Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

Wakuu hii story pigieni mstari ndio imeishia hapa, alishawahi kuisimulia na haikuwa na wachangiaji lakini hakuimaliza. Kwaiyo fanyeni mambo mengine tu...

Aisee! Mumsamehe jamaa, labda atakuja na maelezo kuhusu hili. Binafsi huwa sipendi to jump to conclusion. Tumsubiri kwanza aje huenda akawa na maelezo mazuri ya kujustify hii kitu.
 
Nakumbuka ilikuwa mwaka 2012, Mara yangu ya kwanza kufika Beit Bridge, mpakani mwa Zimbabwe na South Africa, ilikuwa saa nane usiku. Ilikuwa safari ya siku tatu kutoka Dar hadi kufika hapo. Ndani ya bus tulikuwa tumechoka sana. Bus lilikuwa na raia wengi wa Zimbabwe na Zambia, Waburundi, Wakenya. Wabongo tulikuwa 4 tu. Wabongo tulipiga mastori kibao, kama watu tuliofahamiana miaka mingi, kumbe ndo ilikuwa mara yetu ya kwanza kukutana.

Tulijichanganya sana na Waburundi na Wakenya. Wazimbabwe hata lugha yao tulikuwa hatuelewi. Dah ilikuwa moment fulani tamu sana.

Pale border Mbongo mmoja hakuruhusiwa kuingia South Africa. Alikamatwa alitaka kutoa rushwa kwa Afisa wa Uhamiaji (Mkaburu) ili apewe miezi 3 ya kuishi kwa Madiba. Huyu mwenzetu aliyekamatwa yeye ilikuwa sio mara yake ya kwanza kuingia South Africa. Ujuaji mwingi ulimponza.

Sisi wengine tuligongewa muhuri wa mwezi 1 tu kuwepo kwa Madiba. Lakini tuliishi zaidi ya Miaka 6, Sio miezi 6, ni miaka 6. Harakati za mtu Mweusi bhana.

Nakumbuka Wabongo wote tulienda kufikia Pretoria kwa jamaa fulani. Kumbuka wote hapo hatujuani, halafu mfukoni nimebakiwa na kama Elfu 50 tu ya Kibongo.

Kati ya sisi tuliotoka Bongo, kuna mwenzetu mmoja anafamiana na huyo jamaa tuliyefikia kwake. Jamaa wa kuitwa Ibra, alitupokea vizuri sana.

Tulikutana na Wabongo kibao pale Pretoria, walituchukua maelezo, tulikutana mpaka na yule demu video queen wa Matonya, wimbo wa Vailet, demu South Africa bado wanamuita Vailet, bado mrembo sana.

Harakati za kuingia mtaani kusaka mishe ndo zikaanzia hapo.

Nilikaa pale ghetto kwa washkaji kama wiki mbili ivi, ndani ya hizi wiki mbili na jamaa zangu tulikuwa tunaenda sana Johannesburg. Mwenyeji wetu alikuwa na rafiki zake wengi huko. Johannesburg na Pretoria sio mbali sana, kwa daladala ni kama dakika 40 tu.

Basi bhana, katika kwenda kwenda Johannesburg siku mmoja kwenye daladala nikawa nimekaa na demu mmoja mkaliii, nikawa namsemesha semesha mara pap akanipa namba yake ya simu. Washkaji zangu wananichora tu.

Mademu wa South Africa wakitongozwa sio wagumu sana kama Dada zetu wa Sinza, siku ya pili demu akawa demu wangu, fasta tukaanza kupanga maisha. Ha ha ha ha

Demu anafanya kazi Bank FNB, pale Midrand njia kama unataka kuelekea Kalfonteen. Baada ya kama siku 4 toka tufahamiane na yule manzi tukaanza kupiga story za jinsi ndoa yetu itakavyokuwa. Jinsi atakavyokuja Bongo kukutana na ndugu zangu, alivyoleta tu stori zake za siku moja atakuja Bongo kukutana na ndugu zangu, mtu wa kwanza kumuwaza alikuwa Mama Riziki, Muuza Vitumbua, Jirani yetu Buza, atakavyoongea mtaa mzima.

Yaan mimi na yule demu ilikuwa ni full uongo uongo tu mpaka demu akajaa. Akaamini kabisa kama kweli mimi ntamuoa.

Zote hizo ni Harakati za Mtu mweusi katika kutafuta sehemu ya kuanzia. Mara siku akanipigia simu akaniambia kwa Kingereza 'Keagan nataka tuishi wote'

Dah

Wadau itaendelea na nyinyi kama mna mastory yenu wekeni hapa Harakati zenu tujifunze



Hii Stori inafanana na ile na haina Kanya wala Kinyesi

Bs tupu
 
Nakuhakikishia jamaa harudi tena, Mana story ya uongo balaa
Aisee! Mumsamehe jamaa, labda atakuja na maelezo kuhusu hili. Binafsi huwa sipendi to jump to conclusion. Tumsubiri kwanza aje huenda akawa na maelezo mazuri ya kujustify hii kitu.
 
Muulize yeye ameshawahi kuandika story yoyote hapa jukwaani??
Katulisha matango pori angalia link hiyo
[emoji1787][emoji38]
Fungua huo uzi hapo juu
[emoji56][emoji56][emoji56]
 
Aisee! Mumsamehe jamaa, labda atakuja na maelezo kuhusu hili. Binafsi huwa sipendi to jump to conclusion. Tumsubiri kwanza aje huenda akawa na maelezo mazuri ya kujustify hii kitu.
Anatufanya Watoto bhana anatunnywesha Chai huku anaringa.
 
SEHEMU YA TANO

Wakuu nitajitahidi kuandika kwa urefu na nitajitahidi kuandika kila kitu ili mtu mwengine aweze kujifunza kitu. Hata matukio yangu ya aibu pia nitawaeleza ili mtu ajifunze kitu kupitia story yangu na Kama kuna Makosa nilifanya basi iwe rahisi kwa mtu mwengine kujifunza na kurekebisha.

Nilivyorudi kwa yule Dada wa Uhamiaji, alifungua Passport yangu bila kusema chochote aligonga Mhuri nikaondoka zangu. Nikajua kumbe mwanzoni alisema vile ili kunitengenezea mazingira ya kutoa rushwa.

Nilivyotoka tu pale Kaunta, wale Vishoka wakanifuata ili niwarudishie ile Pesa yao, Kwacha 50. Kumbuka hapo nilikuwa bado sijabadili pesa za Kigeni. Nikawauliza wale Jamaa, Kwacha 50 ni sawa na shilingi ngapi za Kitanzania ili niwarudishie pesa yenu, wakaniambia "Wewe tupe Laki Moja tu"

Nikaona wananiletea Ujinga, nikatoka mpaka nje kwa Jamaa ambae alikuwa anawabadilishia watu fedha, Wale Vishoka wapo nyuma yangu tu. Nikataka kubadilisha Pesa yule Jamaa akakataa akasema "Malizana kwanza na hao Jamaa zako".

Nikamwambia kuhusu hawa Jamaa niachie Mimi, wewe nipe huduma tu ya Kubadilisha Pesa, Jamaa alikataa. Nikamwambia basi niambie Kwacha 50 ni sawa na shilingi ngapi za Kitanzania, Hata hilo nalo alikataa aliendelea kusema " Maliza kwanza na hao Jamaa".

Nikaondoka pale kurudi kwenye Bus ili nimuulize Dereva au Konda, Wale Vishoka wapo tu nyuma yangu. Dereva na Konda nao walikataa kutoa ushirikiano kwa madai ya kwamba nimalizane kwanza na wale Vishoka.

Hapo Vishoka wanatoa maneno yote ya Shombo. Lakini nilijifanya kama Siwasikii vile, mwisho wa siku nikawaambia oya nyie sikilizeni Mimi hiyo Laki Moja sina fanyeni mnachotaka kufanya. Tukaanza kuvutana vutana pale na kurushiana maneno. Abiria wengine wapo kimya wanatusikiliza tu.

Mwisho wa Mabishano nilikubali kuwapatia Elfu 50. Roho iliniuma sana. Nilijua fika hapa nimepigwa. Baadae nilikuja kujua kuwa Kwacha 50 ilikuwa kama Elfu Nane ya Kitanzania. Ndo hivyo nilishapigwa.

Baada ya wale Vishoka kushuka ndani ya Bus niliwauliza Dereva na Konda kwa nini walikataa kunisaidia. Wakaniambia kuwa wao ile njia wanapita kila siku na hao Vishoka wapo hapo Boda ya Tunduma miaka na miaka. Kwa hiyo kama wangenisaidia basi Bus lao lingefanya kazi katika Boda hiyo kwa tabu sana pengine wangeweza kutobolewa matairi kila watakapokuwa wanapita hapo. Kwa kweli niliwaelewa.

Aisee kumbe sikuwa peke yangu niliyepigwa usiku ule. Mara waliingia Abiria wengine na Vishoka wengine wakigombana kama ilivyokuwa kwangu. Moyoni nikasema hapa itakuwa kuna mchezo unachezwa kati ya Maafisa Uhamiaji na hawa Vishoka. Ndo mana wanaruhusiwa kuingia hadi ndani.

Tulilala ndani ya Bus hadi asubuhi ndo tukaendelea na safari ya kuelekea Zambia.
Kamalizie hii simulizi yako
 
SEHEMU YA TISA

Kwa ambao hawajafika South Afrika, Umbali kutoka Pretoria mpaka Joberg ni Kama Dakika 45 tu, Lakini Umbali kutoka Pretoria mpaka Capetown ni Masaa 24. Ni Mbali ndo mana Ahamad na Dada yake walitumia ndege.

Sikukaa sana pale kwa Vailet, Vailet aliniambia twende Mitaa wanayokaa Wabongo nikutafutie sehemu ya kuishi.

Kumbuka mpaka nafika hapo Pretoria nimesafiri siku 4, nimechoka sana. Sijawai kusafiri Umbali mrefu hivyo. Halafu mpaka muda huo nipo barabarani nazurura tu na Begi langu mgongoni.

Wakuu hapa ilipofika story yetu, kutokana na Harakati za Maisha na Biashara ambazo nilikuta watu wanafanya ambazo nitazieleza huko mbele, naomba sitotaja watu majina yao ya ukweli.Tukafika mpaka Mitaa fulani kuna Saloon nyingi, Vailet akamuita jamaa mmoja tumpe jina X, Nakumbuka akamwambia "X huyu jamaa ndo ameshuka hapa muda huu, naomba mtafutie sehemu ya kulala" alisema hivyo, wakapiga story kidogo halafu Vailet akasepa. Nikawa chini ya Mikono ya mtu mwengine.

Basi pale X akaanza wenyewe wanasema "Kunichukua Maelezo". Akaanza kuniuliza Dar natokea sehemu gan na maswali mengine mengi. Nikamjibu yote. Nilivyotaja sehemu niliyotokea hapa Dar kuwa ni Temeke, X akasema kuna watu kutoka Temeke kibao wako hapa. Ngoja nimpigie simu Jamaa mmoja wa Temeke akufate tena ndo utaishi kwake.

Alimpigia simu huyo jamaa, Jamaa akasema atanifuata. Mpaka inafika saa mbili usiku X anafunga Saloon yake huyo Jamaa bado alikuwa hajafika. X akafunga akasepa, akaniambia "Msubiri jamaa usiwe na wasiwasi atakuja tu" Nilipigwa na Baridi kwenye nchi ya watu mpaka Saa Sita usiku jamaa bado hajafika. Kumbuka hapo nimechoka ile mbaya. Inaingia siku ya Tano bila kulala Vizuri. Nina Usingizi Kinoma.
....
 
Huyu mleta uzi,kumbe muongo, inaonesha kweli amewahi kwenda lakini ukilinganisha story yake hiyo iliyofukunyuliwa na wadau, na hii ya sasa inaonesha wazi baadhi anatupanga si kweli kabisa.
 
Wakuu hii story pigieni mstari ndio imeishia hapa, alishawahi kuisimulia na haikuwa na wachangiaji lakini hakuimaliza. Kwaiyo fanyeni mambo mengine tu...

Na ametuweza kweli
 
Back
Top Bottom