Nilivyokuwa najiona mjanja, nikaishia kutapeliwa Milioni 42

Nilivyokuwa najiona mjanja, nikaishia kutapeliwa Milioni 42

Nashukuru kwa ufafanuzi mkuu,ndio maana niliuliza mwaka na jina la chuo nilikua sijui kama zamani boom lilikua linapokelewa kwa muhasibu.
Kipindi icho ilikua 620,000(boom 420k na stationary 200k) unapewa pesa mkononi, 1st year wengi sana walipoteza pesa zao siku Hio Hio maana siunajua kiwewe tena Cha pesa
 
Dogo una spirit ya hustling, una uthubutu, una nidhamu ya fedha bila shaka ushafika mbali sana kibiashara. Mshukuru sana Mungu wengi tuneshindwa tunaishia kwenye ndoto tu!!
Niomba uni tag ukileta sehemu ya 2
 
Pesa inatengenezwa pale ambapo wengine hawawezi kudhani inawezekana.

Hivi unadhani kwa akili ya kawaida tu ile over invoice ya ATCL kwenye uhalisia wa kawaida unaweza kudhani mtu/watu anaweza/wanaweza kuyafanya yale??

Nimeona hoja yako hapo juu labda nisaidie kumjibia mleta uzi.

2. Hiyo miaka ya 2010 alivyokuwa anauza Ipad kama wali ulikuwa 1,000 tena chuoni, unashindwaje kuamini miaka 7 au 8 nyuma wali kuwa 200 kwenye canteen za shule za sekondari??

4. Mimi nimesoma Private School, tena hapahapa Dar yenye kila aina ya usimamizi na nidhamu. Lakini nilifanya biashara ya kuuza pipi (Ivory) na vyakula kama Sambusa na Chipsi kwa miaka mitatu kuanzia Form Two mpaka Form Four bila hata kushtukiwa. Ile shule ilikuwa ukiruka tu ukuta uingie mtaani wale wa mtaani iwe raia au hata walinzi wa shule wakikukamata na wakakupeleka shuleni wanalipwa laki moja cash (kwa kulisema hili nadhani waliosoma ile shule kama wapo hapa watakuwa wameijua) ila kwa mazingira hayohayo magumu mimi na biashara yangu ilisurvive kwa miaka mitatu na ilikuwa lazima hii mizigo ifuatwe nje na ije kuuzwa shuleni. Kuna mbinu nyingi sana nilikuwa natumia, nilinunua viongozi wa dormitories pamoja na maprefects ikiwemo Head Boy, nilijenga urafiki na Patrons ingawa hawakujua ninachofanya. Nilifanya hivyo makusudi ili wale spies directly wasiweze kuwa threat kwangu sababu walijua wakienda either kwa maprefects au Patrons kunichongea lazima habari zitanifikia. So kwa upande wa jamaa tena shule za serikali ambazo walimu wapo busy na mambo yao sidhani kama inashindikana jamaa alichokifanya.

Kitu kinachotenganisha utajiri na umaskini ni UTHUBUTU tu. Maskini wamekariri njia rahisi na salama kupata pesa ila matajiri ni tofauti. Maskini ni muoga, anaogopa kupoteza alichonacho, tajiri yeye plan yake anaangalia atachopata kwanza sio alichonacho mkononi.​
Point mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwamba anajua kunusa pesa , ila kwa miaka ya sasa hivi pesa ilivyokuwa ngumu unaweza kukuta hana maisha kabisa.
STORY YAKO INAFUNDISHA SANA MKUU.
 
Story inaweza kuwa chai lakini ukikosoanuwe na uhakika na hiyo taarifa unayoikosoa.
Halafu pasaka hii wacha watu wafurahi kidogo...
Anyway, kuna watu huwa wana mastory yao ya hivi kumbe wanataka kupiga watu nakumbuka story za forex za yule wa kudownload noti alianzia story zake tangu yupo tumboni hajazaliwa, vidudu, primary o level advance, jeshini chuo kumbe dah....majanga pia kuna wengine wanataka kushare experience.... mtu akipigwa si atajijua mwenyewe tuuu....
 
Kwanza nikupongeze kwa juhudi za kutafuta pesa toka O-Level,
Pili,ningependa kujua mwaka ulioingia chuoni na jina la Chuo ulichosoma ambacho kilikua na utaratibu kwa wanafunzi kwenda kuchukua Pesa za Boom kwa muhasibu badala ya kuwekewa kwenye account.

Udsm ilikuwa hivyo miaka mingi. Bumu la kwanza unapewa dirishani kwa mhasibu
 
Tumekula wali kwa 100 pale Mvomero kwa Mama Ombopa. Nimekunywa na kuuza soda kwenye mnada wa Mkongeni kwa soda Tsh 50. Mama yangu alikuwa anachoma vitumbua nami nikawa namuuzia kwa Tsh 5 then ikaja Tsh 10 huyo ya wali kuuzwa 200 ni kitu cha kawaida tena huo ulikuwa wali nyama.
Mkongeni dakawa hiyo
 
Kama ni haramu mbona benki hazifilisiki
Yes, i wanted to say that, game ya hela bana ni ishu tu ya kuwa makini na kujua kuicheza. Watu wanasema ni haramu kutoa jela kwa riba, kwan kuna mtu anamnyang'anya mtu hela si anachukua kwa hiari yake na shida zake? Benki zote zinapata faida kwa biashara hyo na kila anayechukua mkopo kama ana akili anatoboa na anarudisha riba ya watu.

so wanaosema ni biashara ya udhalimu ndo wale wanaoamini ile kauli kuwa money is a source of all evils, na huwez kuwa na hyo mentality af ukawa na hela, big noo

Dah wazee nataka hela ila tu nisimkabe au kumwibia mtu hahah
 
Back
Top Bottom