Nilitaka kumpiga makofi Afisa wa uhamiaji

Nilitaka kumpiga makofi Afisa wa uhamiaji


Halafu usikute wakati anaongea na wewe alikuwa anatafuna karanga hovyo hovyo bila utaratibu.

Hapo alikuwa anatengeneza mazingira ya rushwa.

Kama tumeamua kufanya vitu mitandaoni sioni sababu ya kufanya nusu mtandaoni halafu tumalizie ana kwa ana. Ni kwanini uhamiaji wasiweke utaratibu wa kumaliza mambo yote mtandaoni?

Njia pekee ya kumaliza rushwa kwenye ofisi za umma ni kuweka utaratibu huduma zote zifanyike kwa njia ya mtandao.
 
Ona huyu naye, hopeless folk.
Uhamiaji njaa tupu, tumewahonga sana wanapokea tu hawana aibu wala haya.

Ukimpa laki anakenua mpaka koromeo linaonekana. Atajichekesha chekesha huku anakuita majina yote, boss, muheshimiwa, mtukufu!

Hata kama huna vigezo ukitoa hela unapewa vibali vyote kiulaini sana.

Kibali cha kazi na cha ukaazi vyote unapewaaaa bwerereee bila vigezo, mradi umetoa tu pesa.
 

Halafu usikute wakati anaongea na wewe alikuwa anatafuna karanga hovyo hovyo bila utaratibu.

Hapo alikuwa anatengeneza mazingira ya rushwa.

Kama tumeamua kufanya vitu mitandaoni sioni sababu ya kufanya nusu mtandaoni halafu tumalizie ana kwa ana. Ni kwanini uhamiaji wasiweke utaratibu wa kumaliza mambo yote mtandaoni?

Njia pekee ya kumaliza rushwa kwenye ofisi za umma ni kuweka utaratibu huduma zote zifanyike kwa njia ya mtandao.
Umeongea neno 👍🏾
 

Halafu usikute wakati anaongea na wewe alikuwa anatafuna karanga hovyo hovyo bila utaratibu.

Hapo alikuwa anatengeneza mazingira ya rushwa.

Kama tumeamua kufanya vitu mitandaoni sioni sababu ya kufanya nusu mtandaoni halafu tumalizie ana kwa ana. Ni kwanini uhamiaji wasiweke utaratibu wa kumaliza mambo yote mtandaoni?

Njia pekee ya kumaliza rushwa kwenye ofisi za umma ni kuweka utaratibu huduma zote zifanyike kwa njia ya mtandao.
Uko sawa kabisa mkuu. Technology inaweza kupunguza rushwa kwa kiwango kikubwa sana maana inapunguza kuonana ana kwa ana na watendaji.

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
''Sasa maasai utatoboa kweli?''

Hii kauli ni ya kibaguzi sana Prejudice, Kwani Maasai sio wananchi? Hawastahili Passport?

Mkuu huyo jamaa muweke wazi ili wahusika wadeal nae, siku nyingine uwe unarekodi kwa siri au japo urekodi sauti tu,kwa ushahidi wa tukio husika,

Pole sana Mkuu.
nilidhani ni waha tu kumbe mpaka masai wanabaguliwa?
 
usipende kurusha rusha ngumi,ni dalili ya usela mavi na kukosa kujisimamia katika maisha.

hapo kilichokupeleka ni kitu kingine cha msingi sana katika maisha,unaamua kumsugua ndosi afisa,unakamatwa,unawekwa mahabusu,kesi mahakamani,hutoboi unalipa fine au kifungo.
umeshavuruga mipango yako.

NB,wewe ni msimamizi wa mipango yako,ukikubali mtu aivuruge,umekubali akutawale.
 
Raha yao kujaza watu upepo tu na usipokuwa makini utajaa kweli.

Swali langu ni kuwa hata wale ngozi nyeupe (Indian&Arabs) wanafanyiwa hivi kweli? Au sisi wamatumbi tu.
Tena hao utawaonea huruma kama hawana hela,mie mzee wangu alisumbuliwa sana na hapo alikuwa ana renew na kuwaombea wadogo zangu alisumbuliwa sana akaambiwa atoe milioni 10 akagoma, wakati kazaliwa tanzania na wazazi wake hawajazaliwa Tanzania lakini walikuwa na uraia wa Tanzania na nyaraka zote aliwapa, mwisho wa siku wadogo zangu wakaamua kwenda kuomba za kenya wakapata fasta bila usumbufu.
 
Tena hao utawaonea huruma kama hawana hela,mie mzee wangu alisumbuliwa sana na hapo alikuwa ana renew na kuwaombea wadogo zangu alisumbuliwa sana akaambiwa atoe milioni 10 akagoma, wakati kazaliwa tanzania na wazazi wake hawajazaliwa Tanzania lakini walikuwa na uraia wa Tanzania na nyaraka zote aliwapa, mwisho wa siku wadogo zangu wakaamua kwenda kuomba za kenya wakapata fasta bila usumbufu.
Duh kumbe! Basi ni tatizo kubwa!
 
Duh kumbe! Basi ni tatizo kubwa!
hapo ilikuwa kipindi cha magu, ila awamu ya sasa watu wengi nawafahamu wameomba na wamepata tena haraka wiki mbili tuu bila kutoa chochote, tena kuna mmoja dom alienda akaambiwa bado hichi akaenda kuleta, akaambiwa tena bado hichi yule afisa akamwambia hiyo document unitumie tuu kwenye wasap nijiridhishe twende ukapige picha na kuweka finger print na after 3 weeks akapata passport yake bila kujuana na mtu au kutoa chochote. sasa hivi kama huna connection na umekamilisha documents zote (alafu vizia ile foleni ya mchana ufike wakiwa wanakaribia kutoka)passport ni wiki mbili ila unapata,ukiwa na connection passport ni siku tatu tuu umepata 😀.
 
Kwa muda mrefu Nilikuwa nasikia kwamba Maafisa Uhamiaji wengi ni wababaishaji, Leo nimeshuhudia kwa macho.

Nilijaza fomu la maombi ya passport online Nikalipia kisha nika download na kuwasilisha Ofisi za uhamiaji mkoa.

Afisa Aliyenipokea akaniuliza wewe ni kabila gani? Nikamuambia Maasai. Akaniuliza, Sasa Maasai utatoboa kweli? Nikamkazia uso[emoji2955]

Akaanza kukagua majina na attachments akaniuliza cheti cha kuzaliwa baba nikamuambia alifariki. Akaniambia cheti chake cha kifo Kiko wapi nikamchomolea.

Akaniuliza namba yake ya NIDA Iko wapi? Nikamuambia mtu aliyefariki mwaka 1996 namba ya NIDA inapatikanaje? Akaniambia ndiyo utaratibu uliopo. Nikashindwa kumuelewa[emoji849]

Akaniambia anataka kitambulisho Cha mama, nikamuambia nimeambatanisha barua ya utambulisho kutoka kwa Afisa mtendaji na kuna namba yake ya ya NIDA kwenye hiyo barua.

Akasema anataka cheti cha kuzaliwa, nikamuambia Kuna Affidavit hapo akasema affidavit siyo cheti.

Hapo ndipo nikajua jamaa ni mpumbavu, nikamuambia kwahiyo mlipoweka kwenye tovuti yenu kuwa affidavit ni mbadala wa cheti cha kuzaliwa, mlikuwa mnatania?

Tukaanza kurushiana maneno nikataka kumpiga makofi akatokea dada mmoja(Afisa mwenzake) Akaniambia samahani kaka naomba nikusikilize. Nikamueleza scenario yote, akakagua fomu na attachments zangu na kuniambia viko sawa niondoke, nitapigiwa simu.

Nikaondoka hatua chache, nikawaza kuwa hawa jamaa wameshaonesha negative attitude, Kuna uwezekano hawatatuma fomu langu makao makuu. Nikarudi nikawaambia wanipe fomu langu nikapokea na kuondoka nalo. Nitaenda likizo hivi Karibuni nitafanyia hili zoezi mkoani kwetu. Ila kumbe Maafisa Uhamiaji wengi ni wapumbavu.
Mkuu ulikua unatengenezewa mazingira ya rushwa sema na wwe umekamilika kila kitu ndiyo maana afisa akakasirika!!
 
Uko sawa kabisa mkuu. Technology inaweza kupunguza rushwa kwa kiwango kikubwa sana maana inapunguza kuonana ana kwa ana na watendaji.

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
Na Watumishi wengi hawapendi.hiyo Technology maana inawanyima kula, lazima.watai sabotage tu kama wale wa Mwendokasi na zile kadi zilivyo yeyuka, na sasa wana furahi wamerudi kwe vi risit vyao vya karatasi hadi sasa wanaamua kuzulumu zile change 50 50 za.wateja, wakati kipindi cha kadi kulikua hakuna hata mambo ya usumbufu wa change!!
 
Back
Top Bottom