yasingekuwepo..
 
Kutokana na sintofahamu na tetesi zinazoendelea kuhusiana na Denis Kibu (mpaka leo sielewi kwa nini watu wanamuita Kibu Denis badala ya Denis Kibu lakini hilo tuliache kwa leo), nimekumbuka kauli yangu niliyowahi kuitoa kuhusu future yake. Niliwahi kusema kuweni na akiba ya maneno, kuna siku mtamkuta Kibu anacheza Ulaya.



Ni kweli Kibu siyo mchezaji mwenye ile unaita kipaji asili cha kina Chama au Aziz Ki ila kitu kimoja ambacho atakupa kila siku atakayoingia uwanjani ni juhudi za asilimia 100. Katika mpira wa sasa ambao mbinu za mchezo na nguvu zina nafasi kubwa kuliko umahiri binafsi wa mchezaji, Kibu ana nafasi kubwa ya kucheza. Kibu anacheza vizuri tu EPL hata kama siyo katika timu kubwa.

Nimalizie kwa kusema, kama kachukua pesa ya Simba akatoweka atakuwa kazingua sana na hapo inaonyesha jinsi management za wachezaji wa Kitanzania zinavyokosa weledi. Kiufupi alikosa washauri wazuri.
Aje kwanza amalizane na club yake l, mpira haupo hivyo
 
Back
Top Bottom