Kama uliona utoto.mbona bado upo hapa??watu wengine.kujimwambafy tuneti utoto Sasa si upite kimya kimya kwani umeitwa.Wala hujasomq mpaka alipofika eti utoto na bado upo humu humu.Mie hata siwezag soma stry za kinamna hii najiona kama utoto..lol..so.uko interested balaa..nimesoma episod 3 nikaona utoto..sijui why!
Kaka Chirundu tumekupataWakuu tunaendelea Muda sio Mrefu, Mnisamehe Leo nitajitahid kuandika sana
Ni mwenyewe aliianzishaNakumbuka ilikuwa mwaka 2012, Mara yangu ya kwanza kufika Beit Bridge, mpakani mwa Zimbabwe na South Africa, ilikuwa saa nane usiku. Ilikuwa safari ya siku tatu kutoka Dar hadi kufika hapo. Ndani ya bus tulikuwa tumechoka sana. Bus lilikuwa na raia wengi wa Zimbabwe na Zambia, Waburundi, Wakenya. Wabongo tulikuwa 4 tu. Wabongo tulipiga mastori kibao, kama watu tuliofahamiana miaka mingi, kumbe ndo ilikuwa mara yetu ya kwanza kukutana.
Tulijichanganya sana na Waburundi na Wakenya. Wazimbabwe hata lugha yao tulikuwa hatuelewi. Dah ilikuwa moment fulani tamu sana.
Pale border Mbongo mmoja hakuruhusiwa kuingia South Africa. Alikamatwa alitaka kutoa rushwa kwa Afisa wa Uhamiaji (Mkaburu) ili apewe miezi 3 ya kuishi kwa Madiba. Huyu mwenzetu aliyekamatwa yeye ilikuwa sio mara yake ya kwanza kuingia South Africa. Ujuaji mwingi ulimponza.
Sisi wengine tuligongewa muhuri wa mwezi 1 tu kuwepo kwa Madiba. Lakini tuliishi zaidi ya Miaka 6, Sio miezi 6, ni miaka 6. Harakati za mtu Mweusi bhana.
Nakumbuka Wabongo wote tulienda kufikia Pretoria kwa jamaa fulani. Kumbuka wote hapo hatujuani, halafu mfukoni nimebakiwa na kama Elfu 50 tu ya Kibongo.
Kati ya sisi tuliotoka Bongo, kuna mwenzetu mmoja anafamiana na huyo jamaa tuliyefikia kwake. Jamaa wa kuitwa Ibra, alitupokea vizuri sana.
Tulikutana na Wabongo kibao pale Pretoria, walituchukua maelezo, tulikutana mpaka na yule demu video queen wa Matonya, wimbo wa Vailet, demu South Africa bado wanamuita Vailet, bado mrembo sana.
Harakati za kuingia mtaani kusaka mishe ndo zikaanzia hapo.
Nilikaa pale ghetto kwa washkaji kama wiki mbili ivi, ndani ya hizi wiki mbili na jamaa zangu tulikuwa tunaenda sana Johannesburg. Mwenyeji wetu alikuwa na rafiki zake wengi huko. Johannesburg na Pretoria sio mbali sana, kwa daladala ni kama dakika 40 tu.
Basi bhana, katika kwenda kwenda Johannesburg siku mmoja kwenye daladala nikawa nimekaa na demu mmoja mkaliii, nikawa namsemesha semesha mara pap akanipa namba yake ya simu. Washkaji zangu wananichora tu.
Mademu wa South Africa wakitongozwa sio wagumu sana kama Dada zetu wa Sinza, siku ya pili demu akawa demu wangu, fasta tukaanza kupanga maisha. Ha ha ha ha
Demu anafanya kazi Bank FNB, pale Midrand njia kama unataka kuelekea Kalfonteen. Baada ya kama siku 4 toka tufahamiane na yule manzi tukaanza kupiga story za jinsi ndoa yetu itakavyokuwa. Jinsi atakavyokuja Bongo kukutana na ndugu zangu, alivyoleta tu stori zake za siku moja atakuja Bongo kukutana na ndugu zangu, mtu wa kwanza kumuwaza alikuwa Mama Riziki, Muuza Vitumbua, Jirani yetu Buza, atakavyoongea mtaa mzima.
Yaan mimi na yule demu ilikuwa ni full uongo uongo tu mpaka demu akajaa. Akaamini kabisa kama kweli mimi ntamuoa.
Zote hizo ni Harakati za Mtu mweusi katika kutafuta sehemu ya kuanzia. Mara siku akanipigia simu akaniambia kwa Kingereza 'Keagan nataka tuishi wote'
Dah
Wadau itaendelea na nyinyi kama mna mastory yenu wekeni hapa Harakati zenu tujifunze
Hii Stori inafanana na haina Kanya wala Kinyesi
Bs tupu
Aliianzisha on 15 april naona ikabuma akaja na hii mpya ya akina Kanya hio ya kwanza anadai yule muuza ngada ni Ibra halafu anasema yeye ni Muisilamu na alienda kanisani kujifanya ni mkristo hata huwezi kujua kipi kipi Bs tu yaani.Ni mwenyewe aliianzisha
Watu washafukua kaburi kilichobaki ni kuchange ID kwishneiWakuu hii story pigieni mstari ndio imeishia hapa, alishawahi kuisimulia na haikuwa na wachangiaji lakini hakuimaliza. Kwaiyo fanyeni mambo mengine tu...
Uzi maalum wa Harakati za kutafuta maisha nje ya nchi na changamoto ulizokutana nazo
Nakumbuka ilikuwa mwaka 2012, Mara yangu ya kwanza kufika Beit Bridge, mpakani mwa Zimbabwe na South Africa, ilikuwa saa nane usiku. Ilikuwa safari ya siku tatu kutoka Dar hadi kufika hapo. Ndani ya bus tulikuwa tumechoka sana. Bus lilikuwa na raia wengi wa Zimbabwe na Zambia, Waburundi...www.jamiiforums.com
Aliyekuambia nasubiria episodes zake nan...mxiewKama uliona utoto.mbona bado upo hapa??watu wengine.kujimwambafy tuneti utoto Sasa si upite kimya kimya kwani umeitwa.Wala hujasomq mpaka alipofika eti utoto na bado upo humu humu.
Nan kafukuzw kazi mzee baba! Juic si ilikua miaka ya 2015 huko? Nimkimbie ili iweje? Uwe unasoma unaelewa..unaleta mambo ya nyuz zingine nikimbie niende wap...! Hebu soma vzr uwe unaelewa..nakimbia au nataka kutoa gunduNaona harufu mbaya hapa unataka kumkimbia jamaa sababu kafukuzwa kazi?
Kwani issue yako ya juice ofisini si inaendelea vizuri
Ghafla mmemgeuka..hahaaa wabongo nomaHalafu kumbe alikaa Mwezi Sauzi akarudi kula kulala kwao Buza
Kwenye ile Stori anawaponda akina Ibra kwa kupiga kazi kumbe yeye ni Kula kulala bure
Bora mtu akuambie ni Fiction ili uamue kusoma au Bando lako ulihamishie jukwaa lingineGhafla mmemgeuka..hahaaa wabongo noma
Sie wa Kwa Minchi na Donge tunaruhusiwa ku comment? 🤣 🤣 🤣 🤣Nipo sahare aisee wew wap?
Alafu wako very smart inaonyesha, unakuta blames nyingi wanaangushiwa wanaija kumbe ni wabongo wamesababisha.Hii ni kweli kwamba wabongo wengi ni wauza madawa South Africa
Mleta uzi hakuna sehemu ameandika kuhusu kurudi kwake usimuwekee maneno mdomoniHalafu kumbe alikaa Mwezi Sauzi akarudi kula kulala kwao Buza
Kwenye ile Stori anawaponda akina Ibra kwa kupiga kazi kumbe yeye ni Kula kulala bure
Ah wapi..mnamhukumu mno...mie nataka jua alitusua? Kama karudi bongo🙄!Bora mtu akuambie ni Fiction ili uamue kusoma au Bando lako ulihamishie jukwaa lingine
Endeleza story mkuu...First attempt ya kujilipua ilikuwa United States ...akiwa Nigeria Ila hakufanikiwa..
Anadai Nigeria Hadi bank statements wanakughushia .. Akiwa ubalozini alikamilisha kila kitu ...kufika dirishani akaulizwa kuhusu invitation letter Akawa hajui Ni nini anajiuma uma tuu ..wakamweka ndani ..Kama gaidi...wakamuuliza do you want/like coffee akasema yes wakamuuliza upo hatiani hiyo nguvu/gut ya kunywa coffee unaitoa wapi lastly aliamua kuzungumza ukweli juu ya ugumu wa maisha wakamwambia afuate procedures vizuri ndo aende ...wazungu wakabaki wanacheka ..baada ya kumchukua maelezo na kujiridhisha wakamwachia
Jana kuna Mbongo kachoma Chuo kikuu cha Cape TownAlafu wako very smart inaonyesha, unakuta blames nyingi wanaangushiwa wanaija kumbe ni wabongo wamesababisha.